English Premiership: 2010-2011

Abdulhalim

Platinum Member
Jul 20, 2007
17,193
3,011
Nduguzanguni, wapenzi wa kabumbu..

Karibu katika ukumbi wenu muupendao ikiwa leo tarehe 15 mwezi wa nane, mwaka 2010, ni siku ile ambapo twakata utepe wa hiki kinyang'anyiro cha ligi bora zaidi kwenye sayari hii kama sio kwenye galaxi tuliyomo.

Basi wale wapenzi wenye mahaba na thread za vilabu sio mbaya mkichangia na huku, wajameni!!


Ratiba ya ufunguzi ni kama ifuatavyo:

Aug 14 11:45 GMT Tottenham Hotspur v Manchester City White Hart Lane

Aug 14 14:00 GMT Aston Villa v West Ham United Villa Park

Aug 14 14:00 GMT Blackburn Rovers v Everton Ewood Park

Aug 14 14:00 GMT Bolton Wanderers v Fulham Reebok Stadium

Aug 14 14:00 GMT Sunderland v Birmingham Stadium of Light

Aug 14 14:00 GMT Wigan Athletic v Blackpool The DW Stadium

Aug 14 14:00 GMT Wolverhampton Wanderers v Stoke City Molineux Stadium

Aug 14 16:30 GMT Chelsea v West Bromwich Albion Stamford Bridge
 
Kama kawaida ya thread za michezo, utabiri ni jadi, basi sina budi kusema ni wapi naweka shilingi yangu mapema.

Mwaka huu au kwa hakika zaidi msimu huu, bila ubishi ubingwa utaondoshwa kule darajani, na kazi kubwa ya ushindani itabakia ktk timu za Manchester, yaani United na City, lakini mwisho wa siku nataraji Mashetani Wekundu wataibuka kidedea. Nafasi ya 3 itakuwa ngumu kutabiri kwa sasa, lakini Chelsea ipo mbele ya Liverpool, Arsenal, Spurs na Everton, natumai hawatajivunga.

Natabiri kuwa na ligi ya msisimko mkali zaidi mwaka huu kuliko mwaka jana, na tuombeane uzima kwetu washabiki na wachezaji tuwaombee uzima na afya, haswa ikikumbwa hawa ndio wanatufanya tuwe na kitu cha kusimulia.
 
Kwasababu mpira unadunda....Karata yangu nairusha kwenye Bwawa La Maini.

Najua wengi wataniona kreze lakini ndio hivyo tena, kila mtu ana chembe chembe za Sheikh Yahya Hussein wake.

Kwa kuanzia na kwa msisitizo ; Kesho Arsene Wenger anapelekewa kilio...........Go Liverpool Go!
 
Kwasababu mpira unadunda....Karata yangu nairusha kwenye Bwawa La Maini.

Najua wengi wataniona kreze lakini ndio hivyo tena, kila mtu ana chembe chembe za Sheikh Yahya Hussein wake.

Kwa kuanzia na kwa msisitizo ; Kesho Arsene Wenger anapelekewa kilio...........Go Liverpool Go!

Bingwa,

Unatabiri kuhusu mechi au ubingwa?
 
Ubingwa mzee. Najua ntaonekana kreze lakini mpira unadunda na msimu huu lazima kombe litue Anfield!

Hapa tatizo sio kuenekana kreze.....ila tayari wewe ni kreze!
Wachambuzi wengi wanaipa ze bluz nafasi ya kutetea kombe....
Mi naina Man U ikiwa imebeba kombe lake hapo Mei 2011!:A S soccer:....Man U are going for # 19, remember?

BTW: Msimamo wa ligi ni huu kwa sasa...

1 Arsenal
2 Aston Villa
3 Birmingham
4 Blackburn
5 Blackpool
6 Bolton
7 Chelsea
8 Everton
9 Fulham
10 Liverpool
11 Man City
12 Man Utd
13 Newcastle
14 Stoke
15 Sunderland
16 Tottenham
17 West Brom
18 West Ham
19 Wigan
20 Wolves

Ze gunaz oyee...
 
Spurs na City wapo uwanjani hivi sasa, mpambano mkali kwelikweli.

Dk 14 bado 0:0
 
City hawa wachezaji iliowasajili sidhani kama wataiweza EPL, mhh..
 
Mtanange umefikia nusu, bado milango haitaki kufunguka. Lets wait for the 2nd half.
 
Hapa tatizo sio kuenekana kreze.....ila tayari wewe ni kreze!
Wachambuzi wengi wanaipa ze bluz nafasi ya kutetea kombe....
Mi naina Man U ikiwa imebeba kombe lake hapo Mei 2011!:A S soccer:....Man U are going for # 19, remember?

BTW: Msimamo wa ligi ni huu kwa sasa...

1 Arsenal
2 Aston Villa
3 Birmingham
4 Blackburn
5 Blackpool
6 Bolton
7 Chelsea
8 Everton
9 Fulham
10 Liverpool
11 Man City
12 Man Utd
13 Newcastle
14 Stoke
15 Sunderland
16 Tottenham
17 West Brom
18 West Ham
19 Wigan
20 Wolves

Ze gunaz oyee...

Teams letter that begins with "W" are going to struggle this season and possibly three of them relegated (West Brom West Ham Wigan Wolves )
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom