Fahamu zaidi kuhusu Vanguard na Rav 4 model ya 2009- 2014

KIMOMWEMOTORS

JF-Expert Member
May 17, 2018
358
670
Toyota ni moja ya Makampuni makubwa zaidi ya uzalishaji magari Duniani na wamejikita zaidi katika utengenezaji wa magari yenye uwezo mkubwa na imara lakini bila kuyasahau ya wastani yenye uwezo wa kawaida na ubora wa.

Kwa ufupi, zifuatazo ni baadhi ya tofauti za Magari haya mawili yaani Toyota Vanguard na Rav 4 model za kuanzia 2009 mpaka 2014

1. Injini

Ni ngumu kuzitofautisha injini hizi mbili kwa kua zote zina mwendo na uwezo mzuri. Rav 4 ina injini ya 2.5L ambayo ni Cylinder/Piston 4. Gari hiyo ina injini yenye Cc 2400 ikiwa na 4WD au AWD.

Wakati Vanguard ina injini za Cc 2400 mpaka 3500 na unaweza kuitumia kwa 4WD na 2WD

2. Magumizi ya Mafuta

Hakuna tofauti kubwa kwenye matumizi ya mafuta haswa kwa hizi za Cc 2400 kwa Cc 2400 kwa kua zote huenda kati ya kilomita 12 mpaka 13 kwa lita moja ya Petrol

3. Idadi ya Viti

Idadi ya viti ni moja ya vitu vya kuzingatia unapofikiria kuchagua gari za muundo huu. Rav 4 ina viti 5 wakati vanguard ina viti 7 jambo linalopelekea nafasi ya mizigo kua ndogo huku nafasi ya mizigo katika Rav 4 ikiwa ni kubwa zaidi

4. Uwezo wa Gari

Vanguard inaonekana kua Imara na yenye nguvu zaidi kuliko Rav 4. Nguvu ya Rav 4 kwa kawaida haizidi HP 170 wakati ya Vanguard ni mpaka HP 270 jambo linaloifanya itawale zaidi barabarani

5. Gharama za Uagizaji

Uzoefu katika hizi gari mbili unaonesha kua zinatofautiana kati ya milioni 1 mpaka milioni 3 kutegemea na mwaka kwa kua zina ushuru tofauti. Mara nyingi Rav 4 huagizwa kwa jumla ya gharama za Tsh 23.5 wakati Vanguard huanzia 25.5m

Hitimisho

Kwa kua sasa unajua machache kuhusu gari hizi mbili yaani Rav 4 ya 2009 mpaka 2014 na Vanguard, na kwa kua zote zinaonekana kua sawa kwenye baadhi ya vitu huku zikitofautiana kwenye mambo machache, sasa kazi ni kwako kuamua kuchagua aina ya gari unayoipenda zaidi kulingana na maelezo hayo.
A9851C7E-6DE6-4C1B-99A8-F202D879393B.jpeg
E6C22AF5-7586-4AFF-A144-83189E4B57C6.jpeg
 
... Kiongozi kwa agizo la RC keshokutwa naleta kamkweche kangu hapo kwenu mnifanyie ukaguzi bure. Nataka nielekee mikoani kula Krismasi.
 
Hakika mnastahiri pongezi sana kwa ufafanuzi wenu ,mie naomba ufafanuzi wa gari mbili yaani Vanguard vs Harrier 240G ya miaka hiyo 2009 mpaka 2014
Shukrani sana boss kwa pongezi zako. Kwa kua Vanguard tumeshaiongelea hapo juu. Kwa ufupi ntaigusia hii Harrier New model yenye nembo 240G

Injini ya Harrier pia ni Cc 2400 huku ikiwa na option ya 4WD na 2WD kwa baadhi ya magari. Kwa wastani utumiaji wa mafuta hautofautiani sana na Vanguard kwa kua hii nayo inaenda kati ya km 11- 12 kwa lita. Idadi ya viti ni kwamba, hii gari ina seat 5, tofauti na Vanguard nyingi zenye siti 7. Harrier ya 240G yenye ina nguvu ya 160Hp wakati Vanguard yenye Cc 2400 ina Hp 170 huku ile Vanguard ya Cc 3500 ikiwa na Hp kubwa kufikia Hp 270

Gharama ya Harrier 240G kwa wastani kwa kiagiza huanzia Tsh 23m. Mwisho kabisa Vanguard inaonekana kuboreshwa zaidi kidogo kwenye nguvu na uimara iwapo barabarani tofauti na Harrier lakini pia Vanguard ina seat nyingi zaidi ingawa harrier ina nafasi kubwa zaidi ya mizigo. Kinachobaki hapo ni muhisika mwenyewe anapendelea gari ya aina gani zaidi kati ya hizo mbili.
 
Naomba tofauti ya Vangurd 2009 vs Mitsubish Outlander 2006

Outlander nyingi zina Cc 2400 kama ilivyo kwa hizi Vanguard nyingi. Mfumo unaotumika kuzifanya gari hizi zitumie mafuta kidogo zaidi wakati injini ni kubwa kwenye Toyota Vanguard hujulikana kama Vvti wakati kwenye Outlander au Mitsubishi huitwa GDI (Gasoline Direct Injection).

Outlander ina 4WD ambayo unaweza kuitumia kulingana na mahitaji na mda mwingi ukatumia 2WD ambayo inavuta miguu ya mbele na hivyo kufanya mafuta kutumika kidogo zaidi. Kwa wastani Outlander hutumia lita moja kwa km 12.5 ikiwa kwenye 4WD na kama utatumia 2WD inaenda mpaka km 14.5 kwa lita. Ina viti saba kama ilivyo kwenye Vanguard, japo chache ni viti 5. Injini ya Outlander yenye Cc 2400 GDI huwa na nguvu ya 166Hp wakati ya Vanguard ni 170 Hp. Kuagiza Outlander mpaka mkononi kwa wastani hugharimu kuanzia 17m.
 
Clugar na harrier ipi ni imara nataka nijitoe muhanga hapo au pia nissani extrail new model na hizo kati ya cluger na harria.
 
Clugar na harrier ipi ni imara nataka nijitoe muhanga hapo au pia nissani extrail new model na hizo kati ya cluger na harria.
Kluger ni maboresho ya Harrier Old Model boss. Zote ni gari nzuri kwenye upande wa uimara na zinakaribiana kwa sehemu kubwa hata gharama za matengenezo na vipuri. Zote ni nzuri sana kwenye Rough Road ingawa kwenye upande wa stability iwapo kwenye mwendo Kluger inaonekana kuboreshwa zaidi haswa kwenye uimara kwa kua huanza kua nyepesi ikifika 140 speed wakati Harrier ikiwa kwenye 120 speed huanza kua nyepesi kidogo
 
Kluger ni maboresho ya Harrier Old Model boss. Zote ni gari nzuri kwenye upande wa uimara na zinakaribiana kwa sehemu kubwa hata gharama za matengenezo na vipuri. Zote ni nzuri sana kwenye Rough Road ingawa kwenye upande wa stability iwapo kwenye mwendo Kluger inaonekana kuboreshwa zaidi haswa kwenye uimara kwa kua huanza kua nyepesi ikifika 140 speed wakati Harrier ikiwa kwenye 120 speed huanza kua nyepesi kidogo
Uko vizuri mkuu, January ntakutafuta.
 
Umesema gharama ya harrier new model yenye nembo 240G kuagiza mpaka mkononi ni million 23 au!?nifafanulie kidogo mkuu
Umesema gharama ya harrier new model yenye nembo 240G kuagiza mpaka mkononi ni million 23 au!?nifafanulie kidogo mkuu
Umesema gharama ya harrier new model yenye nembo 240G kuagiza mpaka mkononi ni million 23 au!?nifafanulie kidogo mkuu
Inaanzia hapo kwenye 23m na mda mwingine inaweza kuanzia hata kwenye 22.5. Sisi hatuweki cha juu bali tunapiga hesabu zote hizi kwa uwazi kabisa ili mtanzania apate kilicho bora kwa gharama nafuu na wakati huo huo akituwezesha kukua zaidi
 
Back
Top Bottom