Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 17,456
- 21,167
Bondia Errol Spence Jr (The truth) amefanikiwa kumtwanga vilivyo Yordenis Ugas kwa T.K.O round ya 10 na kufanikiwa kuunganisha mikanda ya WBA, WBC na IBF amebakisha mkanda mmoja tu wa WBO ambao unashikiliwa na Terence Crawford ili awe Undisputed Welterweight Champion.
Error Spence hakuishia hapo tu bali alimuita Terence Crawford (Bud) ili wamalize utata kati yao nani ni bora zaidi.
Bud alirespond kwa kumpongeza na kumtaka awamu hii asitafute visingizio pambano kati yao lifanyike.
Ikumbukwe kabla ya Errol Spence hajapigana na Yordenis Ugas ilibidi apambane na Manny Pacquiao ila pambano halikuwezekana kutokana na Errol Spence kupata ajali na hivyo pambano likawekwa kati ya Yordenis Ugas na Manny Pacquiao na Yordenis akafanikiwa kumsambaratisha vipande vipande Manny Pacquiao na kumstaafisha kabisa.
Pambano la Error Spence na Crawford kama litafanyika bila shaka litavunja na kuweka rekodi mpya mbalimbali.
Error Spence hakuishia hapo tu bali alimuita Terence Crawford (Bud) ili wamalize utata kati yao nani ni bora zaidi.
Bud alirespond kwa kumpongeza na kumtaka awamu hii asitafute visingizio pambano kati yao lifanyike.
Ikumbukwe kabla ya Errol Spence hajapigana na Yordenis Ugas ilibidi apambane na Manny Pacquiao ila pambano halikuwezekana kutokana na Errol Spence kupata ajali na hivyo pambano likawekwa kati ya Yordenis Ugas na Manny Pacquiao na Yordenis akafanikiwa kumsambaratisha vipande vipande Manny Pacquiao na kumstaafisha kabisa.
Pambano la Error Spence na Crawford kama litafanyika bila shaka litavunja na kuweka rekodi mpya mbalimbali.