FortJeasus
JF-Expert Member
- Jan 19, 2012
- 603
- 397
Mbunge wa viti maalum Ester Bulaya (CCM) nae amekanusha kumpigia debe Zitto kwenye Urais.
Kupitia ukurasa wake wa Facebook, ameandika;
"Nasikitika sana kuambiwa kuwa nimempigia debe urais mh Zitto Kabwe. Huu ni uwongo wa kutubwa tulienda Kigoma kuwaunga mkono wasanii wa Kigoma walioamuwa kwenda kuchangisha fedha za ujenzi wa kituo cha vijana. Nilienda kama mbunge wa vijana kwa ajili ya kuunga mkono vijana wenzangu. Huu ni uzushi mkubwa. Natambua kila chama kina utaratibu wa kupata mgombea urahisi"
Nawasilisha
No!
Yawezekana hatujui lugha za kigeni! sawa!Hata lugha zetu zitushinde!Yawezekana jawabu ni typing errors!Iweje sasa yamejitokeza makosa mengi hivi tena katika sentensi chache alizoandika!!Ni wazi Ndugu Mbunge angeamua kuandika kurasa sita angeishia kutufedhehesha sana sisi wadadisi wa mambo!!
Inaudhi kuona makosa ya wazi kama haya yanafanywa na Ndugu Mbunge wa Viti Maalumu ,anayewakilisha Vijana wa CCM!!!
Kama mtu anaonekana hajali kuhariri anayoandika, atawezaje kuchuja anayozungumza na wananchi unaowaongoza?
Kielelezo cha kukosa umakini!