Ergonomic Keyboards

castongo

Member
Mar 16, 2008
57
67
Umewahi kusikia kuhusu ergonomic keyboards? Ni computer keyboards ambazo, funguo zake zimepangwa kwenye muundo tofauti kitaalam kulingana na mwelekeo wa mwili wa mwanadamu. Kwamba computer keyboards zile za kawaida funguo zake zinakua zimepangwa tu kwenye safu zilizo nyooka, na kumfanya anayechapisha kubana viwiko kwenye ubavu. Lakini hizi zinampa mtu nafasi ya kujiachia kidogo kama kujinafasi.
Niliposoma article fulani kuhusu keyboard hizi nikapuuzia, nikajua zitakua zinapatikana mbele.
Juzi katika pitapita yangu Kariakoo, kwenye duka la vifaa used vya computer, nikaona keyboard hizi. Nikauliza nikatajiwa 10,000. Nikaombaomba hadi 5,000 nikachukua. Ni moja yenye muundo wa "V"
ergo_02.jpg

Hasara ya keyboard ya namna hii ni kwamba inahitaji kamuda kidogo kuzoea, pia inawafaa zaidi wale wanaochapisha bila kuangalia keyboard. Wachunguliaji wasinunue maana italeta ugumu zaidi katika kutafuta herufi. Wakati fulani nilijizoesha kuchapisha herufi "B" kwa mkono wa kulia, baadae nikagundua ni makosa, nikaanza kuirudisha kwenye mkono wa kushoto, sasa naona faida yake. Maana hapa B imewekwa kushoto.
Hapa nimeshajizoesha kidogo na imeanza kunoga. Wakati mwingine kujaribu mambo tofauti, inapendeza zaidi.
 
hata kwa buku 10 sio shida!, hebu nambie hilo duka lipo kwa wapi?
 
hata kwa buku 10 sio shida!, hebu nambie hilo duka lipo kwa wapi?
Ukitokea makutano ya Uhuru na Msimbazi, ukiendelea na Uhuru kwenda makutano ya Uhuru na Congo, maduka ya vifaa vya computer upande wako wa kulia. Naona risiti hapa imeandikwa Juba Computers
 
Ukitokea makutano ya Uhuru na Msimbazi, ukiendelea na Uhuru kwenda makutano ya Uhuru na Congo, maduka ya vifaa vya computer upande wako wa kulia. Naona risiti hapa imeandikwa Juba Computers
Ila nilizoacha pale sidhani kama zipo kwenye shape sana, pengine hawakua na bidii ya kuangalia zaidi. Lakini nadhani hata ukipita kwenye maduka ya jirani jirani pale zitakuwepo tu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom