Laibon
Member
- Jun 22, 2009
- 9
- 1
Wana JF naomba kutoa hoja;
Kama JK akishinda urais basi ni budi Lowawa awe waziri mkuu kwani alionewa kushinikizwa kujiuzulu.
Wote mnafahamu kuwa hakuna mtu amechukuliwa hatua kwenye RICHMOOND saga- wote wako huru wamesafishwa bungeni na hata, wanapeta kwenye wakiomba kura majimboni kwao na huenda wakashinda kwa kishindo.
Nasema hivi kwasababu ni juzi tu JK alikuwa Monduli na aliambia umma hajawahi ona mchapakazi kama Lowassa. Sasa kama rais na bunge limesafisha, JK akiingia madarakani itakuwa vyema huyu mchapakazi awepo. Lowassa ni mchapakazi,ni jasiri na mwenye maamuzi na hilo halina ubishi, tatizo kubwa ni kwamba amekula sana kuliko wenzake ndio maana hata CCM wenziwe walimkaanga bungeni, lakini si asilimia kubwa ya wana CCM na watendaji wa serikali ni walaji? Hili wote mnalikubali, sasa Lowassa ana kosa gani mbele ya wanaCCM wenzake? Eti amekula sana? Labda mikono yake ni mipana, na kinywa chake kikubwa kiasi kwamba anaweza kula chapati bila kukunja, kwanini asile sana???!
Kama JK akipita namshauri aachane na Pinda, hana ujasiri na sio thabiti kama Lowassa.
Kama wote ni walaji basi tumchague mlaji mchapakazi basi angalau tutaambulia kimoja!
Natoa hoja:eyebrows:
Kama JK akishinda urais basi ni budi Lowawa awe waziri mkuu kwani alionewa kushinikizwa kujiuzulu.
Wote mnafahamu kuwa hakuna mtu amechukuliwa hatua kwenye RICHMOOND saga- wote wako huru wamesafishwa bungeni na hata, wanapeta kwenye wakiomba kura majimboni kwao na huenda wakashinda kwa kishindo.
Nasema hivi kwasababu ni juzi tu JK alikuwa Monduli na aliambia umma hajawahi ona mchapakazi kama Lowassa. Sasa kama rais na bunge limesafisha, JK akiingia madarakani itakuwa vyema huyu mchapakazi awepo. Lowassa ni mchapakazi,ni jasiri na mwenye maamuzi na hilo halina ubishi, tatizo kubwa ni kwamba amekula sana kuliko wenzake ndio maana hata CCM wenziwe walimkaanga bungeni, lakini si asilimia kubwa ya wana CCM na watendaji wa serikali ni walaji? Hili wote mnalikubali, sasa Lowassa ana kosa gani mbele ya wanaCCM wenzake? Eti amekula sana? Labda mikono yake ni mipana, na kinywa chake kikubwa kiasi kwamba anaweza kula chapati bila kukunja, kwanini asile sana???!
Kama JK akipita namshauri aachane na Pinda, hana ujasiri na sio thabiti kama Lowassa.
Kama wote ni walaji basi tumchague mlaji mchapakazi basi angalau tutaambulia kimoja!
Natoa hoja:eyebrows: