EU inaingilia siasa za ndani nchini!

EU inaingilia siasa za ndani nchini!

tumewaita/tumewaalika kuangalia (observe) uchaguzi+tumewaomba msaada kugharamia uchaguzi. Sasa umeona wapi observer asiyetoa report? Observers waliotoa report iliyowapendeza mlirudiarudia kuzitangaza report zao mkafurahiii na kucheka hadi mkaachia ushuzi. Hii report ya EU haijawapendeza, mnalialia. Wao walichoona sio lazima na wewe ukione na ni mjinga tu anayelazimisha kila mtu aone kama anavyoona yeye
 
tumewaita/tumewaalika kuangalia (observe) uchaguzi+tumewaomba msaada kugharamia uchaguzi. Sasa umeona wapi observer asiyetoa report? Observers waliotoa report iliyowapendeza mlirudiarudia kuzitangaza report zao mkafurahiii na kucheka hadi mkaachia ushuzi. Hii report ya EU haijawapendeza, mnalialia. Wao walichoona sio lazima na wewe ukione na ni mjinga tu anayelazimisha kila mtu aone kama anavyoona yeye
Mualike mkweo nyumbani halafu akusimange, unamtoa mkuku , tena kwa mkuki!
 
Ahsante sana Mkuu. Pesa yao tamu sana lakini kama hawaridhiki na utawala wa sheria nchini ambapo pia wanatoa pesa nyingi sana wakae kimya lakini wakitia neno KOSA! Baniani mbaya..... Akili za CCM ndivyo zilivyo.

Mnapokea fedha zao kusaidia kuendesha uchaguzi na miradi ya maendeleo Kisha mnawaita waje kuangalia uchaguzi,halafu wakitoa maoni Yao mnakasirika
Akili ya CCM
 
Imarisha taasisi za kidemokrasia ili watu wasiwe na mashaka.Kwani walikuja kwa mwaliko wa nani
Mkuu Demokrasia zimeanza kuuliwa kwenye vyama vya siasa.Katiba ambazo haziruhusu mwanachama kuhoji/kupata haki kortini,kubadili gia angani nk.
 
Hakuna siasa za ndani siku hizi,enzi hizo zimeshapita. Huwezi kufanya mambo ya hovyo kwa watu wako mwenyewe harafu utegemee dunia itakaa kimya.Chukulia mfano kilichotokea Ivory cost, rais ameshindwa uchaguzi na hataki kuachia madaraka na hii ikapelekea machafuko na watu wakauawa.Katika mazingira kama hayo uhuru wako utaingiliwa tu.Kimsingi wako sahihi na kusema kweli walitakiwa kwenda hatua mmoja mbele zaidi.
 
Kama kilichotokea na kinachotokea Libya, Iraq na Syria ndo wao wanakiita eti demokrasia basi ninadhani sisi waafrika aina ya uongozi wetu inafaa kuigwa. Ningewaona wana maana na wanasema wanachokimaanisha kama wangemfufua Gadaffi na kuirudisha Libya ilivyokuwa chini ya Gadaffi. Sijui hawa ni watu wa aina gani ambao wanajifanya kutetea haki za binadamu kwa kushinikiza kuondolewa adhabu ya kifo lakini kumbe wao ndo washenzi wakubuhu. Kwanini kama wanachukizwa na adhabu hii walitenheneza mazingira ya kumuua Gadaffi, hii haki wao waliitoa wapi? Alafu eti leo mtu anaona fahari kusikiliza simulizi za kinafiki za wazungu, ushenzi wa hari ya juu. Na mie nasema kama ningeliweza ningeshiriki Alqueda ili kuhakikisha na wao wanahenya matendo yao ya kishetani hapa duniani wakiongozwa na US
 
Hakuna siasa za ndani siku hizi,enzi hizo zimeshapita. Huwezi kufanya mambo ya hovyo kwa watu wako mwenyewe harafu utegemee dunia itakaa kimya.Chukulia mfano kilichotokea Ivory cost, rais ameshindwa uchaguzi na hataki kuachia madaraka na hii ikapelekea machafuko na watu wakauawa.Katika mazingira kama hayo uhuru wako utaingiliwa tu.Kimsingi wako sahihi na kusema kweli walitakiwa kwenda hatua mmoja mbele zaidi.
Kumbe, si umeona pale US wananchi wako mtaani wanampinga mshikaji kuwa rais, sasa iambie na wewe nchi yako iandike kwamba jamaa ni mbabe na hafai kuongoza wamarekani alafu usubiri kama watakwambia siku hizi hakuna siasa za ndani ..toeni tamko na nyie juu ya Donald.
 
kama huwezi kuona ukweli katika usemi wao ju ya uchaguzi wa Zanzibar basi uko miongoni mwa wale waliosemwa na MH Rais VILAZA! TENA KILAZA GRADE a. Ni bora ungeondolewa akili ukapewa uti wa mgongo peke yake!
Wako sahihi 100%. Hakuna cha kukosoa kwenye usemi wao! mtoa mada pole sana maana inaonekana hujiwezi!!!
 
Kabla ya kuwajibu unatakiwa ujue nafasi yako duniani. Ukweli mchungu ni kwamba ukiwajibu mbofu wanakuvuruga wakati wowote wakijisikia wao. Tena sio lazima walete makombora, wanaweza wakakunyima dawa tu mjiharishie nchi nzima hadi muwaamkie

Sikuwai kuwaza kuwa kuna siku nitamkumbuka Membe

Utajiju. Utamkumbuka mpaka kambona
 
Unataka kusema yule kijana wa Tunisia aliyejimwagia mafuta akajichoma moto hadharani kwa ajili ya kunyanyaswa na askari jiji akitafuta ridhiki ilikuwa ni covert action ya majasusi wa ulaya?
Mkuu Kukukakara, watu wanajitoa akili kwa kutetea upuuzi! Wanajifanya hawajui nini kilitokea Libya. Leo wanajifanya vipofu hata kwa yale yaliyotokea Zanzibar... mwenzao Membe aliamua kuwaambia ukweli lakini hawakumwelewa, wakafikiri ni kwa sababu alikosa nafasi ya kugombea urais...
 
Kama kilichotokea na kinachotokea Libya, Iraq na Syria ndo wao wanakiita eti demokrasia basi ninadhani sisi waafrika aina ya uongozi wetu inafaa kuigwa. Ningewaona wana maana na wanasema wanachokimaanisha kama wangemfufua Gadaffi na kuirudisha Libya ilivyokuwa chini ya Gadaffi. Sijui hawa ni watu wa aina gani ambao wanajifanya kutetea haki za binadamu kwa kushinikiza kuondolewa adhabu ya kifo lakini kumbe wao ndo washenzi wakubuhu. Kwanini kama wanachukizwa na adhabu hii walitenheneza mazingira ya kumuua Gadaffi, hii haki wao waliitoa wapi? Alafu eti leo mtu anaona fahari kusikiliza simulizi za kinafiki za wazungu, ushenzi wa hari ya juu. Na mie nasema kama ningeliweza ningeshiriki Alqueda ili kuhakikisha na wao wanahenya matendo yao ya kishetani hapa duniani wakiongozwa na US
Mkuu umemaliza mzizi wa fitna.
Leo Waziri wetu wa mambo ya Nje akisimama na kusema Trump ni mufilisi, utalisikia valangati na tifu watakalolizua.
 
Kwani nyie mnazuiwa kuwakosoa au kutoa maoni kwa mambo yao ya ndani? Mbona Trump anaongea shombo kibao lakn mko kimyaa tu,sawa kabisa waongee labda watasaidia kukwangua gamba la njano na kijani
 
p
kama huwezi kuona ukweli katika usemi wao ju ya uchaguzi wa Zanzibar basi uko miongoni mwa wale waliosemwa na MH Rais VILAZA! TENA KILAZA GRADE a. Ni bora ungeondolewa akili ukapewa uti wa mgongo peke yake!
Wako sahihi 100%. Hakuna cha kukosoa kwenye usemi wao! mtoa mada pole sana maana inaonekana hujiwezi!!!
Ni dhambi kubwa mtu mwenye akili kutegemea watu wakuongoze, mnatawaliwa kiakili.
You need mental emancipation.
 
Mnapokea fedha zao kusaidia kuendesha uchaguzi na miradi ya maendeleo Kisha mnawaita waje kuangalia uchaguzi,halafu wakitoa maoni Yao mnakasirika
Akili ya CCM

ukae kwangu bure,msosi bure,halafu unarudi home night kali,nikihoji una mind,jitegemee km North Korea basi uachiwe linchi lako na ubongo wenyewe wa sisimizi huo tuone km hamtakula mizizi
 
Haya mambo waliyoyasema hata sisi wenyewe ndio tunayataka na yalishasemwa na watanzania wengi .wewe mpuuzi mtoa mada hukumbuki marehemu mtikila alifika mpaka mahakamani kudai mgombea binafsi?

Kuhusu suala la kuhoji matokeo yavraisi mahakamani hata katika maoni ya tume ya warioba yalitolewa navwananchi wengi tu tena hata wananchi wachini ndio tunataka matokeo yahojiwe mahakamani

Wewe hutaki wananchi wakosoe watawala wakati mwalimu alisema bila kukosolewa huweza kujijua .unataka sheria ya mtandao ili udikteta uimarike na kukua?
 
Nakubaliana na wewe kwa point ya kutuingilia kimaamuzi, matatizo yetu yatamalizwa na sisi wenyewe. But hii haiondoi ukweli kuwa uchaguzi ulijaa siasa chafu za CCM na haukuwa wa haki kuanzia bara hadi visiwani.
Matatizo yetu huwa hatujui kuyamaliza kwa maridhiano hilo huwa halipo ni ubabe ubabe tu na vitisho wale waangalizi hawakuja ili waende changuu kutizama kasa wanajua kazi waliyoijia wametoa tu ripoti na ushauri tujifunze kukubali ukweli na jamaa wame tuacha na matatizo yetu visiwani tuhangaike nayo hawaja ingilia chochote ila wamesitisha usaidizi hawana desturi ya kufadhili pasipo na Demokrasi kosa lao nini?.
 
Eu wanaingilia mambo ya ndani ya nchi nyingine? Wakati mnawakaribisha kuja kuangalia huo uchaguzi ulikuwa was nchi gani? Na vipi kama wangesema uchaguzi ulikuwa huru na kwamba haukuwa na kasoro, wangekuwa wameingilia pia mambo ya ndani ya nchi nyingine?
 
p

Ni dhambi kubwa mtu mwenye akili kutegemea watu wakuongoze, mnatawaliwa kiakili.
You need mental emancipation.
Mtu akikushauri haitoshi kumaanisha anakuongoza! wewe unajalibu kulipeleka huko iliulinde unachotaka kulinda kwa kuonesha makosa ya wakosoaji! wanakasoro zao sikatai lakini si katika jambo hili wanalolizungumzia!
 
Back
Top Bottom