Faini Tshs 300,000 kucheza pool table asubuhi

Faini Tshs 300,000 kucheza pool table asubuhi

mkuu hayo makambi hayana tofauti na yale ya adolf hitla...
pia huo utakuwa utumwa wa kisasa!
Mkuu hayo mashamba wameshayaandaa je watapata chakula mchana na cha usiku ? Watalipwa mshahara shs ngapi? Pakulala je.
 
1458308641207.jpg
1458308669887.jpg
 
Hakuna shida hapo tumemuelewa vizur kumbe tatizo pool table tu hapa kijiwen kwetu tumeamua asubuh tunacheza karata, na draft or bao manake ni michezo pia ikifika Saa kumi tunaanza pool table .
Hii akili ya kitoto kabisa yaani unamkomoa Magufuli ama unajikomoa wewe mwenyewe? Kwenye kucheza kamari ya pool ndo utajenga nyumba nzuri? Gari zuri Na kusomesha watoto? Ama huko kwenye karata?lazima vijana tujifunze kutumia fursa kufanya kazi zilizo halali, kweli kwa akili hizi vijana wengi wakiume wataolewa sana siku za mbeleni.
 
Jamani mlio summarize, siku za siku kuu ...mechi zinaanza mda gani?
 
kweli magufuli ana taaabu!!! aliposema pool hakumaanisha pool tuu
alimaanisha matendo yote yasiyokuwa ya kikazi muda unaotambulika kuwa ni wakazi. mfano ukiwa ni pool hamuelewi????????
 
Issue ni pale viongozi watakapokomalizia pool tu wakati Rais alitoa pool kama mfano mmojawapo wa shughuli anazoziona hazina tija ya moja kwa moja ....
Ubunifu wa viongozi wetu ni ziro. Muda si mrefu wataanza kupiga simu kwenye tv na radio stations kumuiga Magufuli.
 
Wangekuwa wanajiuliza maswali madogo km haya huenda ingesaidia,tatizo mkuu wa kaya si presidential material ukitazama utadhani ni mwenyekiti wa kijiji anavyoropoka daily.
Hili suala watalikurupukia hawa viongozi wetu kwa kuwa rais kasema. Kwani kuna mtu anayempangia mwenzake kazi ya kufanya au ratiba ya kufanya hiyo kazi kama si mwajiri wake au baba yake? Kwa watumishi wa serikali sawa, acha wakamatwe kama watakuwa wanacheza pool au mchezo wowote muda huo wa kazi. Lakini mtu amejiajiri, kazi anazozifanya anazijua mwenyewe, ofisi yake mahali ilipo anapajua mwenyewe na ratiba yake ya kazi anaijua mwenyewe, unawezaje kumpangia muda wa kufanya hiki au kile? Hii kauli tangu inatoka siku ya kwanza ilinitia ukakasi, na pamoja na juhudi anazozifanya Rais Magufuli katika mambo mengi, kauli kama hii ya kucheza pool, ile ya kusema wakuu wa mikoa waweke ndani watu wengi ILI WANANCHI WAJUE KUWA WANASTAHILI KUHESHIMIWA na nyingine zinazofanana na hizo zinanifanya miwe na wasiwasi kuwa huko mbele mambo yanaweza kuanza kwenda mrama maana si kauli makini sana.
 
Kama ni hivo ngoja nihamie kwenye bao na draft maana huku kuna masharti nafuu sio huko kwenye pultebo
 
kweli magufuli ana taaabu!!! aliposema pool hakumaanisha pool tuu
alimaanisha matendo yote yasiyokuwa ya kikazi muda unaotambulika kuwa ni wakazi. mfano ukiwa ni pool hamuelewi????????
Huo muda unaotambulika kuwa ni wa kazi ni muda ni upi? Nani anayepanga muda wa kazi wa mfanyakazi kama si mwajiri wake? Sasa unataka kuniambia kila mwananchi wa Tanzania ameajiriwa na Serikali? Je, serikali inafahamu kazi wanazofanya wananchi wote na muda zinapotakiwa kufanyika? Hebu tumia akili japo kidogo, si kushabikia kwa kuwa tu Rais kasema
 
kweli na iwe hivo mda wa asubuhi ni kutafuta pesa
Wengine pesa wanatafuta mchana na wengine usiku. Mtu kama haujamwajiri wala kumpangia kazi huwezi kujua muda wake wa kufanya kazi ni upi. Kama mtu biashara yake ni night club au Casino, unataka saa nne akafanye kazi gani muda huo? Au kama anamiliki Bar na hapo ndio ofisini kwake na Rais amesema wateja wasije kunywa pombe asubuhi maana ni muda wa kazi, unataka yeye aende wapi muda huo? Kama wakiamua kucheza 'pool', bao, karata, draft wakisubiria wateja waanze kuja saa 10 atakuwa amefanya kosa gani?
 
Wengine pesa wanatafuta mchana na wengine usiku. Mtu kama haujamwajiri wala kumpangia kazi huwezi kujua muda wake wa kufanya kazi ni upi. Kama mtu biashara yake ni night club au Casino, unataka saa nne akafanye kazi gani muda huo? Au kama anamiliki Bar na hapo ndio ofisini kwake na Rais amesema wateja wasije kunywa pombe asubuhi maana ni muda wa kazi, unataka yeye aende wapi muda huo? Kama wakiamua kucheza 'pool', bao, karata, draft wakisubiria wateja waanze kuja saa 10 atakuwa amefanya kosa gani?
usiongee hili mbele ya mtoto wako hata amini kuwa wewe ni baba.
hivi kuwa mpinzani ni lazima upinge tuuu kila jambo unapinga tuu
 
1. Nadhani tatizo si watu kucheza pool tables au drafti na the likes..tatizo ni KWA NINI WANACHEZA? no ajira/uvivu/mipangilio ya kazi za kujiajiri/ e.t.c
(research needed)..wakijua tatizo halisi ndo wapange strategies za kusolve na solution inakuwa scientific na longlasting.
2.Hatuko ile dunia ya kudhani muda wa kazi ni mchana tuuu..Magu mwenyewe anataka nchi yenye uchumi wa viwanda..huko viwandani tunaenda vibarua vya usiku...sasa mchana lazima tule bata kidogo kwenye pool table pale, tule hela za wanachuo wanakuja pale na boom kuuubwa kiwango LOW.
 
usiongee hili mbele ya mtoto wako hata amini kuwa wewe ni baba.
hivi kuwa mpinzani ni lazima upinge tuuu kila jambo unapinga tuu
Haujasema chochote. Bora mimi hataamini kama ni baba, lakini wa kwako ukiongea staili yako hataamini kama wewe si kichaa. Kama huwezi kuona mantiki ya ninachosema subiri uone. Si amri imetolewa? Hakuna sababu ya kubishana na kukashifiana kwenye keyboard. Tutayaona live. Hayo makambi wawe wamejenga kabisa maana watawapeleka wengi huko.
 
Haujasema chochote. Bora mimi hataamini kama ni baba, lakini wa kwako ukiongea staili yako hataamini kama wewe si kichaa. Kama huwezi kuona mantiki ya ninachosema subiri uone. Si amri imetolewa? Hakuna sababu ya kubishana na kukashifiana kwenye keyboard. Tutayaona live. Hayo makambi wawe wamejenga kabisa maana watawapeleka wengi huko.
hapo kidoogo mwanao anaweza kukuita mjomba..
nchi hii ina opportunity ever happen! wahindi na wachina wanakuja mafukara wanaondoka ma milionea!!! wanaona opportunity! si kila mtanzania aliye fanikiwa amewezeshwa ni kujitambua tuuu!
Kama hawataki kufanya kazi wakamatwe maana hakuna njia nyingine
 
Hili ndilo naliongelea kila siku, nchi inaongozwa na watu wengi wasiofikiria, sasa kama hawa wameona hili nalo ni la muhimu.. Hehehe!

Serikali ya sasa hivi ni ya kituko sana, Magufuli inabidi afukuze wote apange upya, aliopanga hawa hawajisomi.

Pool hata ikifutwa kabisa nchini haipunguzi wala kuongeza kitu HATA KIDOGO, yaani badala ya kukaa na kufikiria wataboreshaje michezo itakayowapa vijana vipato wanasema mtu haruhusiwi kucheza pool, tunapangiana mida ya kufanya vitu? Sirudi bongo, huu ujinga siwezi kuuvumilia.
 
Back
Top Bottom