Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Aliyekuwa Mbunge wa viti maalumu kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na kada wa chama hicho Ester Bulaya amerejea Chama Cha Mapinduzi (CCM), na kutangaza nia ya kugombea Ubunge wa Jimbo la Bunda Mjini mkoani Mara kupitia CCM.
Bulaya ambaye alijizolea umaarufu mkubwa kupitia CHADEMA amesema alikuwa ndani ya chama hicho kwa mkopo na sasa anarejea nyumbani na kwamba furaha yake ni kuwatumikia wananchi akiwa ndani ya CCM, ambayo ameitaja kama chama chenye dira, maono na dhima ya kweli ya kuwatumikia wananchi.
Soma, Pia: Ester Bulaya aliyekuwa CHADEMA atimkia CCM, achukua fomu ya Ubunge Bunda Mjini
Ester Bulaya ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalumu wa CHADEMA ambao chama hicho kilitangaza kuwavua uanachama, lakini walisalia bungeni hadi kuhitimishwa kwa Bunge la 12 kwa amri ya mahakama.
Bulaya ambaye alijizolea umaarufu mkubwa kupitia CHADEMA amesema alikuwa ndani ya chama hicho kwa mkopo na sasa anarejea nyumbani na kwamba furaha yake ni kuwatumikia wananchi akiwa ndani ya CCM, ambayo ameitaja kama chama chenye dira, maono na dhima ya kweli ya kuwatumikia wananchi.
Soma, Pia: Ester Bulaya aliyekuwa CHADEMA atimkia CCM, achukua fomu ya Ubunge Bunda Mjini
Ester Bulaya ni miongoni mwa wabunge 19 wa Viti Maalumu wa CHADEMA ambao chama hicho kilitangaza kuwavua uanachama, lakini walisalia bungeni hadi kuhitimishwa kwa Bunge la 12 kwa amri ya mahakama.