Fangasi sugu sehemu za siri

Fangasi sugu sehemu za siri

Habari great minds,
Nina tatizo la fangasi sugu sehemu za siri kwa miaka zaidi ya 4, huwa linanisumbua miwasho japo kuna muda linapungua na kupotea.

Nimeshatumia kila aina ya dawa zikiwemo za kupaka na kumeza, na kufuata maelekezo yote lakini tatizo bado lipo.

Kwa mikoa niliyokuwa naishi Mwanza tatizo lilikuwa la kuja kwa muda na kupungua hadi kupotea kwa mda kutokana na msimu.

Lakini kwa sasa nipo Dar tatizo limekuwa kubwa sana hadi kuleta michubuko ya ngozi sehemu za siri hii kutokana na joto kali,

Naombeni kwa aliyewahi kupatwa na fangasi sugu na akapona kwa dawa zingine tofauti na za kumeza na kupata za hospitalini maana nimeenda hospitali nyingi zikiwemo za binafsi.

Naomba anisaidie niweze kupona maana kuna muda inanipa shida hadi kutembea.

Nashukuru sana.
Fungus sugu inaweza ikawa dalili ya upungufu wa kinga mwilini je ushawahi kupima vvu toka tatizo likupate?
 
Hiyo ndio dawa zingine atamaliza pesa muhimu awe amehakikisha kuvumilia kwa sekunde 3-5 baada ya hapo Kuna upepo mzuri utampuliza na muwasho utapotea kabisa baada ya masaa ataanza kubandua ngoz ambayo n useless iliokuwa inasababisha muwasho.

Muhimu ajikaze na ahakikishe amefunga mlango kama nyumba haina bord juu aangalie asije akarukia kenchi.

Muhimu ajikaze Dettol ya maji n msaada mkubwa wengi imewaokoa fast and clear na gharama nafuu matumizi siku chache
Sh ngp inauzwa!?
 
Fungas ni suala la kimazingira zaidi, kama unakaa maeneo yenye watu wengi na mna share choo basi hiyo hata utumie dawa gani ni ngumu kupona.

Kama unaweza, jaribu kukaa chumba cha self-contain uone kama kutakua na mabadiliko.

Wakati niko shule hayo mambo yalikua yakawaida sana, hadi kuna wati nilihisi pumbu zitaanguka
 
Nineumwa fungus 2 yrs shulen pugu sec na Mwaka MMOJA nyumban hiv nomepima sana sasahizi napiga pressure na mkojo yutiiiiiiiaiiiiii
 
Tunaomba picha picha picha tukukague vizuri Madaktari hizo fangasi zinaonekanaje tukusaidie km unaona aibu hapa tuma PM
Mhhh bro atume halafu ukute we mwnyw mwalimu tu huna u dokta wowote unataka kuangalia mbupu tu
 
Hapo kuna vitu vya kuzingatia vya nje kwanza
1. Usafi wa mwili kwa ujumla hasa maeneo husika
2. Uvaaji wa boxer zenye asili ya cotton 100%, na hapa nitapendekeza boxers zisizobana ili upate hewa.
Jambo linalofuata ni tiba ya ugonjwa wenyewe hapa kuna maelezo marefu maana kunakutibu ndani na nje, waweza ni PM.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom