Erdogan ameapa kujenga upya mji uliokumbwa na Tetemeko

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,331
33,141
Erdogan ameapa kujenga upya mji uliokumbwa na Tetemeko.jpeg

erdogan / Photo: AA Archive
Rais wa Uturuki ameapa kulijenga upya eneo la kusini mwa nchi hiyo kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililosababisha vifo vya zaidi ya watu 50,000 mwezi uliopita.

"Lengo letu ni kuinua eneo la tetemeko la ardhi," Recep Tayyip Erdogan alisema Jumapili baada ya chakula cha jioni na waathiriwa wa tetemeko la ardhi huko Istanbul, wakati wa mlo maalumu wa kufuturu kwa Waislamu katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.

Türkiye inapanga kujenga majengo ya kutosha katika mwaka mmoja ili kukidhi mahitaji ya waathirika wa tetemeko hilo, Erdogan alisema, akiongeza kuwa nyumba 319,000 zitajengwa katika mwaka wa kwanza na 650,000 kwa jumla.

Pia aliahidi kuponya majeraha ya waathiriwa.

Mnamo Februari 6, matetemeko ya nguvu ya 7.7 na 7.6 yalipiga mikoa 11 ya Uturuki - Adana, Adiyaman, Diyarbakir, Elazig, Hatay, Gaziantep, Kahramanmaras, Kilis, Malatya, Osmaniye, na Sanliurfa.

Zaidi ya watu milioni 13.5 huko Türkiye wameathiriwa na matetemeko hayo, pamoja na wengine wengi kaskazini mwa Syria.

chanzo. Erdogan ameapa kujenga upya mji uliokumbwa na Tetemeko - TRT Afrika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom