Pesa hizo zinakwenda wapi? au kama wakubwa ndio wanaokula?Tujiulize sisi wabongo kuna maendeleo gani mpaka sasa? Miji inakosa Umeme maji Safi tunatumia Visima badala ya mabomba ya maji?Rushwa imezidi hakuna Maendeleo yoyote yale Watu wote wanakimbilia mijini na kuacha Vijijini,Ardhi nzuri tunayo Maji ya kutosha tunayo lakini bado mijini tunakosa Umeme na Maji Ya kunywa Je hayo ndio Maendeleo? Tutafika kule tunakokwenda?Mito,Maziwa,tunayo lakini tunashindwa ni jinsi gani namna ya kutumia hiyo Mito na Maziwa?Uchumi tunao lakini tunaukalia Je tutakuwa mpaka lini Masikini wa kuomba omba Misaada kutoka nje?itafika wakati hao wanaotupa Msaada Watachoka kutupa hiyo Misaada na Wataacha kutupa hiyo Misaada tutakuwa Omba Omba Mpaka lini? Watanzania Wenzangu?Tujiulize hilo? kila wakati. Tuache kuogopana kuambiana ukweli na vitendo ndivyo vinavyotakia sio kunyamaza kimya tu.