maisha Ya Ubachelor Unaweza Kujishaua Kufululiza Kupika Msosi Hata Mwezi Mzima Ila Vyombo Visafi Vikiisha Ndani Unarudi Kwenye Utaratibu Ule Ule Wa Kula Chipsi Na Paja La Bukujero.
Maisha Ya ubachela Kila Siku Tunapoteza Vijiko Kidogo Kidogo Kwa Kumwaga Maji Ya Ukoko Wa Ugali..
Maisha Ya Ubachela Unaweza Kuloweka Sufuria Ulopikia Ugali Likakaa Na Maji Wiki Nzima Yakianza Kunuka Unamwaga Halafu Unaweka Tena Maji Mengine..
Maisha Ya ubachela Mara Nyingine Neti Hugeuka Kuwa Hema.. Ikichomekwa Haichomolewi Mpaka Siku Utakapopata Mgeni..
Maisha Ya Ubachela Hufika Kipindi Mtu Unageuka na kuwa kamnyama fulani ivi [emoji2], Unanusa Kwanza Nguo Ili Ujue Kama Unaweza Kuipa Round Ya Pili Au Hapana..
hivi kwanini mnapenda kutusumbua mabachera sio kanisani,kazini,msikitini,vikao vya familia,mtandaoni kazi kutusema sisi tuna kitu gani tunawakosesha tukibaki bachela