Fao la Kujitoa: Maoni ushauri na maono

CHA The GREAT

JF-Expert Member
Nov 11, 2010
651
853
Kwa muda mrefu, kumekuwepo zuio la kujitoa kwenye mifuko ya jamii maarufu kama 'fao la kujitoa'.

Sababu zimekuwa kwamba, ni utekelezaji wa sheria ya mifuko ya hifadhi ya jamii na ile ya SSRA.

Hapo mwanzo, kabla ya tarehe 11-Mei-2016, ilikuwa mtu akiacha kazi au kupoteza ajira, basi alikuwa anaenda kujitoa kwa maana ya kuchukua michango yake yote.

Zuio la kujitoa limekuwa mjadala mpana na ambao haujaisha hadi hivi sasa. Nimekuwa nikifuatilia hili kwa kuwa mimi pia ni mhanga mkubwa. Na taarifa zilizopo hivi sasa ni kuwa, serikali imekuja na 'fao la kukosa ajira' kama mbadala wa 'fao la kujitoa'.

Taarifa hiyo, haijaeleza kwa kina mbadala huo wa 'fao la kukosa ajira' ukoje. Wapo wanaodai kuwa, mtu aliyepoteza ajira atalipwa 30% ya mshahara wake kwa miezi 6, lakini hakuna conclusion ya baada ya miezi sita kuisha bila mtu kuwa na ajira au kupata ajira itakuaje.

Maoni yangu na maoni ya wengi kuhusu hili suala ni kurejeshwa fao la kujitoa kwa sababu zifuatazo.

1. Ajira (hasa sekta binafsi) si za uhakika na hazina security. Leo ni mfanyakazi kesho umemkosea bosi kwa kupiga chafya tu mbele yake basi ajira hauna.

2. Mishahara kwenye sekta binafsi, ukweli ni kwamba ni midogo mno. Ni midogo kiasi kwamba hakuna mtu mzima anaweza kuweka akiba kwa mishahara hiyo. Kwa mazingira kama haya, ikitokea mtu kapoteza ajira kutokana na mazingira yaliyopo, ukweli ni kwamba mtu huyo aliyepoteza ajira atakuwa na wakati mgumu. Hatoweza kuanzisha hata biashara ya mtaji wa laki moja tu.

Angalizo: Siku zote sheria (kwa uelewa wangu mdogo) huanzishwa kama makubaliano ya jamii yote kwa ujumla. Sheria huanzishwa ili kukidhi mahitaji ya jamii husika, kwa maana hii ni lazima kuwepo makubaliano kwa wahusika ama wadau wakuu. Sheria kuanzishwa bila makubaliano kwa wahusika wakuu ni utengenezaji wa mgogoro.

Kila nikisoma maoni kuhusu hili suala la mafao kupitia social medium, nagundua jambo moja kuu; kwamba wahusika wakuu au wadau wakuu ambao ni wafanyakazi na wanachama wa mifuko ya jamii hawakuhusishwa, huo ndiyo ukweli--hata mimi ninayeandika haya sijahusishwa. Nachukua nafasi hii kusema kuwa, suala la fao la kujitoa lazima lizingatiwe kwa umuhimu wake, wadau wakuu wahusishwe na kusikilizwa na si kama ilivyo hivi kwa hivi sasa.

Wenu katika uhuru wa kutoa maoni.
 
Mifuko ya jamii ni pyramid scheme..kama hamna ajira huwezi kujitoa,mana hela inakua haipo ya kukupa,wewe unayetoka unalipwa hela ya anayeingia
 
NSSF hela wanatoa...ila upige fitna na makarateka aka rushwa
Ndugu yangu, hiyo back door mpaka lini? Na kwa nini back door wakati haki ni yako. Are you for it? Ok, sawa NSSF wanatoa, vipi kuhusu PPF ambao wao hadi sasa wanasumbua. Think BIG.
 
Mifuko ya jamii ni pyramid scheme..kama hamna ajira huwezi kujitoa,mana hela inakua haipo ya kukupa,wewe unayetoka unalipwa hela ya anayeingia

Nini maana ya uwepo wa mifuko ya jamii, kwa mfano?
 
Serikali yetu wenyewe na inatutesa wenyewe.. Hivi hawajui usawa huu mtu ukiachishwa kazi ndio hupati tena? Hawa watu ni vilaza hasa
 
Tutaumia wengi sana.

Serikali iwe na huruma, wabunge wawe na huruma.

.......
 
Kutumia retirement/ pension fund kama unemployment benefit ni wazo litakalosababisha matatizosana wakati watu watakapofikakuda wa kustaafu halafu washakula mafao yote.
 
Issue ipo hivi:

Hilo fao linaanzishwa na linawakuta watu tayari wameshaachishwa kazi na hawajapewa fao la kujitoa, je hao nao wataanza kulipwa au hao haliwahusu?
 
Issue ipo hivi:

Hilo fao linaanzishwa na linawakuta watu tayari wameshaachishwa kazi na hawajapewa fao la kujitoa, je hao nao wataanza kulipwa au hao haliwahusu?
Mfumo mzima wa ajira afrika ni mbovu sasa wanachokifanya ni upuuzi kama wa mugabe kumwachia urais mkewe
 
Africa hovyo sana .... ShitHoles Countries !!! ...watakuja watu hapa eti mbona ulaya watu hawajitoi.....Unaanzaje kufananisha Ulaya na African hususan linchi la ovyo ovyo kama Tanzania?
 
Wapunguze PAYE ni makubwa mno, hizo asilimia watakazopunguza ziingie kwenye account ya mhusika kama fao lake, wapunguze pia makato ya mafao kwa sasa kwani ni makubwa pia na asilimia zake zichanganywe na zile za PAYE na mhusika atunziwe kama wafanyavyo kwa jina la Fao la kujitoa, akiacha au kuachishwa kazi na akizitaka achukue hela zake..

Mwisho wa siku kwenye salary slip isomeke, PAYE, FAO LA KUJITOA, PENSION FUND.
 
Kwanza mi huwa najiuliza maswali na sipati majibu,

Hivi hawa viumbe wanao jiita viongozi,wenye kujilazimisha kutuhudumia eti wanatujali,,,nani kawaambia kuwa ni lazima wateseke kwa ajili yetu?

Si watufuate watuulize tunacho taka,badala ya kuamua kwa niaba yetu,huku maamuzi wanayo fanya ni ya kitoto na kutudhalilisha!
 
Haya mambo kuyapatia muafaka na jamii ikaridhika inahitajika akili kubwa sana na sio akili hii tuliyonayo na kuitegemea..

Research kubwa sana inahitajika kwenye hili suala tena bila unafiki kuliko hivi linavyochukuliwa kirahisi, jamii ya kitanzania ina hitaji sana hili fao la kujitoa kuliko hadithi wanazo jaribu kuzitengeneza..

Hili suala linahitaji nguvu ya umma na si kutegemea akili za wale jamaa mjengoni, akili ya kumtetea mtanzania wa kawaida au mfanyakazi alielemewa na mzigo haipo Tanzania, ni nguvu ya pamoja kwa wafanyakazi ndio nusuru pekee..
 
Hii Serikali ya washamba na malimbukeni kama alivyosema zitto inadhulumu sana watumishi
 
INASIKITISHA,INAUMA,INANY'ONG'ONYESHA KWA SISI WAZALENDO,INA DISCOURAGE, INAHUZUNISHA,INAKERA, yaani mtu anataka fao lake kwa sababu yeye hana ajira ,documents ya termination zipo kutoka kwa mwajiri halafu ukifika Nssf eti mtu anakuambia andika maombi ya kuomba mafao, pesa zangu halafu niziombe tena ndio maana tunaitwa SHITHOLE pambafu sana, HIVI HIZO SUKARI ZITAKAPOZALISHWA SISI TUTAKUWA NA HISA ZA KIWANDA AU
VILE VIWANJA WANAVYOVITANGAZA WATUKOPESHE BASI SISI WENYE MAFAO KULE NSSF.
 
Tatizo watanzania wengi si wafuatiliaji wa mambo,ila kwa mtu unayefuatlilia unaweza kuona jinsi gani hili swala kwa sasa haliwezekani kujitoa,hata kama likiwezekana basi yatakuwa madeni tu maana kiuhalisia hela za kulipa mafao hazipo....hii mifuko ni chimbo la mafisadi kuchota hela,then hii mifuko ili kuhadaa watu inakua inajenga majengo kama vitega uchumi ambavyo navyo ni chimbo la kichota hela,sababu kama lile jengo limejengwa kwa hela zako jiulize wewe unanufaika vipi na lile jengo..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom