Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 33,623
- 40,176
Kocha mkuu wa Simba amezungumza kuelekea mchezo wa Dabi nakumesema.." Labda watacheza kwa ajili ya sare, labda wataamua kubaki nyuma na kucheza kuipata sare maana bila shaka wakipata sare watakuwa mabingwa, na sisi tunahitaji kucheza kushinda (ili tuwe mabingwa)...
Hivyo utakuwa mchezo wa kuvutia. Natumai Uwanja wa Benjamin Mkapa utakuwa nusu Kijani, Nusa Nyekundu na kujaa kwa uwezo wake wote wa watazamaji 60,000 walioketi...Na nina hakika utakuwa mchezo bora sana...
Tuwe na matumaini mara hii, iwapo itatokea mazingira ya Penati na ni ya wazi kama ilivyokuwa kwenye mchezo uliopita tulipopata nafasi mbili za namna hio kupitia Kibu Denis...Tuombe iwe fair na wazi (toka kwa mwamuzi)...
Kwa sababu tunahitaji sherehe ya Soka la Tanzania kufanyika siku hio...Tuna Mchezo wa Yanga Na Simba ni mchezo wa timu mbili kubwa zaidi nchini na siku hio tutakutana Uso kwa Uso na bila shaka dunia itakuwa inatazama..."
credit: Chazymedia