Mpishi bora ni yule anayepika chakula vizuri na wala sio uzoefu wa kukaa jikoni miaka mingi.Naomba thread isomeke CDM Vs CCM nani zaidi, maana hapa ishabiki wa kochama hautaleta ukweli maana, huyo Wasira ameonekana jana tu tayari amemzidi mtu ambaye yupo ktk siasa kwa zaidi yake.
Kwa kuweka kumbukumbu sahihi, Coca cola kwa huku afrika mashariki waliendeshaga shindano linaloitwa "COCACOLA POP STAR"
na washindi wake kwa Tz walikuwa "WAKILISHA" ambalo ni kundi lilohusisha Langa, Sarah na Witness.
Ile Pop Idol ya mwaka 2003 ndiyo ilimng'arisha Esther Wasira (ambaye ndiye huyu anayejadiliwa hapa kwa upande mmoja), Terrence na Banana haikuhusika na Coca Cola.
Ni hayo tu Mkuu wangu.
Shukriyah........... Lol!
Umeona eeeeh!!Wassira Ester kitu ingine kabisa mimi nilikuwa simfahamu jana nikawasha itv kusikiliza kongamano la kumkumbuka Kambarage, asalaaale binti nouma sijawahi kuona nilikuwa na kikao cha harusi nikaomba udhuru
Jk unasikia:-? Kama Ester tu anakufunika, je Dr wa ukweli..Umeona eeeeh!!
Kuna taarifa zinadai huyu Esther Wassira ndiye aliyethibitisha kuwa ITV ni Television ya taifa, kwani wakati anaongea kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Nyerere, Rais JK naye alikuwa live TBC katika maadhimisho kama hayo, lakini watu wengi walikuwa wanaangalia ITV kumsikiliza Esther Wassira badala ya kumsikiliza mkuu wa nchi!!!
unasema kweli mkuuUnajaribu kushindanisha mlima na kichuguu!!!!wa CDM ni mlima wa CCM ni kichuguu...!!
Naomba kujuzwa kuna binti wassira mmoja aliwahi kuimba wimbo wa Sheilaa akiwa secondari, hivi ndo huyu Esther.?
Huyu binti namkumbuka akiwa loyola 2003,alikuwa anashindana kwenye mashindano ya muziki ya pop idol,alikuwa mmoja wa waimbaji mahili na nakumbuka alitinga mpaka top 3.
*Esther Bulaya ni mbunge wa kike, kijana kwa tiketi ya CCM viti maalum, watu wengi wamepata kumzungumzia uwezo wake wa kisiasa humu JF mara kadhaa. Ameonekana Bungeni na mara kadhaa kwenye majukwaa ya kisiasa akijenga hoja.
*Esther Wassira alionekana kwa mara ya kwanza kwenye ulingo wa kisiasa siku akichukua kadi ya CHADEMA, watu wengi walitaka kumfahamu uwezo wake wa kisiasa(kujenga hoja na kuamsha ushawishi), na kupitia hotuba aliyoitoa kwenye kongamano la kumbukumbu ya mwalimu Nyerere pale Nkurumah kila mtu sasa anaweza kumzungumzia.
*Sababu za kutaka kuwalinganisha kisiasa.
1/Mfanano wao (Wote ni wanasiasa, vijana, wanawake, wanatoka Bunda, wameshawahi kuwa na mzozo wa kisiasa na Steven Wassira, wote wanaitwa Esther!!)
2/Wanatoka vyama viwili vinavyopinzana.
3/Watu wengi wanataka kuona mmoja wao akirithi kiti cha ubunge wa Steven Wassira kule Bunda 2015.
***Wadau wa JF mnaweza kuchangia kwa kujenga hoja za ulinganifu wao kisiasa.
Anaonekana ni mzalendo na mwanamapinduzi. Ametoka kwenye familia ambayo angeweza kupewa kazi nzuri tena ukizingatia ana ubongo lakini ameacha yote kwa ajili ya umma. nimependa aliposema, yanifaa nini kutumikia familia ya watu 5 wakati naweza kutumikia watanzania milioni hamsini?Esther Wasira Akienda huko bungeni na akagoma kusign posho ya vikao vya bunge nitamuamini,vinginevyo ni yaleyale kugeuzana Mazombi!