Mtukutu wa Nyaigela
JF-Expert Member
- Sep 4, 2018
- 6,519
- 11,039
Kuna watu wamekuwa wakijenga hoja kuwa siku hizi watoto wamekosa maadili na hawana heshima. Na wanafika mbali wanalaumu kuwa wazazi ndio chanzo.
Mimi nina mawazo tofauti. Hivi kuna mtoto jeuri kuliko mtoto wa kwanza kuzaliwa hapa duniani kwa mujibu wa Biblia, yaani Kaini. Huyu alimuua mdogo wake. Alitakiwa kutoa sadaka ya kuchinja wanyama, yeye kwa ujeuri wake akasema anaweza kutoa hata mazao ya shambani kwani sadaka ni sadaka tu. Mwisho wa siku sadaka yake ilikataliwa na akawa na hasira
Kuna hawa mapacha waligombana toka tumboni na mwisho mmoja wapo alienda kuishi kwa mjomba wake, naongelea Esau na Yakobo.
Kuna hawa watoto wa Yakobo walimuuza Yusuph, kisha wakamdanganya baba yao kuwa wameokota nguo zake zikiwa na damu kuashiria kuwa kaliwa na wanyama wakali.
Watoto wamekuwa changamoto miaka yote hiyo. Na humo humo utakuta watoto watiifu na wazuri. Changamoto walizopitia wazazi wa zamani kulea watoto ndio hizo hizo wazazi wa leo wanapitia. Tusikate tamaa
Mimi nina mawazo tofauti. Hivi kuna mtoto jeuri kuliko mtoto wa kwanza kuzaliwa hapa duniani kwa mujibu wa Biblia, yaani Kaini. Huyu alimuua mdogo wake. Alitakiwa kutoa sadaka ya kuchinja wanyama, yeye kwa ujeuri wake akasema anaweza kutoa hata mazao ya shambani kwani sadaka ni sadaka tu. Mwisho wa siku sadaka yake ilikataliwa na akawa na hasira
Kuna hawa mapacha waligombana toka tumboni na mwisho mmoja wapo alienda kuishi kwa mjomba wake, naongelea Esau na Yakobo.
Kuna hawa watoto wa Yakobo walimuuza Yusuph, kisha wakamdanganya baba yao kuwa wameokota nguo zake zikiwa na damu kuashiria kuwa kaliwa na wanyama wakali.
Watoto wamekuwa changamoto miaka yote hiyo. Na humo humo utakuta watoto watiifu na wazuri. Changamoto walizopitia wazazi wa zamani kulea watoto ndio hizo hizo wazazi wa leo wanapitia. Tusikate tamaa