Sioni ubaya kwa serikali kuelekeza baadhi ya fedha za maafa kwenye taasisi nyingine za kiserikali

Tume ya Katiba

JF-Expert Member
Apr 6, 2012
4,896
1,862
Nianze tu kwa kuwapa pole wahanga wa tetemeko la KAGERA, mpate nguvu za kusimama na kuendelea na shughuli nyingine za ujenzi wa Taifa.

Nije kwenye mada, Kumekuwepo na wachangiaji wengi kwenye mitandao ya kijamii, na vyombo vingine wakiponda msimamo wa serikali kuelekeza pesa za Maafa ya kagera kwenye shughuli nyengine za kiserikali, binafsi kwa maoni yangu ni kuwa sioni ubaya kwa serikali kuelekeza pesa kwenye shughuli nyingine za maendeleo kwa sababu zifuatazo.

Kwanza watu watambue kwamba lengo kuu la pesa zile ni kuyarejesha maisha ya waathirika katika hali zao za kawaida kama ilivyokuwa kabla ya kukumbwa na shida ile, Mfano yule aliyebomokea na nyumba kuijenga, aliyeharibilkiwa mazao shambani kumuwezesha kama mbegu na pembejeo, aliye patwa na msiba ni kumliwaza kwa kuwa nae na michango midogo midogo, si lengo la michango ile kuwatajirisha wahanga au kuwajaza mapesa ...HAPANA. Si lengo la michango ile kuifanya kagera kuwa DUBAI...HAPANA.

Kwa Mtazamo wangu, ikiwa lengo hili limekamilika, pesa inaweza kuelekezwa sehemu nyingine yoyote ikiwemo kuboresha maeneo mengine yenye hatari ya kukumbwa na jaga kama lile, au eneo lolote lenye manufaa ya ujumla kwa jamii.

Kwa muktadha huu basi, ikiwa pesa zilizochangwa zimevuka lengo kuu la awali la kurejesha maisha ya waathirika katika hali yao ya kawaida sioni ubaya kwa ziada ya pesa zile kuelekezwa kuboresha miundombinu mingine ya serikali ambayo itakuwa ni kwa faida ya jamii yote kwa ujumla wakiwemo waathirika wa tetemeko.

Kitendo chochote cha kutaka kutafunwa pesa zote na wana kagera nakichukulia kama ni kitendo cha ubinafsi na ukosefu wa uzalendo.

Tusijenge tabia ya kupinga kila kitu jamani.

Nitoe lawama zangu kwa wasaidizi wa JPM kwa kuacha upotoshaji huu kunawiri.

Kwa hili nipo pamoja na JPM.

Asante

Tume ya katiba
(Mtaalamu wa mifumo ya komputer na Mtakwimu anayeishi UHAMISHONI.)
 
Toka huko uhamishoni rudi nyumbani uje usaidie wahanga wa tetemeko.
Tumesaidiwa tumeshindwa kusaidika acha mungu atuadhibu kwa mkono wake mwenyewe
 
Mkuu ulichokisema hapa ni sahihi kabsa....Hata mimi jana nilileta uzi humu ndani juu ya hili swala....nikawauliza Wenye ushaidi wa matumizi ya sivyo ndivyo juu ya hizi pesa walete ushaidi hapa nilikuwa na maana ya kwamba si kweli HIZI pesa zimetumika nje ya mkoa husika ama nje ya lengo husika...PESA ZOTE ZINAELEKEZWA HUKO KAGERA kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu na huduma muhimu..na IKIWEZEKANA kuanzisha HUDUMA nyingne ambazo ni muhimu LAKINI SI kuwajengea WAHANGA nyumba...Hapa kinachotakiwa kuangalia kwa jicho la ziada ni MAKUNDI MAALUMU ndio yapewe kipaumbele juu ya MAKAZI yao LAKINI SI WAHANGA WOTE au jambo la muhimu kabsa ni kuiomba serikali kuondoa kodi kwenye VIFAA VYA UJENZI ili bei iwe nafuu kwa hawa WAHANGA.....sasa hawa WENZETU wa UPINZANI UCHWARA wao ndio wamepata PAKUTOKEA JUU YA HILI maana NI WATU WA MATUKIO KWELI SIKU HIZI......TUSISHANGAE KESHO WAKAHIMIZA MAANDAMANO NCHI NZIMA kupitia hili....
 
Yaani hapa ndio umeharibu kabisa Tume ya Katiba. Kwamba waadhirika wa tetemeko walishapata misaada ya kutosha sasa eti ielekezwe kwingine. Unaamini kabisa kwamba maisha ya waadhirika wote yamerudi katika hali ya kawaida? Hivi watu wengine mkoje?
Hata hivyo pesa iliyochangwa kusaidia watu wa kagera eti ipelekwe kigoma au mwanza? Au eti wabunge wa ccm wagawane? Yoy must be insane!
 
S
Mkuu ulichokisema hapa ni sahihi kabsa....Hata mimi jana nilileta uzi humu ndani juu ya hili swala....nikawauliza Wenye ushaidi wa matumizi ya sivyo ndivyo juu ya hizi pesa walete ushaidi hapa nilikuwa na maana ya kwamba si kweli HIZI pesa zimetumika nje ya mkoa husika ama nje ya lengo husika...PESA ZOTE ZINAELEKEZWA HUKO KAGERA kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu na huduma muhimu..na IKIWEZEKANA kuanzisha HUDUMA nyingne ambazo ni muhimu LAKINI SI kuwajengea WAHANGA nyumba...Hapa kinachotakiwa kuangalia kwa jicho la ziada ni MAKUNDI MAALUMU ndio yapewe kipaumbele juu ya MAKAZI yao LAKINI SI WAHANGA WOTE.....sasa hawa WENZETU wa UPINZANI UCHWARA wao ndio wamepata PAKUTOKEA JUU YA HILI maana NI WATU WA MATUKIO KWELI SIKU HIZI......
Sasa kwa nini hilo jicho la ziada halikuyaona hayo mpaka watubwapige kelele?
 
Kama ni ziada imepatikana ni sawa, lakini kama walengwa ambao picha, takwimu na sura zao zilitumika kumobilize funds wanaambiwa fedha zimetumika mahali pengine na kwamba wao waliolengwa wajihudumie/wajenge majumba yao kwa fedha zao hapo kuna shida. Hakuna tofauti na NGO inayopelekea picha za waathirika wa UKIMWI kwa wafadhili halafu fedha zikiletwa wanatumia kujengwa majengo ya kifahari ambayo hayawanufaishi waengwa.
 
Back
Top Bottom