Fahamu athari ya jina lako katika mapenzi

Fahamu athari ya jina lako katika mapenzi

jerryempire

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2017
Posts
5,830
Reaction score
10,093
Habarini wana jf,
Kumekuwa na matatizo mengi sana katika mahusiano yetu ya kila siku, hasa ya kamapenzi na hata kijamii(na wenzetu).

Mahusiano hayakai,watu kila siku wanasalitiana,na hata wengine kuchukiana bila sababu.

Wengi wamekuwa na majibu yanayofanana huku wengine wakifika mbali kwa kusema kuwa huwezi pendwa au kumpenda mtu pasipo matumizi ya fedha.

Lakini ki uhalisia fedha inanafasi ndogo sana tena ndogo mno katika mapenzi

Sababu ya mapenzi kudumu au kupendana baina ya fulani na fulani ni uwiano wa majina

Najua utastuka lakini huo ndo ukweli halisi, majina yanachukua nafasi kubwa sana katika kudumisha na hata furaha katika mapenzi iwe kwa wapenzi wetu na hata wengine wanao tuzunguka na hata pia wale tunaotaka kufanya nao biashara,

Endapo hakutakuwa na uwiano sahihi wa majina yenu basi uhusiano wenu kamwe hautadumu na hata ukidumu hautakuwa na furaha hivyo hivyo hata katika biashara yenu pia,

Endapo utafanya biashara na mtu ambae hamna uwiano katika majina yenu ni ngumu sana kufanikiwa na hata mkifanikiwa biashara yenu itaandamwa sana na matatizo mpka pale mtapofilisika.

UTAJUAJE UWIANO WA MAJINA YENU,
Elimu hii ya uwiano wa majina ilikuwa ikitumika sana na wazee wetu na ndio elimu hii hii inayotumika kuwaliza watu kwa kuwatoza gharama kubwa ili wasaidiwe

Endapo unataka kuanzisha mahusiano ya kimapenzi, kirafiki na hata kibiashara na mtu, kiuwiano unatakiwa muwe mmezidiana herufi saba au zaidi mfano jerry na rachel wanaweza kuwa wapenzi na kudumu na hata kibiashara lakini jerry na mary hawawezi kuwa wapenzi wala kushirikiana katika biashara na hata wakiwa wapenzi hawawezi kudumu wala kuwa na mahusiano ya furaha.

Kanuni hii pia unaweza kuitumia au hata kuithibitisha endapo unataka kupima mapenzi ya watu wawili au kutaka kujua nani anakupenda zaidi kwa kuangalia herufi za mwanzo za majina yao

Yule ambae herufi yake ya kwanza ya jina lake na lako zimezidiana (zimepishana herufi saba au zaidi) na herufi yko ya kwanza jua huyo ndo mwenye mapenzi na wewe zaidi kushinda mwengine na hivyo hivyo kwenye kutafuta mpenzi
 
maelezo yako butu! ongea kwa mfano, Wema vs Abduli , au Hamis Vs Fatima, PIA UNATAKIWA UELEZE JE Majina yenye kiswahili na kiingereza yanatambuliwaje kwenye formula yako mfano, Fatima>Fetty , Khamisi etc
 
Hii Kali mfano me Allan mwenzangu Naomi kiutabili inaikuaje
 
karibu unipinge kwa fact na si mihemko
nipo kwa ajili ya kuwasaidia
Fact yangu ni kwamba ulioongea hapo huo ni upuuzi na nia ya kuwaibia watu wenye matatizo ya mahusiano
Jina halipendi unaopenda ni moyo ungeniambia kuwa jina la mtu linaweza kusadifu tabia yake kidogo inamantiki japo hii dhana inaande kupotea kabisa

Ingekuwa hivyo kusingekuwa na maumivu ya mapenzi kwa sababu wote mnakuwa hamna hisia sababu ya majina hayajapishana herufi saba,

Mapenzi ni hisia inayoanzia kwenye macho hadi moyoni

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom