Fahamu: Meno yaliyooza yanatibika

clion dismas

Senior Member
Aug 6, 2017
185
170
SOMO LA 23

AFYA YA MENO

clion odhiambo , contacts : odhiamboclion@gmail.com : BE BLESSED

Utangulizi

MENO YALIYOOZA YANATIBIKA.

is

Meno kuoza ni ugonjwa ambao umeathiri rika zote kwa sasa, si watoto wala watu wazima. Ni ugonjwa ambao kwa hakika mtu anajitengenezea mazingira ya kuupata, ni ugonjwa wa tabia.

KWA UFUPI

Tafiti nyingi ulimwenguni kama FDA na ADA za marekani, zimeonyesha uhusiano wa vyakula vya kusindikwa pamoja na maradhi ya meno. Chanzo kikuu cha meno kuoza, usababishwa na sukari inayozalishwa baada ya mmeng`enyo wa vyakula vya wanga inayopelekea bakteria aina ya Streptococcus mutans kushambulia afya ya kinywa na bakteria wengine wengi kufuatia kudhuru meno na kinywa. Sababu nyingine ni kama: Upungufu wa madini ( CHOKAA, FOSFORASI, MAGNEZIAMU) , upungufu wa vitamini kwenye vyakula( A,D,K), usafi wa meno usio sawa, vyakula vyenye winggi wa tindikali lakini pia tabia mbaya za mlo.


Sukari hii, hubadilishwa na bakteria walio kinywani na kusababisha tindikali. Ambapo hii tindikali utafuna madini ya chokaa yaliyo katika uso wa juu wa jino (enameli) na kusababisha kuoza kwa jino au meno.

FLORAIDI INA MCHANGO GANI?

Floraidi ni aina ya kampaundi asilia ( au ya kutengeneza) inayo patikana katika aina kadhaa za vyakula inayosaidia meno kuwa imara. Floraidi inapatikana kwa wingi katika miamba na udongo, pale maji yanapopita katika miamba uzalisha floraidi ayoni ambazo zinaingia katika miili yetu na kujenga maeneo ya meno na mifupa kwa ujumla. Tafiti zinaonyesha kwamba, watoto kwa asilimia 60 na watu wazima kwa asilimia 35 wanaotumia madini ya floraidi afya ya meno yao inakua bora Zaidi.

Baikaboneti (baking soda)
is


Ni aina ya chumvichumvi yenye asili ya alkali iliyo na uwezo wa kuzuia makuzi ya bakteria aina ya S.mutan na kufanya meno kuwa meupe. Katika Journal of Dental Hygiene, Vol. 79, No. 4, October 2005, imebaini jambo hili.Ukiamua kutumia kuswaki nayo, hakikisha huimezi, sukutua na uiteme. kwa sababu ya uwingi wa madini ya sodiamu na pia, mwili unazalisha baikaboneti unayoihitaji. uzuri ni kwamba, hii, sio sumu.

Haidrojeni perokisaidi ( hydrogen peroxide)
is


Ni aina ya kampaundi ambayo inauwezo wa kuzia lakini pia kuondoa utando wa njano kwenye meno kwa kuua bakteria jamii ya S. mutans. huu ni utofauti ambao upo kati ya bicarbonate na hii kampaundi. Journal of Dental Hygiene, Vol. 79, No. 4, October 2005 imeeleza kwamba pale ivi vitu viwili vinapotumika kwa pamoja matokeo bado ni yaleyale. Sodium Bicarbonate and Bicarbonate of Soda


Onyo Ni vyema ifahamike, baking soda inapotumika inaongeza madini mengi ya sodiamu mwilini ambayo uhusishwa na maradhi ya shinikizo la damu.kijiko kimoja cha chai kina gramu 1.259 za sodiamu ambazo ni nyingi. Kwa mtu asiye na maradhi ya shinikizo la damu la juu, kwa siku anashauriwa kutumia kiasi chini ya 2.3 gramu, aliye na maradhi , anatumia chini ya gramu 1.5.

Usitumie hii baikaboneti kama dawa labda kama tuu, tabibu wako amekuambia kufanya hivyo.

VYAKULA VYA KUTIBU MENO YALIYOOZA.

Zingatia, vyakula ndio suluhu ya kutibu meno yaliyooza. Tafiti zimeonyesha kwamba, baadhi ya vyakula vya asili vinaweza kuziba na kukuza tena sehemu ya jino iliyoliwa na bakteria. Navyo ni:-

1. Vyakula vyenye uwingi wa vitamin D na chokaa (Ca)
Tafiti ilifanywa uko jijini uingereza katika makundi matatu ya watoto wenye meno yaliyooza, 1.waliopewa vyakula vya nafaka na tindikali phytic 2. Walipewa chakula cha kawaida na vitamin D, 3. Walikula nafaka nzima, mbogamboga na matunda pamoja na vitamin D.
MATOKEO,
kundi la 3 walionyesha kupona kabisa ndani ya miezi 6, wakati kundi la 2 walikua na afadhali lakini kundi la 1 kuoza kuliongezeka.

2. Vyakula vyisivyo na sukari za kuongezwa
Sukari ina tindikali nyingi ambayo ndio chanzo kikubwa cha meno kuoza, ni chakula cha bakteria kinywani, jitahidi kutumia asali na matunda na sio sukari na vitu vyote vyenye sukari ya kuongeza kama pipi, soda, lambalamba na chokoleti.

3. Tumia lishe bora ya kila kitu asilia
vyakula vyote vyafaa vilivyoelezewa humu. Zingatia njia sahihi za mapishi ya vyakula asilia, rejea juu na usome MAHARAGWE YA SOYA.Lazima fahamike, hata chakula kizuri kinaitaji utaratibu wa kukiandaa ili kiweze kua bora.Lakini pia zingatia usafi wa kinywa, haya yote kuyafanya bila usafi wa kinywa ni sawa na bure. Sukutua kwa mafuta ya nazi na karafuu Tafiti zimeonesha kuwepo ahueni na kupona kabisa kwa kutumia njia hii. Vuta mafuta ya nazi kinywani, asubuhi na mapema, sukutua kwa dakika 10 hadi 20, tema mafuta, safisha kinywa kwa maji ya vuguvugu yenye chumvichumvi. Alafu sukutua kama kawaida, kwa kutumia dawa za asili.

WAZAZI/WALEZI

NI MUDA WA KUJIHOJI, TAFITI ZA AFYA ZINAONYESHA KWAMBA VITU VYENYE SUKARI NYINGI VINACHANGIA SANA KATIKA KUATHIRI UBONGO WA MTOTO. UPEO WAKE WA KUFIKIRIA, AKILI YAKE KWA UJUMLA PAMOJA NA UBONGO.

KWA SEHEMU KUBWA, WAZAZI TUNAWANUNULIA WATOTO WETU VITU VITAMU KAMA ZAWADI ZA WATOTO, KWA AJILI YA KUWAFURAHISHA KWA MUDA BILA YA KUFAHAMU YA KWAMBA TUNAWAATHIRI PIA. NIWASIHI NINYI MNAOWAPA WATOTO MALEZI, WAZOEZENI WATOTO VITU VIZURI VYA ASILIA KAMA MATUNDA PALE WANAPOKUA WADOGO ILI KIZAZI CHA KESHO KIWEZE KUWA KIZAZI CHENYE MANUFAA KATIKA TAIFA NA DUNIA KWA UJUMLA KIAFYA, KIAKILI LAKINI PIA KIROHO.

MAANDIKO YANASEMA:- “Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee.” (Mithali 22:6)

JIHOJI: "Unamlea mtoto wako?"

Rejea

Center for disease control and prevention (CDC) American dental association (ADA) Fluoride in Water. THE INFLUENCE OF A CEREAL-FREE DIE RICH IN VITAMIN D AND CALCIUM ON DENTAL CARIES IN CHILDREN IT I BY MAY MELLANBY AND C. LEE PATTISON, M.B., B.S. (Pharmacology Department, University of Sheffield, and King Edward VII Hospital, Sheffield)
 

Attachments

  • upload_2017-9-21_15-0-33.png
    upload_2017-9-21_15-0-33.png
    14.7 KB · Views: 178
Ndio, ambayo ina sifa ya kuondoa huo utando wa njano ni HAIDROJENI PEROKSAIDI( HYDROGEN PEROXIDE). Kama nilivyoelezea hapo juu ndugu JOSEVEREST, chapa mandashi( baking soda) yenyewe huzuia kutengenezeka kwa utando mpya lakini haiondoi ule wa awali tofauti na peroxide ambayo hupambana na utando wa awali huku ikizuia ule utando mpya unaoweza kutengenezeka. ndani ya wiki 5-7 kwa utando komavu unaisha kabisa. Kama ndugu PILOT 7 alivosema, ni jambo la mda lakini niongezee na ufasaha wa usafi wa kinywa. huwezi kuwa unasukutua na peroxide wakati bado unalala bila kuswaki au unaswaki mara moja utegemee miujiza. AHSANTE.
 
Ndio, ambayo ina sifa ya kuondoa huo utando wa njano ni HAIDROJENI PEROKSAIDI( HYDROGEN PEROXIDE). Kama nilivyoelezea hapo juu ndugu JOSEVEREST, chapa mandashi( baking soda) yenyewe huzuia kutengenezeka kwa utando mpya lakini haiondoi ule wa awali tofauti na peroxide ambayo hupambana na utando wa awali huku ikizuia ule utando mpya unaoweza kutengenezeka. ndani ya wiki 5-7 kwa utando komavu unaisha kabisa. Kama ndugu PILOT 7 alivosema, ni jambo la mda lakini niongezee na ufasaha wa usafi wa kinywa. huwezi kuwa unasukutua na peroxide wakati bado unalala bila kuswaki au unaswaki mara moja utegemee miujiza. AHSANTE.
anhaaa sawa kiongozi
 
Unatumia hydrogen peroxide kwa muda gani

1. KWA AJILI YA KUNG`ARISHIA MENO, HADI PALE UTAKAPO PATA MATOKEO UNAYOYAHITAJI.

2. KWA AJILI YA KUUJENGA MWLI NA KUJIKINGA PIA KUPONYA MARADHI, WALAU MARA 3 KWA WIKI. MAANA, MWILI WAKO UNATENGENEZA KIASI UNACHOHIJAJI KILA SIKU.
 
Na je haiwezi kuleta shida ikitokea umemeza bahati mbaya

HABARI NDUGU,
Kwa hizi tuzitumiazo kwa lengo la kung`arisha na kusafisha kinywa, zimepimwa na kuthibitishwa na "ADA" PAMOJA "UE" kwamba ndicho kiwango kinachofaa. yaani, hata ikiwa mwilini kwa kiasi kile, haina madhara . Kwani unasukutua nayo, aada ya dakika tatno hivii, unapiga mswaki kawaida.

lada pia nikujuze,:-

HYDROGEN PEROXIDE NA CARBAMIDE PEROKSAIDI NI KEMIKALI AMBAZO ZINA SIFA YA KUONGEZA WEUPE, YAANI KUNG`ARISHA.( BLEACH) lLAKINI PIA KUONGEZA KINGA MWILI( BODY IMMUNITY).

UPATIKANAJI WAKE
MAJI YA MVUA NA KWENYE MAJI YA ZIWA NA BAHARINI NA KATIKA MWILI WA BINADAMU

MATUMIZI- YAWEZA TUMIKA :-
-KAMA MAJI- YAANI UNAINYWA
-KAMA DAWA YA MSWAKI, UKIICHANGANYA NA CHAPA MANDASHI

AIDHA: WAWEZA ITUMIA UKIWA:-


1. NYUMBANI-( 3%-6%)- BILA UANGALIZI

2. CHINI YA UANGALIZI MAALUM WA TABIBU( IN OFFICE)- ASILIMIA 30-35, HYDROGEN PEROXIDE

ILE YENYE ZAIDI YA ASILIMIA 35, IMEZUIWA NA MASHIRIKA MENGI YA AFYA DUNIANI KAMA “ADA” NA “EU”, INAHARIBU NA KUUA BAADHI YA SELI ZINAZOZALIWA. PALE UNAPOKUWA CHINI YA UANGALIZI, HUWEZI RUHUSIWA KUIMEZA, NA HATA IKITOKEA BAHATI MBAYA, KUNA HUDUMA STAHIKI UTAPEWA.

KUMEKUWA NA MJADALA, UNAOENDELEA UNAOTAKA BAINI KAMA KUNA MADHARA KAMA:-

1. KUPOTEA KWA ULINGANO WA USO WA MENO( ROUGHNESS)

2. KUPOTEA KWA BAADHI YA MADINI( KALSHAMU NA FOSFORASI)

3. KUPUNGUA KWA NGUVU YA MIZIZ(TISHU) ISHIKAYO MENO

( INGAWAJE TAFITI ZA KISAYANSI ZINAENDELEA KWA WINGI, HADI SASA NYINGI ZINAONYESHA MADINI YA KALSHIAMU NA FOSFORASI KATIKA USO WA JUU WA JINO(ENAMELI), HAZIPOTEI.)

NAMANA GANI/ KIASI

(3-6) ASILIMIA NI SALAMA KWA MATUMIZI. UKIWA NYUMBANI, WAWEZA KUNYWA WALAU MARA TATU KWA SIKU.( NDIO, KUNYWA, TONE MOJA AU KIJIKO KIMOJA CHA CHAI CHANGANYA NA MAJI NUSU LITA MOJA YA KUNYWA NA UNYWE.)

MARA NYINGI, 3%, NDIZO UTUMIKA KWA MATATIZO YA KINYWA( ZIPO MADUKA YA DAWA NA SUPER MARKET).

WAWEZA CHANGANYA NA BAKING POWDER NA PEROXIDE UKATENGENEZA DAWA YA KUSUKUTIA MENO. INALETA FAIDA SANA NA MATOKEO MAZURI, LAKINI KWA HAPA, FANYA WALAU MARA MOJA KWA WIKI. SABABU, BAKING POWDER INA MADINI YA SODIAMU MENGI.( HII AUNYWI NA AUMEZI, TEMA.)

IFAHAMIKE KUWA, MIILI YETU INATENGENEZA NA KUTUMIA PEROXIDE KWA AJILI YA KUUA BAKTERIA, FANGASI NA SARATANI.

PALE TU MWILI UNAPOHISI HALI ISIYO SAHIHI, KATIKA DAMU, SELI AINA YA,T-SELI UZALISHA PEROXIDE KATIKA SELI NYEUPE ZA MWILI WAKO.

MAZIWA YA MAMA YA MWANZO KABISA(COLOSTRUM), YANA ASILIMIA NYINGI SANA ZAIDI YA 20, AMBAZO UMKINGA MTOTO NA MARADHI MBALIMBALI.

ONYO:

KWA WALE WALIPEWA FIGO NA WENGINE( TRASPLANT), WASIITUMIE, MAANA INAZUIA BAADHI YA OGANI KUFANYA KAZI NA FIGO ILO.

TUMIA LISAA KABLA YA KULALA KWA MAANA, UONGEZA MOLEKULI ZA OKSIJENI AMBAZO UPELEKEA KUKOSEKANA KWA USINGIZI MUDA MREFU, LAKINI TUMIA MASAA MATATU BAADA YA KULA. AU TUMIA KABLA UJALA CHOCHOTE.

UNAPOANZA KUITUMIA INAKUA NA MAUDHI MENGI, KAMA KICHHEFUCHEFU, KUTAPIKA NA MENGINE KAMA HAYO.

KWA MAELEZO ZAIDI- PATA USHAURI WA TABIBU WA MENO UISHIKO

WASALAAM.
 
Naomba kuuliza..nitapata wapi Huduma ya braces kwa hapa tz, front teeth kweny low jaw yame mis aligne...
 
Jamani hiii peroxide ni ile ya kusafishia vidonda ambayo inauzwa kwenye maduka ya dawa???
 
Naomba kuuliza..nitapata wapi Huduma ya braces kwa hapa tz, front teeth kweny low jaw yame mis aligne...[/QUOTE

kuna kijana alifanyiwa huduma iyo: yeye alifanyia muhimbili, kitengo cha meno. fika pale utapata ushauri na ufafanuzi zaidi. ingawaje kuna maeneo mengi ya private wanafanya ivo. hosiptali nyingi za rufaa pia wana miundombinu ya huduma iyo.
 
Jamani hiii peroxide ni ile ya kusafishia vidonda ambayo inauzwa kwenye maduka ya dawa???


naam, ni hiyihiyo, sema content, yaani asilimia ndio utofautiana.

NIKUHABARISHE KIDOGO: ASALI INATIBU MADONDA KWA SABABU YA KUWA NA HYDROGEN PEROXIDE KWA WINGI.
PEROXIDE HUZUIA MAKUZI YA VIMELEA WADOGOWADOGO KATIKA ENEO LA KIDONDA.
 
Naweza kupata wapi Huduma ya meno kupangiliwa maana hii dental formula niliyonayo haiko poa kabisa meno yapo zigzag

Itakuwa vizur nikiainishiwa gharama
Location ambayo nipo mm ni Dar es Salaam
 
Naweza kupata wapi Huduma ya meno kupangiliwa maana hii dental formula niliyonayo haiko poa kabisa meno yapo zigzag

Itakuwa vizur nikiainishiwa gharama
Location ambayo nipo mm ni Dar es Salaam


HUDUMA YA ORTHODONTIC INAPATIKANA NDUGU:
GHARAMA UTOFAUTIANA SEHEMU NA SEHEMU, NI VYEMA UVITEMBELEE VITUO NILIVYO AINISHA HAPO JUU.

YAANI
1. MUHIMBILI
2. TMJ
3. AGA KHAN
4. DENTAL STUDIO: MASAKI, SEA CLIFF, OROFA YA KWANZA- 0753 601 155

NA HOSIPTALI NYINGINE NYINGI ZA RUFAA.

AHSANTE.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom