Wakuu, nimepitia kurasa za mitandaoni kama Jumia na Kuoatana na kukutana na tangazo la Epson L382 ikiwa dukani kuuzwa. Nimejisikia kuipenda, lakini nataka kujua kitu kuihusu. Najua humu kuna wataalamu waliobobea kuihusu kabisa.
Naomba kujua changamoto za hii Printer na iwapo inafaa kwa matumizi ya Stationary ambapo sina photocopier, yaani naitegemea hiyo kwa kutoa kopi na ku-print, pia ku-scan. Vipi?! Inaweza kunipa faida au?
L382, sio heavy duty printer ila ni economical. kutumia katika stationery inaweza kukuangusha kutokana na Spidi yake ndogo wakati wa kutoa copy ukilinganisha na laserjet printers/copiers.
**hizi ni Hasara zake:
- Slow copying
-spidi ya kuprint sio tatizo ingawa haifikii laserjet
-Reset software yake inaweza kuwa inakugharimu kiasi ukifikisha page kama kila 1000 pages.
-huwezi kuset number of copies wakati wa kutoa copy
-huwezi kuseti contrast/brightness ya copy
-error message huwa zinatokea kwenye computer
**Hizi ni faida zake:
-economical, hapo utafurahia gharama ndogo ya wino
-Print quality ni nzuri sana na colored(Ukitumia karatasi nzuri huwa inapiga hadi 5760dpi)
-ni special kwaajili ya kuPrint picha kwa kutumia photo paper (Kama za epson glossy au clarion glossy)
-Rahisi kuoperate na kuweka wino.
-Wino mwingi bei rahisi (Tafuta wino mzuri)
-ina uweza kuprint hadi karatasi ngumu za gramate 300 au zaidi kidogo, hapo utaprint hadi business cards, vipeperushi, brochures......
Ushauri; ukipata L210 naiaminia zaidi.