Fanya yote ila usimzalie mtoto huyo mwanaume!

Fanya yote ila usimzalie mtoto huyo mwanaume!

Binti wa zamani

Platinum Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
11,763
Reaction score
27,152
Mabinti, hasa nyie wadogo wa alfu mbili, hata akuambiaje, Usijichanganye kumzalia mtoto.
  1. Hakuna jukumu kubwa kwenye maisha zaidi ya kuzaa na kulea watoto. Mwanaume akikuambia bado hayuko tayari kukuoa ila anataka umzalie, huyo ni tapeli kama matapeli wengine tu.

  2. Kama huna kipato cha kueleweka usizae kiholela. Na ukiolewa, hakikisha una shughuli ya kiuchumi ya kukuwezesha kuhudumia watoto wako ikitokea amekutelekeza, mmeachana au bahati mbaya amefariki.

  3. Mapenzi kunoga na ahadi za kukuoa siyo sababu ya kubeba mimba. Wanaume wasio wababaifu, wenye kujua nafasi yao kwenye malezi wamebaki wachache sana ni kama bahati nasibu (Rejea hoja No 1 & 2).

  4. Zaa kwa ajili yako pale utakapokua tayari kiuchumi, kiakili na kimwili. Usizae ili uolewe au ili umtulize mwanaume, fahamu kuwa jukumu la malezi kwa kiasi kikubwa ni lako kama mama na yakitokea matatizo, atakayehangaika na mtoto / watoto ni wewe.

  5. Tumia uzazi wa mpango kuepuka mimba zisizotarajiwa kama hutaki basi tumia Kalenda au Condom (Kama hujui namna ya kujikinga kwa kutumia kalenda njoo hapa wamama tukusaidie na tukuelimishe.)

Ukitaka kujua huyo baba watoto wako mtarajiwa atakuwaje mkikosana na mna mtoto nenda kasome replies za wababa kwenye uzi wa jana wa waziri Dkt. Gwajima D - Jamii tuzungumze kuhusu baadhi ya wababa na matunzo kwa watoto - humo wamefunguka bila kuficha makucha yao.


Usiwe kama kenge mpaka uvuje damu ndiyo usikie - USIMZALIE BILA NDOA au UHAKIKA WA KUWEZA KUHUDUMIA MWANAO PEKE YAKO BILA YEYE.

Ni hayo tu, siku njema kwenu!


********
Naomba mtoe neno kwenye hili Lamomy , Leejay49 , nakwede97 , Demi , Aaliyyah , Mamndenyi , Bantu Lady , Ms R , leo dada , Numbisa , cocochanel , cocastic , Evelyn Salt , ephen_

Cc:
Wanawake wa JF:

waifu material * Mallerina
Atoto * Sister Abigail
realMamyQashy LilithTo yeye
MsweetChujio * Palina
Anastasia21 * ledadaCarleen * Midekoo
Mama Mwana * Hornet
SweetyCandyEllerie Bexley
Donatila *Jackcharty * Kelsea * Braying * Mrs Byesige
 
Hii reply ya leo dada naipin📌 hapa wasichana / wanawake wote muione.

📌📌
Kwangu mimi Nina mtazamo wa tofauti kidogo na nina misimamo yangu .......

Binti au mwanamke kwanza zaa ukiwa tayari ukihisi na kujua kabisa kwamba uko tayari kuzaa na kubeba majukumu bila kusumbua watu.....
Hapa namaanisha si kuzaa tu kufurahisha jamii, au unazaa kufurahisha bwana, au unazaa ili asikuache. Zaa ukiwa tayari na ukijua kabisa kwamba ukishazaa maisha yanabadilika completely jukumu kwa asilimia kubwa ni lako hata kama baba atahudumia fedha kaa ukijua kwa asilimia kubwa ya malezi yanakutegemea wewe mwenyewe.

Hawa wanaume hubadilika pindi mwanamke akizaa sababu ni nyingi mojawapo ni;

1. Malezi
Ukisha zaa malezi yanakutegemea hata kama tutapata dada wa kazi lakini ni lazima uwajibike hasa mtoto akiwa mdogo.

2. Usafi
Hapa ukisha zaa mwanamke kwanza Kuna kiharufu cha uzazi hili kuisha huchukua muda kidogo. Na harufu ya mtoto hii pia huchukua muda japo huisha lakini.

3. Huruma.
Baada ya kuzaa baadhi ya wanaume huona huruma na kuamua kuwa na mpango wa kando kipindi ambacho mwanamke ana uzazi au malezi. Sasa huruma hugeuka shubiri kwenye mahusiano kwani mwanaume anaweza kuzama huko mpaka ndoa au mahusiano kuvunjika.

4. Mabadiliko.
Mwanamke akishazaa Kuna mabadiliko hutokea na wengi kuanzia mabadiliko ya mwili, unene, ziwa kulegea, alama yaani stretch mark, urembo kwa baadhi ya wanawake kupungua na kupelekea mwanaume kukuona tofauti.

Sasa hapa binti/ mdogo wangu utakapo pata mtoto bila kuwa tayari utateseka sanaaa. Sababu utayari utakupa uvumilivu kuweza kuvumilia mabadiliko ya mtoto/ watoto kwani kila kitu kina raha na karaha zake.......

Ni vyema sana kuzaa ukiwa ndani ya ndoa kwani mwanaume anaweza kupokea mabadiliko na mkaweza kulea kwa amani na kufurahia uzao wenu.
Binti watoto changamoto na uzazi una changamoto nyingii mno usikubali kuwa single mother kirahisi ikitokea sawa.

Na binti kumbuka kuzaa sio lazima na kuolewa sio lazima.

Usiweke mitego ya kuolewa kwa kuwa wewe unataka kuolewa. Au kwa kuwa wewe ni jobless mwenzio anakazi ujitege either kwa mimba au madawa au kivyovyote ujifanye malaika dada hiyo ndoa utaachwa mchana kweupe na kubaki kuwa single mother na uanze kuona uchungu wa one hand.

Olewa na olewa na mtu ambaye Yuko tayari kwani akiwa tayari atakuvumilia kwa halisi zote na mabadiliko yote yatakayotokea kwenye maisha yenu.

Mimi sisapot mabinti kuzaa kwa fasheni, kuzaa wakiwa na umri mdogo , binti kuzaa kwa manufaa yake binafsi hilo suala anaye tumia zaidi ni binti.

Wanaume.
Hawa siwatetei na sina mengi ya kuongea juu yao kwa sababu.
Hakuna mwanaume anayeweza kupindua kwa mwanamke anayesimama katika nafasi yake na vitu vingi kwenye mahusiano hata ndoa kuwa imara inategemea mwanamke na nafasi yake alivyosimama.

Sasa wewe mpe utii, heshima , uvumilivu na upendo bila bila kusahau mizagamuano ya kutosha mpe mahaba mpe ufundi wako wote hata akipeleka kegeli zake huko nje kimoyoni akili kuwa wewe ndio kiboko yao.
Mpe utulivu mwanaume atatambua thamani yako na atakuthamini mengine yataenda bila kusahau maombi/ Dua kulingana na Imani yako maana Hawa kenge hawatabiliki.

Namalizia kwa kusema hivi nikiwa kama mama na kwenye ndoa nina miaka kumi na tatu.

Kuzaa sio lazima usizae kwa mihemuko eti kisa class mate zako wamezaa, sijui umri umeenda hapana kwa kweli maana huyo mtoto atakuwa nuksi tu kwako.

Na wale mabinti mlioko kwenye mahusiano na waume za watu au mahusiano ya muda mrefu eti mwanaume hataki ndoa anataka mzae kataa na usikubali na ukikubali hakikisha anakujengea na kukupa mradi endelevu utakaokuwezesha kulea na kusomesha mwanae haiwezekani binti usijaribu kubeba mizigo peke yako.

Mahusiano ni starehe na si karaha sasa kama ni starehe binti furahia na ikikuchosha acha sio lazima na hakikisha unachagua mtu sahihi wa kustarehe nae sio kila mtu. Usisahau mwili wako ni hekalu na hekaluni kunakaa vitu visafi na vitakatifu

Ndoa sio lazima olewa ukiwa tayari na si kwa sababu maana hizo sababu zikikosena ni lazima ndoa ivunjike.


Binti wa zamani yangu ni hayo.

📌📌

 
Wanawake sijui huwa mna akili za namna gani asee, sasa wewe unaona ndoa ndio kitu kinachoweza kumzuia mwanaume fedhuli asiyejali majukumu yake kukuletea mapicha picha hapo mbele??!!! No wonder mkiingia kwenye ndoa huwa mnaanza kuota mapembe kwa kuona mmemaliza yote, na hapa ndio wanaume na sisi tunawonyesha kuwa huu mchezo hauhitaji hasira.

Hapa ndio huwa naona nilichukua uamuzi sahihi wakuachana na masuala ya kutaka kuoa, kuoa kwa enzi hizi ni sawa na kufuga kijini kidogo ndani yako kinacho kuangamiza taratibu. Unaingia kwenye ndoa na mtua anayewaza 'Je ukifariki' huu ni ushetani wa hali ya juu sana
 
Hahaha kwani NDOA ndio nini?

Kuna watu wanatambulishwa kila siku kwao mwanamke mpya na wana wachumba zaidi ya 10 na wanazalishwa wote.

Kama umechoka wanaume pumzika tu.

Mwanamke akiniambia anitambulishe ndiyo anikubali nakwenda, nikitest nikakuta Litimus inakuwa Nyeusi nasepa, siyo dhambi.

Wewe unavigezo nami nina vigezo.
 
Hawa wanaume wa siku hizi ni .......................................................... (wape jina unalofikiri na linawafaa)
Mabinti, hasa nyie wadogo wa alfu mbili, hata akuambiaje, Usijichanganye kumzalia mtoto.
  1. Hakuna jukumu kubwa kwenye maisha zaidi ya kuzaa na kulea watoto. Mwanaume akikuambia bado hayuko tayari kukuoa ila anataka umzalie, huyo ni tapeli kama matapeli wengine tu.

  2. Kama hajaja kwenu kukuchumbia, hajakuoa usizae kiholela. Na ukiolewa, hakikisha una shughuli ya kiuchumi ya kukuwezesha kuhudumia watoto wako ikitokea amefariki, amekutelekeza au mmeachana.

  3. Mapenzi kunoga na ahadi za kukuoa siyo sababu ya kubeba tumbo hilo. Wanaume wasio wababaifu, wenye kujua nafasi yao kwenye malezi wamebaki wachache sana ni kama bahati nasibu (Rejea hoja No 1).

  4. Tumia uzazi wa mpango kuepuka mimba zisizotarajiwa kama hutaki basi tumia Kalenda au Condom (Kama hujui namna ya kujikinga kwa kutumia kalenda njoo hapa wamama tukusaidie na tukuelimishe.)

Ukitaka kujua huyo baba watoto wako mtarajiwa atakuwaje mkikosana na mna mtoto nenda kasome replies za wababa kwenye uzi wa jana wa waziri Dkt. Gwajima D Jamii tuzungumze kuhusu baadhi ya wababa na matunzo kwa watoto - humu wamefunguka bila kuficha makucha yao.


Usiwe kama kenge mpaka uvuje damu ndiyo usikie - USIMZALIE BILA NDOA.
Ni hayo tu, siku njema kwenu!


********
Naomba mtoe neno kwenye hili Lamomy , Leejay49 , nakwede97 , Demi , Aaliyyah , Bantu Lady , Ms R , leo dada , Numbisa , cocochanel , cocastic , Evelyn Salt , ephen_
Check movie inaitwa STRAW.
 
Waambie kwanza wajitegemee kiuchumi.
Unataka mwanaume akulipie kodi, akupe pocket money na mahitaji yako yote,
unadhani akija kusema umzalie utaanzia wapi kukataa?
Nimewaambia hapo juu, hebu soma tena!
Ila kwa msisitizo: mwanamke kuwa mtegemezi au omba omba kwa wanaume ni aibu na ujinga!
 
Back
Top Bottom