Evarist Chahali amjutia Rais Magufuli

Evarist Chahali amjutia Rais Magufuli

linapokuja swala la utendaji mzuri wa magufuli ni wachache sana wanapingana naye. hata wapinzani wanakiri kabisa kuwa magufuli anafanya vizuri.
Wapinzani wapi hao, wakina mrema cheyo
 
sio mwandishi huyo,hilo ni shushushu bobefu liloomba hifadhi ya ukimbizi/kisiasa huko scotland kutokana na............alishahadithiaga mwenyewe
 
mh pole kama ulitegemea makubwa kutoka kwa Mr president . lakini alitakiwa kumtathimini kwanza mtu huyo kwa kuangalia historia yake. kumbe lililo msukuma ni hasira na chuki dhidi ya lowasa .na hapo ndo inafaa kufanya maamuzi wakati unapo kuwa huna hasira wala chuki .Mwandishi pole na vumilia maana kura yako inakibali cha miaka mitano.
 
Mimi namuombea sana atawala miaka ya nkamia pia asisahau kumpa udc juma nkamia
 
UKAWA walichemka kumuweka Lowassa, mtu waliyemsema sana kwa ufisadi. Kwa hiyo Chahali akisema alimpigia chapuo Magufuli kwa sababu hiyo, nitamuelewa.

Hususan kwa sababu Magufuli hakuonyesha ujinga wake dhahiri mpaka aliochaguliwa kuwa rais.

..ni kweli kumchukua Lowassa ilikuwa ni kosa kubwa.

..na jinsi alivyoshindwa kujipigia kampeni ilikuwa inakatisha tamaa.

..lakini Chahali naye alikuwa na option ya kutompigia kampeni yeyote yule.

..anayoyafanya Magu sasa hivi siyo mambo ya ajabu hata kidogo kwa wale ambao walikuwa makini kumfuatilia tangu akiwa waziri.

..Kwa hiyo nimeshangazwa kidogo mchambuzi wa kiwango cha Evarist Chahali kutokuweza ku predict Magu atakuwa kiongozi wa aina gani.
 
Ameandika vizuri, ila hapo mwisho bado amerudia kujikanayaga kwamba "tumuombee". Hivi bado mnafikri huyu jamaa anahitaji maombi?? Kama watu wameomba na kupiga magoti tangu 2015 na bado hakuna mabadiliko yoyote zaidi ya kuongezeka kwa ukatili, hapo mnataka aombewe maombi gani zaidi?
Lands maombi tuyaelekeze upande wa Pili maana wa kwanza umedunda[emoji4] [emoji4]
 
NIMESOMA YOTE

NIKIRI KUWA SIJAWAH KUMWOMBEA RAIS YEYOTE NA HAITAKUJA KUTOKEA.
 
Ameandika vizuri, ila hapo mwisho bado amerudia kujikanayaga kwamba "tumuombee". Hivi bado mnafikri huyu jamaa anahitaji maombi?? Kama watu wameomba na kupiga magoti tangu 2015 na bado hakuna mabadiliko yoyote zaidi ya kuongezeka kwa ukatili, hapo mnataka aombewe maombi gani zaidi?
Halafu kingine alichokisahau ni kuhusiana na uchakachuaji wa kura , wako wanaoamini kwamba ccm haikushinda uchaguzi ule , nikiwemo mimi binafsi .

Kwa mfano jimbo la Kyela , mtu aliyetangazwa kuwa ni mbunge hakushinda uchaguzi ule na wananchi wote wanajua .
 
Kwa takribani miaka 2 kabla ya kuanza kampeni za uchaguzi mwaka 2015, nilikuwa napata nakala ya kila wiki ya RaiaMwema. Huwa wanaweka makala zao kwenye mtandao siku kadhaa ya baada ya gazeti kutoka, lakini bado nilikuwa nanunua gazeti hilo ili kuonyesha shukrani kwa makala zao nzuri. Hivyo 'tone' yao ilivyobadilika nilitambua kirahisi. Kuna makahaba jana yalibisha, lakini leo mmoja wa waandishi waliobadilisha 'tone' ya gazeti kakiri hadharani kuwa waliiandika habari 'nzuri' za CCM. Ni matumaini yangu hata ndugu yetu Mwanakijiji akili zitamrudia maana nae hawezi kuenea kwenye 'chupa' kwa muda mrefu.

Ndugu zangu, wengine tunachokipigania ni kikubwa kuliko Lowassa, Mbowe, Sumaye wala Dr. Slaa. Hatuna shida na rais wa sasa na tunapenda afanikiwe ktk mikakati yake, kushinda kwake ndo kushinda kwetu. Kikubwa ni kwamba tunahitaji mageuzi makubwa nchini mwetu, mageuzi ya kukata matawi. Mageuzi hayo hayawezi kuletwa na watu walioyakalia matawi hayo. That is the least we can do for our descendants.
 
Sasa si ahamie CHADEMA awe na Amani

Hahitaji kuhamia cdm ili kuzungumza ukweli. Japo huko ccm mzungumza ni cdm. Huyo Chahali ni mmoja tu ya watu waliojilipua kuzungumza ukweli kwamba kikichotarijiwa toka kwa jamaa sio wanachokiona. Na hapo na bado, wengi huko mbele watafunguka wakiwa wamechelewa na hapo ndio ukweli utakuwa wazi peupe. Ikifikia hapo tutegemee mauaji ya waziwazi. Ila kuna muda wa kujirekebisha, sio lazima useme unaleta maendeleo kwa kupandikiza chuki na kuzuia mawazo tofauti
 
Pole sana Chahali. Sisi tuliomjua huyo bwana mkubwa siku nyingi tulikushangaa sana ulivyoshupaa. Lakini ni vyema kwamba umeshtuka sasa japo it's too late. Lkn pia kuhusu matokeo ya uchaguzi wewe haukuwepo kwahiyo haujui undani wake. Waulize wanaojua watakueleza. Na swala la maombi haliwezekani kufanikiwa kwani ni lazima kwanza anayeombewa atambue makosa yake na ayatubu. Otherwise utaomba mpk uchoke na mwisho utamlaumu Mungu kwamba kasinzia kumbe la muombewaji hana utashi (will power). All in all be blessed for realising your mistakes
 
Pole ndugu, ila mkome kujitoa ufahamu kwa watu wasiojulikana. Uongozi ni karama, na ni kujengwa. Watz bado tuko karne ya 19.
 
Pole ndugu, ila mkome kujitoa ufahamu kwa watu wasiojulikana. Uongozi ni karama, na ni kujengwa. Watz bado tuko karne ya 19.
 
Back
Top Bottom