Familia yateketea kwa ajali Msata

Familia yateketea kwa ajali Msata

Ajali ni ya kugongana au wamepiga mzinga wenyewe tu?

NB:Ajali zinazotokea wakati wa ku-overtake huwa mbaya sababu mtu unanyoosha goti mpaka mwisho ili msiumane,sasa hesabu zikishindikana inakuwa maafa!
 
Punguza povu mkuu. Jf ni mtandao wa kijamii kupashana habari za hapa na pale sio lazima kila mada uchangie. Ukiona hauwafahamu wahusika pita tu kila. Hata sie hatuwafahamu ila tumesikitika kupoteza watanzania wenzetu
Taarifa mngewapelekea wanaowafahamu huko makwao basi,sio mtuletee huku public tukiwahoji mnalia.
 
Nilikuwa hii nchi last month kutembea
Nikaamua kuendesha Gari mwenyewe ni ndani ya siku mbili niliacha na kutafuta dereva yaani kila ukifika unapokwenda unapaki na kuhema hasa kama ulikuwa unakimbia
Halafu waifu akawa anataka twende mikumi na watoto, mimi ndio dereva, nilipanda mzuka na makelele mpaka nilijishangaa….
 
#HABARI: Wanafamilia watano wa familia ya Francis Kaggi, wamefariki dunia baada ya kupata ajali, wakitoka kwenye maziko mkoani Tanga.

Taarifa iliyochapwa mitandaoni huku ikionesha wanafamilia hao, pamoja na ratiba ya mazishi, imewataja walifariki kuwa ni Francis Kaggi, na wanawe wanne Janemary Kaggi, Maria Kaggi, Joshua Kaggi, Elineema Kaggi.

Imeeleza kwamba, Mtoto wake wa pili alitarajia kuanza elimu yake ya juu Chuo Kikuu Ardhi (ARU), na wa kwanza wa kike alikuwa anafanya kazi mkoani Tabora na mdogo alikuwa anasoma shule ya awali.

Na mwingine alikuwa anafanya kazi Tanesco. Chanzo cha vifo ni ajali, wakitoka kumzika mama wa mumewe siku ya Alhamisi, na Jumapili walianza safari asubuhi, huku baba wa familia ambaye ni Francis, akiwa ni dereva wa gari hilo.

Inaelezwa mkewe Francis, pekee amenusurika ajalini, na dada wa kazi akiwa amelazwa chumba cha uangalizi maalum (ICU).
FB_IMG_1758083079349.jpg
 
Waafrika walivyo wajinga kwwnye msiba watasema mke amemroga mme afe ili achukue mali
Ikiwemo na wewe sababu umechangia wazo ....hata pole hamna kiongozi.....mungu amsaidie huyo mama wakati huu mgumu
 
Back
Top Bottom