Je, Wazanzibari Wamehusika?
"Kuangalia tatizo bila kuona ukweli wote ni kama kujaribu kupiga msumeno ukiwa na mwinuko mmoja tu."
Kuna mjadala mkubwa unaendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusu yaliyojiri Oktoba 29, kabla na baada ya siku hiyo. Mojawapo ya hoja zinazojitokeza ni kwamba matatizo ya Tanzania Bara yanatokana na Zanzibar, na si kutoka ndani ya Bara yenyewe. Hoja hii imenichokoza sana. Hebu tuangalie kwa mifano halisi.
Bunge la Jamhuri ya Muungano
Bunge la Tanzania lina takriban asilimia 99 ya wabunge ambao ni Watanzania Bara, wakiwemo Spika, Naibu Spika, Katibu wa Bunge, na wabunge wengine wote. Pia, karibu asilimia 99 ya wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge ni Watanzania Bara.
Hoja: Je, Wazanzibari wanahusikaje hapa?
Jibu: Hakuna ushahidi unaoonyesha Zanzibar inaathiri uendeshaji wa Bunge.
Je, bunge lililo na takriban 97% ya Watanzania Bara litapaza sauti kuhusu yaliyojiri Oktoba 29 na kuwa upande wa kulaumu Zanzibar? Ngoja tuone.
Vyombo vya Habari
Asilimia 99 ya wahariri wa vyombo vya habari nchini ni Watanzania Bara. Taasisi zote kubwa za habari, zikiwemo MOAT na Jukwaa la Wahariri, zinaongozwa na Watanzania Bara.
Hoja zinazoulizwa: Je, ina maana wameshikwa kiakili na Wazanzibari?
Jibu: Vyombo vya habari vinaongozwa na Watanzania Bara; hivyo basi, Wazanzibari wanahusikaje?
Madai ya Askari wa KMKM
Kuna madai kwamba askari wa KMKM waliletwa Tanzania Bara ili kuzuia vurugu. Lakini kumbuka: askari wa KMKM Zanzibar hawazidi 5,000. Tuseme hata kama walioletwa Bara ni mia moja (100), je, inawezekana hawa watu 100 waliweza kuzunguka nchi nzima?
Mfano: Wako Mwanza, wakaja Manzese, Arusha, Mbagala, Katoro, Mara, Shinyanga, kisha wakarudi Ubungo na Goba.
Hilo linaingia akilini kweli? Jamani, tumuogopeni Mungu.
Mahakama
Asilimia 99 ya majaji ni Watanzania Bara, na labda 1% tu ndio Wazanzibari. Je, inawezekana kwamba 1% hii ingeathiri kesi kubwa kama ile ya Lissu au zile zinazohusu Chadema?
Hitimisho: Hoja kwamba Zanzibar inahusika kimsingi katika Mahakama ya Taifa haina msingi wa kweli.
Wafanyakazi wa Serikali
Takribani asilimia 95 au zaidi ya wafanyakazi wa Serikali Bara ni Watanzania Bara. Je, ina maana Zanzibar inahusika katika mambo yanayotokea Bara?
Jibu: Idadi ndogo ya Wazanzibari haiwezi kuwa na mchango mkubwa wa kitaifa kwenye uendeshaji wa Serikali Bara.
Wizara ya Fedha
Waziri, makatibu wakuu, na karibu asilimia 99 ya wafanyakazi wote wa Wizara ya Fedha ni Watanzania Bara.
Swali: Je, Wazanzibari wanahusika vipi?
Jibu: Hoja kwamba Zanzibar inafaidika zaidi chini ya utawala wa Dkt. Samia inahitaji ushahidi zaidi.
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
Msajili, wasaidizi wake, na wafanyakazi wengine wote kwa asilimia 99 ni Watanzania Bara.
Hoja: Hii ina maana Mpina alizuiliwa kwa shindiko kutoka Zanzibar?
Jibu: Hakuna ushahidi wa kuunga mkono hoja hiyo.
Hitimisho
Watanzania Bara, tujiulize tulipoanguka; tusilaumu Wazanzibari. Haiwezekani kuwalaumu watu milioni moja dhidi ya watu milioni sitini wa Bara.
Kama hoja hiyo ingekuwa kweli, basi hawa Wazanzibari milioni moja wangekuwa watu wenye akili ya kipekee — magenius wa hali ya juu!
Watanzania Bara, tuangalie tulipoanguka, tusiwabebeshe lawama
"Kuangalia tatizo bila kuona ukweli wote ni kama kujaribu kupiga msumeno ukiwa na mwinuko mmoja tu."
Kuna mjadala mkubwa unaendelea kwenye mitandao ya kijamii kuhusu yaliyojiri Oktoba 29, kabla na baada ya siku hiyo. Mojawapo ya hoja zinazojitokeza ni kwamba matatizo ya Tanzania Bara yanatokana na Zanzibar, na si kutoka ndani ya Bara yenyewe. Hoja hii imenichokoza sana. Hebu tuangalie kwa mifano halisi.
Bunge la Jamhuri ya Muungano
Bunge la Tanzania lina takriban asilimia 99 ya wabunge ambao ni Watanzania Bara, wakiwemo Spika, Naibu Spika, Katibu wa Bunge, na wabunge wengine wote. Pia, karibu asilimia 99 ya wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge ni Watanzania Bara.
Hoja: Je, Wazanzibari wanahusikaje hapa?
Jibu: Hakuna ushahidi unaoonyesha Zanzibar inaathiri uendeshaji wa Bunge.
Je, bunge lililo na takriban 97% ya Watanzania Bara litapaza sauti kuhusu yaliyojiri Oktoba 29 na kuwa upande wa kulaumu Zanzibar? Ngoja tuone.
Vyombo vya Habari
Asilimia 99 ya wahariri wa vyombo vya habari nchini ni Watanzania Bara. Taasisi zote kubwa za habari, zikiwemo MOAT na Jukwaa la Wahariri, zinaongozwa na Watanzania Bara.
Hoja zinazoulizwa: Je, ina maana wameshikwa kiakili na Wazanzibari?
Jibu: Vyombo vya habari vinaongozwa na Watanzania Bara; hivyo basi, Wazanzibari wanahusikaje?
Madai ya Askari wa KMKM
Kuna madai kwamba askari wa KMKM waliletwa Tanzania Bara ili kuzuia vurugu. Lakini kumbuka: askari wa KMKM Zanzibar hawazidi 5,000. Tuseme hata kama walioletwa Bara ni mia moja (100), je, inawezekana hawa watu 100 waliweza kuzunguka nchi nzima?
Mfano: Wako Mwanza, wakaja Manzese, Arusha, Mbagala, Katoro, Mara, Shinyanga, kisha wakarudi Ubungo na Goba.
Hilo linaingia akilini kweli? Jamani, tumuogopeni Mungu.
Mahakama
Asilimia 99 ya majaji ni Watanzania Bara, na labda 1% tu ndio Wazanzibari. Je, inawezekana kwamba 1% hii ingeathiri kesi kubwa kama ile ya Lissu au zile zinazohusu Chadema?
Hitimisho: Hoja kwamba Zanzibar inahusika kimsingi katika Mahakama ya Taifa haina msingi wa kweli.
Wafanyakazi wa Serikali
Takribani asilimia 95 au zaidi ya wafanyakazi wa Serikali Bara ni Watanzania Bara. Je, ina maana Zanzibar inahusika katika mambo yanayotokea Bara?
Jibu: Idadi ndogo ya Wazanzibari haiwezi kuwa na mchango mkubwa wa kitaifa kwenye uendeshaji wa Serikali Bara.
Wizara ya Fedha
Waziri, makatibu wakuu, na karibu asilimia 99 ya wafanyakazi wote wa Wizara ya Fedha ni Watanzania Bara.
Swali: Je, Wazanzibari wanahusika vipi?
Jibu: Hoja kwamba Zanzibar inafaidika zaidi chini ya utawala wa Dkt. Samia inahitaji ushahidi zaidi.
Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa
Msajili, wasaidizi wake, na wafanyakazi wengine wote kwa asilimia 99 ni Watanzania Bara.
Hoja: Hii ina maana Mpina alizuiliwa kwa shindiko kutoka Zanzibar?
Jibu: Hakuna ushahidi wa kuunga mkono hoja hiyo.
Hitimisho
Watanzania Bara, tujiulize tulipoanguka; tusilaumu Wazanzibari. Haiwezekani kuwalaumu watu milioni moja dhidi ya watu milioni sitini wa Bara.
Kama hoja hiyo ingekuwa kweli, basi hawa Wazanzibari milioni moja wangekuwa watu wenye akili ya kipekee — magenius wa hali ya juu!
Watanzania Bara, tuangalie tulipoanguka, tusiwabebeshe lawama