FA leo: Manchester United Vs Chelsea

FA leo: Manchester United Vs Chelsea

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,685
Man U na Chelsea zimekutana mara 166 katika mashindano mbalimbali, ambapo Manchester United imeshinda mechi 72, Chelsea (45), na wametoka sare mechi 49.
Chelsea itamkosa kiungo wake Juan Mata katika mchezo wa leo wa Kombe la FA dhidi ya Manchester United kwa sababu anaumwa. Kocha wa wa Chelsea Rafael Benitez anahitaji wachezaji wake kutulia zaidi kwani wanatakiwa kucheza mechi mbili muhimu katika saa 48 baada ya kuchapwa mwishoni mwa wiki.
Wakati Mata akiwa benchi, beki Gary Cahill anatarajiwa kurejea leo akiwa amepona goti lake lililomkosesha mechi waliyofungwa 2-1 na Southampton siku ya Jumamosi.
Vinara wa Ligi Kuu, Manchester United watamkosa beki wake Rafael anayesumbuliwa na nyonga aliyoumia wakati wa mechi dhidi ya Sunderland mwishoni mwa wiki. Wakati beki Rio Ferdinand, mkongwe Ryan Giggs na mshambuliaji Wayne Rooney waliopumzishwa Jumamosi wanatarajiwa kushuka dimbani leo.
Manchester United mchezo wa kwanza walitangulia kushinda 2-0 kabla ya kulazimishwa sare 2-2 na Chelsea. Mechi ya leo mchana tutegemee kuwa kali zaidi ukilinganisha na iliyopita.

 
television ya sky sports kutwa nzima inasema mata atakuwepo dimbani baada ya kukosa mechi mbili za chelsea..!hopefully mechi itakuwa nzuri na mwisho wa mchezo man utd ataondoka na ushindi ingawa man utd mara nyingi huwa wanaambulia kipigo kila wakisogea darajani
 
Sijawai kuwaombea mema Man U toka nizaliwe japo sina timu nnayoishabikia England, yoyote itakayocheza nao naisapoti.
 
Man U EPL inawatosha hili la FA bingwa mtetezi lazima alitetee kwa mara ya pili mfululizo!! Go go go the blues!!
 
Mkuu yetu macho! lkn The Blues wanatakiwa wakaze msuli angalau wapate kikombe cha FA.
 
Bora wanamichezo hususan wa miguu tunajadili ya maana. Hoja za leo nyingi zinatisha lakini kwenye football nafagilia ukweli tu. mambo ya ujinga na wajinga wao huko huko sio soccer bwana.

Mapema nitawahi uwanjani kuangalia mtanange, mech Saa gapi? sina uhakika sana kama ni saa nane na nusu au saa tisa.
 
Kama kawaida yake Chicharito atafunga bao,Chelsea wanamjua vizuri
 
Saa nane unusu kila kitu

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Ni chelsea vs man u.sio man u vs chelsea.
Unajua ukisema kitu kimija unawapa watu faida zaidi ya moja mfano ukisema man u vs chelsea ntajua mambo yafuatayo
1)leo ni siku ya match hiyo
2)ntajua kuwa man u ndo wenyej
3)ntajua kuwa itachezewa old trafod
4)ntajua kuwa m
an u watavaa jezi za nyumban
5)ntajua kuwa nyimbo gan za ushangiliaji zitaimbwa
6)ntkadiria idadi ya watu watakao ingia
7)ntajua wall gan ya man u itatumika kwa man u supporters kutoa mawazo yao
8)ntajua sut atakayo vaa furguson
9),ntajua bigjee atakazo kula furguson
10)ntajua kuwaaaa .....
 
ze buluu ndio champion of the match .mashetani wameshindwa yesu kafufuka jana tu.wapi hazard
 
Kama kawaida ni Chelsea vs Chicharito kwa hyo hatutamshangaa chicha aktupia bao na Man U kushinda kwani hata beki na kipa wa chelsea wanamjua vizuri.........
 
Ni chelsea vs man u.sio man u vs chelsea.Unajua ukisema kitu kimija unawapa watu faida zaidi ya moja mfano ukisema man u vs chelsea ntajua mambo yafuatayo1)leo ni siku ya match hiyo2)ntajua kuwa man u ndo wenyej3)ntajua kuwa itachezewa old trafod4)ntajua kuwa man u watavaa jezi za nyumban 5)ntajua kuwa nyimbo gan za ushangiliaji zitaimbwa6)ntkadiria idadi ya watu watakao ingia7)ntajua wall gan ya man u itatumika kwa man u supporters kutoa mawazo yao8)ntajua sut atakayo vaa furguson9),ntajua bigjee atakazo kula furguson10)ntajua kuwaaaa .....
duh we mkal wa statistics
 
Man U na Chelsea zimekutana mara 166 katika mashindano mbalimbali, ambapo Manchester United imeshinda mechi 72, Chelsea (45), na wametoka sare mechi 49.
Chelsea itamkosa kiungo wake Juan Mata katika mchezo wa leo wa Kombe la FA dhidi ya Manchester United kwa sababu anaumwa. Kocha wa wa Chelsea Rafael Benitez anahitaji wachezaji wake kutulia zaidi kwani wanatakiwa kucheza mechi mbili muhimu katika saa 48 baada ya kuchapwa mwishoni mwa wiki.
Wakati Mata akiwa benchi, beki Gary Cahill anatarajiwa kurejea leo akiwa amepona goti lake lililomkosesha mechi waliyofungwa 2-1 na Southampton siku ya Jumamosi.
Vinara wa Ligi Kuu, Manchester United watamkosa beki wake Rafael anayesumbuliwa na nyonga aliyoumia wakati wa mechi dhidi ya Sunderland mwishoni mwa wiki. Wakati beki Rio Ferdinand, mkongwe Ryan Giggs na mshambuliaji Wayne Rooney waliopumzishwa Jumamosi wanatarajiwa kushuka dimbani leo.
Manchester United mchezo wa kwanza walitangulia kushinda 2-0 kabla ya kulazimishwa sare 2-2 na Chelsea. Mechi ya leo mchana tutegemee kuwa kali zaidi ukilinganisha na iliyopita.


mata yupo uwanjani leo
 
television ya sky sports kutwa nzima inasema mata atakuwepo dimbani baada ya kukosa mechi mbili za chelsea..!hopefully mechi itakuwa nzuri na mwisho wa mchezo man utd ataondoka na ushindi ingawa man utd mara nyingi huwa wanaambulia kipigo kila wakisogea darajani

Una uhakika kuwa kila Man Utd ikisogea darajani inafungwa? naomba unikumbushe mechi ya ligi msimu huu Man ilishinda 3 kwa 2 kwenye uwanja gani?
 
Back
Top Bottom