Idimulwa
JF-Expert Member
- May 27, 2011
- 4,503
- 1,722
Mbunge wa Nyamagana-MWANZA Ezekiel Wenje na aliyekuwa diwani wa kata ya Sombetini-ARUSHA kupitia CCM kabla ya kujiuzulu na kujiunga CHADEMA bwana Alphonce Mawazo,watazindua kampeni za CHADEMA kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa diwani katika kata ya Lwenzera iliyoko tarafa ya Bugando,wilayani Geita ndani ya mkoa mpya wa GEITA kesho kutwa tarehe 06/10/2012.
Uchaguzi huo unafanyika kufuatia kifo cha diwani ANATORY MKUFU wa CCM.Katika uchaguzi huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kati ya vyama vya CCM na CHADEMA,CHADEMA itashirisha vikosi kutoka ndani ya mkoa wa Geita, Mwanza pamoja na Makao makuu katika kusaka ushindi.Makada na Madiwani wote wa mikoa ya Mwanza na Geita waliohama kutoka CCM na kujiunga CHADEMA watashiriki kikamilifu pamoja na timu yote iliyokiwezesha CHADEMA kuitetea kata ya KIRUMBA jijini MWANZA hapo 01,April 2012, licha ya upinzani mkali na mbinu chafu kutoka CCM,ikiwemo kuraruliwa kwa mapanga baadhi ya wafuasi na madiwani wa CHADEMA usiku wa kuamkia siku ya kupiga kura Kirumba.
Matokeo ya chaguzi ndogo zinazotarajiwa kufanyika katika kata 29 nchini,mnamo tarehe 28-10-2012 yatatumika kama kipimo cha kuweza kufahamu kama harakati za kisiasa zinazoendelea kufanyika nchi nzima chini ya kauli mbiu 'Vuguvugu la Mabadiliko'(Movement For Change) zinafanikiwa au la.Na ili kuhakikisha kuwa kanda ya ziwa ukiwemo mkoa huu mpya wa GEITA, inaendelea kuwa ngome imara ya CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu 2015,viongozi wa Taifa CHADEMA akiwemo katibu mkuu Dr W.Slaa watashiriki pia katika kampeni za Lwenzera.
Chama Cha Wananchi-CUF kinashiriki pia na tayari kimeshazindua kampeni zake juzi,CCM bado na haijajulikana bayana watazindua kampeni zao lini.
Ni kiwaahidi kuwa taarifuni kila kitakachokuwa kinajiri juu ya uchaguzi huu, ni mimi IDIMULWA wa JF.
Uchaguzi huo unafanyika kufuatia kifo cha diwani ANATORY MKUFU wa CCM.Katika uchaguzi huo unaotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kati ya vyama vya CCM na CHADEMA,CHADEMA itashirisha vikosi kutoka ndani ya mkoa wa Geita, Mwanza pamoja na Makao makuu katika kusaka ushindi.Makada na Madiwani wote wa mikoa ya Mwanza na Geita waliohama kutoka CCM na kujiunga CHADEMA watashiriki kikamilifu pamoja na timu yote iliyokiwezesha CHADEMA kuitetea kata ya KIRUMBA jijini MWANZA hapo 01,April 2012, licha ya upinzani mkali na mbinu chafu kutoka CCM,ikiwemo kuraruliwa kwa mapanga baadhi ya wafuasi na madiwani wa CHADEMA usiku wa kuamkia siku ya kupiga kura Kirumba.
Matokeo ya chaguzi ndogo zinazotarajiwa kufanyika katika kata 29 nchini,mnamo tarehe 28-10-2012 yatatumika kama kipimo cha kuweza kufahamu kama harakati za kisiasa zinazoendelea kufanyika nchi nzima chini ya kauli mbiu 'Vuguvugu la Mabadiliko'(Movement For Change) zinafanikiwa au la.Na ili kuhakikisha kuwa kanda ya ziwa ukiwemo mkoa huu mpya wa GEITA, inaendelea kuwa ngome imara ya CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu 2015,viongozi wa Taifa CHADEMA akiwemo katibu mkuu Dr W.Slaa watashiriki pia katika kampeni za Lwenzera.
Chama Cha Wananchi-CUF kinashiriki pia na tayari kimeshazindua kampeni zake juzi,CCM bado na haijajulikana bayana watazindua kampeni zao lini.
Ni kiwaahidi kuwa taarifuni kila kitakachokuwa kinajiri juu ya uchaguzi huu, ni mimi IDIMULWA wa JF.