Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum Ester Bulaya ametangaza kuwa atachukua fomu Jimbo la Bunda Mjini kupitia CCM.
Bulaya pia alishawahi kuwa Mbunge wa Jimbo hilo kupitia CHADEMA, amesema anajiandaa kuchukua fomu katika zoezi ndani ya CCM lililoanza leo.
Aliyekuwa Mbunge wa viti Maalum Esther Bulaya ametangaza kuwa atachukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuwania Ubunge Jimbo la Bunda Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Bulaya ambaye awali alikuwa mwanachama wa CCM kabla ya kujiunga na CHADEMA na kurejea CCM hivi karibuni, aliingia kwenye mgogoro na CHADEMA yeye pamoja na Wabunge wenzake 18 mara baada ya kuelezwa kuwa taratibu za wao kupata Ubunge wa viti maalum hazikuzingatia Miongozo na kanuni za CHADEMA, suala ambalo liliwafanya kuwa kimya mpaka Bunge lilipohitimishwa, wachache wao wakionekana kuhamia Vyama vingine.
Bulaya ni miongoni mwa wanawake waliowahi kupata Tuzo ya umahiri kwenye masuala ya jinsia, ikilenga kutambua mchango wake katika kupambana kwenye majukwaa ya kisiasa na kumshinda mwanasiasa mkongwe Steven Wasira kwenye Jimbo la Bunda mwaka 2015
Bulaya pia alishawahi kuwa Mbunge wa Jimbo hilo kupitia CHADEMA, amesema anajiandaa kuchukua fomu katika zoezi ndani ya CCM lililoanza leo.
Aliyekuwa Mbunge wa viti Maalum Esther Bulaya ametangaza kuwa atachukua fomu ya kuomba ridhaa ya kuwania Ubunge Jimbo la Bunda Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Bulaya ambaye awali alikuwa mwanachama wa CCM kabla ya kujiunga na CHADEMA na kurejea CCM hivi karibuni, aliingia kwenye mgogoro na CHADEMA yeye pamoja na Wabunge wenzake 18 mara baada ya kuelezwa kuwa taratibu za wao kupata Ubunge wa viti maalum hazikuzingatia Miongozo na kanuni za CHADEMA, suala ambalo liliwafanya kuwa kimya mpaka Bunge lilipohitimishwa, wachache wao wakionekana kuhamia Vyama vingine.
Bulaya ni miongoni mwa wanawake waliowahi kupata Tuzo ya umahiri kwenye masuala ya jinsia, ikilenga kutambua mchango wake katika kupambana kwenye majukwaa ya kisiasa na kumshinda mwanasiasa mkongwe Steven Wasira kwenye Jimbo la Bunda mwaka 2015