Fahamu kuhusu vita ya Karansebes

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Apr 29, 2016
20,744
25,438
Unaweza kudhani ni hadithi ya kutunga lakini hii kweli ilitokea! Vita ya Karansebes, ni miongoni mwa matukio yaliyoushangaza sana ulimwengu baada ya wanajeshi wa jeshi moja la Austria, kushambuliana wenyewe kwa wenyewe na kusababisha wanajeshi zaidi ya 10,000 kupoteza maisha.

6e413925c45fbe0e294f8a74b12e6eeb.jpg

Ilikuwaje? Usiku wa Septemba 17, 1788, wanajeshi zaidi ya 100,000 wa Jeshi la Austria lililokuwa linaundwa na makabila mbalimbali, walikuwa wameweka kambi katika Mji wa Karansebes (Romania ya sasa) wakijiandaa kuvamia Himaya ya Ottoman (Uturuki ya sasa).
Ili kurahisisha uvamizi, wanajeshi waligawana katika makundi, wengine wakaenda upande mmoja na wengine upande mwingine. Wakati wakijiandaa kufanya shambulio, kukatokea kutoelewana kati yao, wakaanza kushambuliana wenyewe kwa wenyewe kimakosa wakidhani wanawapiga wanajeshi wa Ottoman.


CHANZO CHAKE KINASHANGAZA
Inaelezwa kuwa kundi moja kati ya yale mawili, lilivuka Mto Timis na kuingia Mji wa Hussar uliokuwa ngome ya wanajeshi washirika, Wahussar waliokuwa wakisaidiana kuwapiga Waturuki. Baada ya kuingia, wanajeshi wa Austria waliomba hifadhi kwa wenyeji wao ambao waliwakarimu kwa pombe na chakula wakati maandalizi ya vita yakiendelea.


Hata hivyo, kutokana na wingi wa wanajeshi hao, pombe iliisha wakati wanajeshi wakiwa bado wanaihitaji, wakaanza kuwashinikiza wenyeji wao wawaongeze, jambo lililosababisha kutokea kwa hali ya kutoelewana na kurushiana maneno. Mmoja kati ya wanajeshi wa Austria, ambaye tayari alishaanza kulewa, kwa hasira alifyatua risasi juu akishinikiza waongezwe pombe.
Mlio wa risasi ulisababisha taharuki kubwa eneo hilo, wenyeji wakahisi wamevamiwa na wanajeshi wa Ottoman (Waturuki), wakawa wanakimbia huku na kule wakitamka neno ‘Turci! Turci!’ (Waturuki! Waturuki).

913dc8b5a97d99b6ca8397e3ee7321bd.jpg

Mkanyagano ulipozidi kuwa mkubwa, ilibidi viongozi wa jeshi la Austria waingilie kati na kuanza kuwatuliza wanajeshi wao ambao nao walishachanganyikiwa wakidhani kweli wamevamiwa na Waturuki! Viongozi hao wakawa wanatumia neno Halt! Halt! Ambalo kijeshi hutumika kuwaamuru wanajeshi kuacha kila wanachokifanya na kutulia mara moja.
Kwa kuwa kabila la wenyeji, Wahussar hawakuwa wakijua Kiingereza wala Kijerumani, waliposikia neno hilo walilifananisha na ‘Allah! Allah!’ ambalo lilikuwa likitumiwa na wanajeshi wa Uturuki wanapokuwa vitani.
Wakaamini walikuwa wamevamiwa na Waturuki, wakaanza kuwashambulia, mapigano makali yakatokea kati yao. Kundi la pili lililokuwa upande wa pili wa mto, liliposikia mapigano yamekolea, nalo lilivuka mto na kwenda uwanja wa vita. Kwa kuwa tayari giza lilikuwa limeingia, wakaanza kuwashambulia wenzao ambao nao walijibu mapigo, vita ikazidi kupamba moto, kila mmoja akiamini anapigana na Waturuki.
Mpaka kunapambazuka, wanajeshi 10,000 walikuwa wamekufa huku wengine wengi wakiwa wamejeruhiwa. Kila mmoja aliyepona akawa anashangaa iweje katika wote waliokufa, wawe ni wa upande mmoja wa wanajeshi wa Austria na washirika wao wa Hussar, hapo ndipo ukweli ulipofahamika kwamba kumbe walikuwa wakipigana wenyewe kwa wenyewe.
Waturuki waliposikia taarifa hizo, walifika haraka eneo hilo na kufanikiwa kuuteka mji wa Hussar na mingine hivyo kushinda vita hiyo kiulaini.


Cc : the bold Nifah
 
he he! tupo kwenye dunia ya matendo lolote laweza kutokea hata kwa kiumbe mwenye akili(binadamu)
bila shaka nadhani waturuki kwakuwa walikuwa wanaamini kuwa allah ndo mungu wao basi nafikiri waliamini kuwa aliwapigania!
 
he he! tupo kwenye dunia ya matendo lolote laweza kutokea hata kwa kiumbe mwenye akili(binadamu)
bila shaka nadhani waturuki kwakuwa walikuwa wanaamini kuwa allah ndo mungu wao basi nafikiri waliamini kuwa aliwapigania!
Hata kwenye BIBLIA kuna story za namna hiyo. Upanga unainuka kwa wapinzani wa Israeli, wanatwangana wao kwa wao then Israeli anaibuka mshindi kilaini kabisa.
 
It all Begins with ALCOHOL
not for sale to person under the Age of 18 ; DRINK RESPONSIBLY
Hii wangesema tu "Not for sale to Anybody; DONT DRINK
labda ingetumika kitabibu/kikemia
 
Hata kwenye BIBLIA kuna story za namna hiyo. Upanga unainuka kwa wapinzani wa Israeli, wanatwangana wao kwa wao then Israeli anaibuka mshindi kilaini kabisa.
Na iwe hivyo kwa MAMA TANZANIA kila anayejaribu kuinuka juu yake apate wendawazimu na HAO MAADUI WOTE WA MAMA TANZANIA wapigane wao kwa wao mpaka wafe wao na vizazi vyao milele yote katika jina la Yahushua ha Mashaich...AMUN RA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom