amos eglan
JF-Expert Member
- Sep 27, 2015
- 310
- 464
Ndugu zangu, habari za muda huu!
Nawasilisha Uzi huu kutaka kujua sintofahamu juu ya pesa walizochangia wananchi kuhusu maafa ya tetemeko la Kagera maana watu bado wanateseka wanalala nje wakipigwa na baridi ilhali watanzania wenzao walijinyima kuwasaidia.
Sasa mpaka muda huu sijaelewa ni kwanini pesa hazijawafikia na wakati ni swala la dharura ili bidi iwafikie punde wananchi hao waliofikwa na tetemeko au wanafanyiwa uhakiki.
Kwa hali hii wananchi watashindwa kusaidia wenzao pindi wanapofikwa na maafa maana hawatakuwa na imani juu ya uwasilishwaji wa msaada.
Kwa sababu haujatoka serikalini bali ni utu wa wazalendo au kuna siasa katika hili? Mwananchi mmoja aliongea kwa masikitiko eti anaambiwa anza kujenga kwanza ukifika juu tutakusaidia kweli jamani.
Nawasilisha Uzi huu kutaka kujua sintofahamu juu ya pesa walizochangia wananchi kuhusu maafa ya tetemeko la Kagera maana watu bado wanateseka wanalala nje wakipigwa na baridi ilhali watanzania wenzao walijinyima kuwasaidia.
Sasa mpaka muda huu sijaelewa ni kwanini pesa hazijawafikia na wakati ni swala la dharura ili bidi iwafikie punde wananchi hao waliofikwa na tetemeko au wanafanyiwa uhakiki.
Kwa hali hii wananchi watashindwa kusaidia wenzao pindi wanapofikwa na maafa maana hawatakuwa na imani juu ya uwasilishwaji wa msaada.
Kwa sababu haujatoka serikalini bali ni utu wa wazalendo au kuna siasa katika hili? Mwananchi mmoja aliongea kwa masikitiko eti anaambiwa anza kujenga kwanza ukifika juu tutakusaidia kweli jamani.