Engineers wa Tanzania

Engineers wa Tanzania

LTK

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2013
Posts
267
Reaction score
99
Engineer wa Tanzania ni hasara sana, yani baada ya kumaliza masomo yao na kufanikiwa kupata kazi, wao hubweteka huko makazini na hakuna maendeleo yoyote ki ujuzi wanayo jiendeleza, kinachobaki anafanya kazi kwa mazoe kwasababu unakuta kakalili machine aina flani au program, siku waki badilisha mfumo alio kua kazoe ana buma ile Mbeya.

Dunia ya sasa ki teknolojia ina badilika kila siku ila Engineer wetu wapo pale pale hawa move na teknolojia, kwasababu hawana tabia ya kujifunza vitu vipya, wao kazi yao ni Service na troubleshooting.

Na ndio maana hata company nyingi zina ajiri wataalamu kutoka nje na si kwamba hapa kwetu hawapo, ila tatizo letu ni watu wa kubweteka hatwendi na dunia ya Teknolojia na hatutaki kujifunza vitu vipya.

Wosia wangu kwenu mnaojiita ma Engineer unakuta hata ERB haiwatambui, mmbadilike ili twende na kasi ya madiliko kwa maendeleo ya nchi yetu.
 
LTK haujafanya stadi ya kutosha kuweza kufahamu fika kwa nini Wahandisi wetu unadhani ni wavivu wa kutafuta elimu na maarifa mapya. Ukiwa na Degree na unafanya kazi ya "See-and-Do" ambayo hata form six anaiweza, unahitaji Masters au PhD ya nini? Elimu hiyo unayoiita ndogo bado hawapewi nafasi ya kuiweka kwenye uzalishaji. Serikali inawasomesha lakini zikija kazi wanawapa wageni kwa kisingizio kwamba hawana ujuzi! Kama hawana ujuzi nani aliwaandalia mitaala yenye elimu ya utapia mlo? Na kwa nini basi kusiwepo na mpango maalumu wa hao wenye ujuzi kufanya kazi na wazawa ili Taifa lisibaki tegemezi milele?
 
Ericus Kimasha , kidogo nimebahatika kufanya kazi na baadhi ya Engineer wa hapa kwetu na nje pia, kuna mambo ambayo kipindi nafanya kazi nilikua ni ya study kwa umakini sana. Swala la mitaala kuna tatizo, na hili tatizo linatokana na vyuo vyetu kutokua na ushirikiano na sehemu za uzalishaji ili wao kujua ni aina gani ya vitu vya kuingizwa katika mtaala au kuvitoa katika mtaala husika, na ndio maana hadi leo hii ukitazama mitaala ya vyuo vyetu ni ile ya zamani isiyo na tija wala haiendani na mahitaji yaliyopo ivi sasa. Engineer wetu tatizo lao kubwa kwanza ni wavivu na ni watu wa kulidhika na ninafikiri hii watanzania wengi tunalo, kuna baadhi ya hawa hawa Engineer wetu wenye juhudi na walijitoha haswa katika kile walicho kisomea wapo mbali na ni mategemeo katika company baadhi, hata hao white colour wana wagwaya katika swala zima la kazi. Swala la kupata ujuzi kutoka kwa wenzetu kuna shida, hasa upande wetu hatupo makini na ni wavivu, nimeisha shuhudia watu wana acha kazi kutokana na kuhimizwa kufanya kazi na kujifunza mambo mapya

LTK haujafanya stadi ya kutosha kuweza kufahamu fika kwa nini Wahandisi wetu unadhani ni wavivu wa kutafuta elimu na maarifa mapya. Ukiwa na Degree na unafanya kazi ya "See-and-Do" ambayo hata form six anaiweza, unahitaji Masters au PhD ya nini? Elimu hiyo unayoiita ndogo bado hawapewi nafasi ya kuiweka kwenye uzalishaji. Serikali inawasomesha lakini zikija kazi wanawapa wageni kwa kisingizio kwamba hawana ujuzi! Kama hawana ujuzi nani aliwaandalia mitaala yenye elimu ya utapia mlo? Na kwa nini basi kusiwepo na mpango maalumu wa hao wenye ujuzi kufanya kazi na wazawa ili Taifa lisibaki tegemezi milele?
 
Last edited by a moderator:
Hawa watoto wa form six wanaenda lini chuo? Wamechafua kweli nyumba muda huu wa waliokua nyumbani! Na hivi vi 50MB vya mini kabang na wenzake; na simu za kupewa na kaka....imekua kero kwa kweli!! Heri waende chuo wakawe bize tupumuwe kidogo...
 
Engineer wa Tanzania ni hasara sana, yani baada ya kumaliza masomo yao na kufanikiwa kupata kazi, wao hubweteka huko makazini na hakuna maendeleo yoyote ki ujuzi wanayo jiendeleza, kinachobaki anafanya kazi kwa mazoe kwasababu unakuta kakalili machine aina flani au program, siku waki badilisha mfumo alio kua kazoe ana buma ile Mbeya.

Dunia ya sasa ki teknolojia ina badilika kila siku ila Engineer wetu wapo pale pale hawa move na teknolojia, kwasababu hawana tabia ya kujifunza vitu vipya, wao kazi yao ni Service na troubleshooting.

Na ndio maana hata company nyingi zina ajiri wataalamu kutoka nje na si kwamba hapa kwetu hawapo, ila tatizo letu ni watu wa kubweteka hatwendi na dunia ya Teknolojia na hatutaki kujifunza vitu vipya.

Wosia wangu kwenu mnaojiita ma Engineer unakuta hata ERB haiwatambui, mmbadilike ili twende na kasi ya madiliko kwa maendeleo ya nchi yetu.

Samahani wewe ni mtaalamu wa nini au fani yako ni nini au elimu yako ya juu kabisa ni ipi?Ukishajibu hayo itatuwia rahisi sana kukujibu maana itatusaidia kujua tunaongea na mtu wa aina gani!Wakati mwingine mtoto wa darasa la saba unamjibu kilasaba la saba,wa form 4 kiform 4,wa six kisix six,chuo kichuo chuo,mwanasiasa kisiasasiasa,mwalimu kuualimu alimu,enginer kihandisi handisi.Mwenzetu unaangukia wapi tukujibu!
 
Watoto wa form six hawana haki ya kujua na kutoa mawazo?
Nyie ndio mnao lifanya hili taifa kua la watu wachache kutoka na ubaguzi wenu, wa kupokea hoja na michango kutoka katika kada mbali mbali.

Hawa watoto wa form six wanaenda lini chuo? Wamechafua kweli nyumba muda huu wa waliokua nyumbani! Na hivi vi 50MB vya mini kabang na wenzake; na simu za kupewa na kaka....imekua kero kwa kweli!! Heri waende chuo wakawe bize tupumuwe kidogo...
 
Engineers always build the world,wapo mainjinia majembe sana..kiteknoham awapo juu..serikali legelege haiwatambui tu.
 
Hatujaja humu kujuana taaluma au level za kielimu. Kama umeelewa mada jibu ka manufaa ya wote na sio kuweka matabaka.

Samahani wewe ni mtaalamu wa nini au fani yako ni nini au elimu yako ya juu kabisa ni ipi?Ukishajibu hayo itatuwia rahisi sana kukujibu maana itatusaidia kujua tunaongea na mtu wa aina gani!Wakati mwingine mtoto wa darasa la saba unamjibu kilasaba la saba,wa form 4 kiform 4,wa six kisix six,chuo kichuo chuo,mwanasiasa kisiasasiasa,mwalimu kuualimu alimu,enginer kihandisi handisi.Mwenzetu unaangukia wapi tukujibu!
 
Mkuu useamcho ni kweli, wapo majembe na wasio majembe. Tujiulize hao majembe wamefanyaje hadi kua hivyo? na hao wasio kua majembe tatizo liko wapi?
Wapo baadhi nilio fanya nao kazi mfano Makoi, huyu ni marehemu, jamaa alikua ni hatari sana hadi wahindi wana mnyoshea mikono, ila ilitokana na jamaa kua na juhudi zake binafsi na kujituma kwa moyo mmoja.

Engineers always build the world,wapo mainjinia majembe sana..kiteknoham awapo juu..serikali legelege haiwatambui tu.
 
LTK nashukuru kwa majibu yako yanaoungana na mtazamao wangu juu ya chanzo cha tatizo. Kwa mfano ukiniuliza kwa nini Wahandisi wa St. Joseph University wako kiutendaji na wanaanza taratibu kuteka hisia na mahitaji wa Waajiri, jibu nitakupa kwamba inatokana na chuo kuwa na sera za kuchunguza na kubadili Masomo mara kwa mara ili yaendane na mahitaji ya soko pamoja na mabadiliko ya Kiteknolojia.

Niliwahi kuhoji kwa Mhadhiri wa Chuo Kimoja kikongwe kutaka kujua kama kwenye Kitivo cha Biashara, Kitengo cha Masoko wana topiki ya Digital marketing akanijibu hawana, nikamuuliza wa Kitivo cha Uhandishi wa Electrics & Electronics kama wanafunzi wake wanafahamu lolote kuhusiana na Termination of Fiber Optic wote wakajibu hizo topiki hawana. Kilichofuata nikataka kujua kwa nini muda wote huo soko limekuwa na mahitaji mapya na Chuo Kikubwa kama kile hakijawa na topiki hizi? Nilikuja kubaini kuwa ili Mtaala wa Chuo ubadilishwe lazima Senate ikae. Na kikao cha Kujadili mapungufu au kupokea mapendekezo ya Mabadiliko ya Mtaala kinafanyika kila baada ya miaka mitatu! Huu ni muda mrefu sana kwenye tasnia za Biashara, Uhandisi na Teknolojia kuwa kumeibuka elimu na maarifa mapya. Kwa mfumo huu nacherea kusema kwamba vyuo vikuu vya umma vinaweza kuwa vinawafundisha wanafunzi elimu iliyopaswa kutumika juzi ambayo maarifa yake yamepitwa na wakati na hayana soko wala tija kwenye mahitaji ya soko la leo. Kuna wadau ambao ni waajiri wakubwa East Africa baada ya kuona ombwe hili wameamua kuhitisha mkutano mwezi ujao. Kwa taarifa zaidi fuatilia hapa:
The Academia - Private Sector Partnership Forum and Exhibitions 2013


blank.gif
blank.gif
 
  • Thanks
Reactions: LTK
Ericus Kimasha
Ulichosema ni kweli 98%, pia hata ukiangalia hiki kitu kinaitwa Contet delivery network ni kitu ambacho ni marketable ila hatuna wajuzi katika sehemu kama hizi na ndipo hapo unakuta company inaingia gharama kuchukua watu nje. Hapa kuna ulazima wa mabadiliko kuanzia kwenye mitaala, na sio mitaala tu na wale wanao simami mabadiliko ya hivi vitu hapo ndipo kiini cha kufanya mtaala uwe bora au mmbaya, pia hata kupunguza mda wa kuifanyia madiliko, atleast iwe baada ya mwaka mmoja , kwa miaka mitatu katika swala la Teknolojia kuna kua na mambo mengi sana yamebadilika.
asante sana kwa hiyo link uliyonipatia.
 
Last edited by a moderator:
Ku-single out wahandisi siyo busara maana udhaifu huo na mapungufu hayo yameathiri fani zote.

Wahandisi wote walisoma masomo ya sayansi (ambayo wengine waliyakimbia kutokana na ugumu wao) na wakafaulu vizuri sana. Hii ni kusema wahandisi are one of the best brains in the world. Tofauti ni kwamba nchi za wenzetu zinawatumia wahandisi kukuza uchumi wao huku tz tukielekeza nguvu zetu kwenye siasa na kuabudu wawekezaji.

Wahandisi wengi ninaowafahamu wameacha hata kufanya kazi za kihandisi kwa kuwa walichosoma hawakifanyii kazi na maslahi na heshima ni ndogo hivyo kushawishika kuingia fani nyingine. Kuna wahandisi ni bankers wazuri tu
 
Watanzania tuache kulalamika,kila mtu afanye wajibu wake then nchi itapiga hatua kubwa sana kimaendeleo!Tatizo tunasubiri mtu fulani afanye,maisha hayaendi Engineers hawajafanya hivi,madaktari hawajafanya hivi!
Nchi ni sawa na gurudumu la baiskeli ambalo lina spoku nyingi ambazo ni kila raia katika nafasi yake na fani yake.Spoku moja au mbili au tatu au nne zinapokatika baiskeli haiwezi kutembea vizuri.Vivyo hivyo katika jamii husika(nchi),daktari afanye kazi yake,mwalimu afanye kazi yake,mhandisi(Engineer) naye kadharika,mwanasiasa naye kazi yake,wahasibu kazi yao,wana habari kazi yao,mahakimu kazi yao,na kadharika na kadharika.
Kila mtu anapofanya wajibu wake vizuri basi itatoa mwanya wa kila mmoja kuconcentrate kwenye kazi yake tu na hapo ndo tutakaposhuhudia uvumbuzi wa teknolijia na mambo mbalimbali yatayolisaidia taifa,mitaala mizuri ya elimu itaandaliwa kwa kuwa watunga sera watakuwa hawana wasiwasi na maisha,wanajua watoto wao wakiugua watatibiwa vizuri na hata hao walioko shule watasoma vizuri.Mhandisi naye ataconcentrate tu kwenye kazi yake ambapo atavumbua(design) mifumo mbalimbali kwa kuwa anajua mtoto wake atasoma shule nzuri na hata akiugua atapata huduma stahiki.Mwalimu naye ataconcentrate vzr na kuwapatia wanafunzi(hao unaotaka wawe maengineer) elimu nzuri baada ya kuwa hana tena mawazo ya nitakula nini au wanangu ada wataitoa wapi!
Husiseme ma Engineer hawajafanya kitu,wanajitahidi sema tu wamesongwa na ugumu wa maisha unaosababishwa na kila mtu kutofanya kazi yake ipasavyo.Tulikuwa na kiwanda chetu cha magari Nyumbu,wahandisi wazalendo walikuwepo kiko wapi sasa?Kiwanda cha baiskeli Avon kiko wapi na wahandisi wetu?Mmmh sio wahandisi tu kila mmoja katika fani yake ajitahidi.Tuna madaktari wangapi wa falsafa,iwe ya siasa,ya uchumi,ya sayansi ya jamii,ya uhandisi n.k wote hawa tunawategemea kuleta mawazo yao na yafanyiwe kazi ili kuleta tija na maendeleo katika nchi yetu.
Kila mmoja kwa nafasi yake afanye wajibu wake!
 
LTK we ni NGWINI TU...HUNA LOLOTE,UHANDISI TUACHIE SISI WE KAPIGE SOGA NA SECRETARY.
 
Wahandisi ni watu muhimu sana katika nchi yoyote ile inayotaka maendeleo ya kiteknolojia tatizo la hapa kwetu ni siasa ndio imeingia katika mfumo wa elimu vifaa vinavyotumika kufundishia vimepitwa na wakati na kingine ni mitaala yetu haimuandai mtu kuwa practical and theory oriented bali inamuandaa tu kumanage tu na sio kufikiria kutatua tatizo na kutafuta best way ya kusolve problems..mf yale majengo yaliyoanguka DSM ni uzembe kuanzia contractor,client, na engneer ambapo vilevile engineer anaweza kuwa ndani ya contractor tatizo lilitokea pale ni kutumia njia ya kizamani katika ujenzi ambapo wenztu wanatumia LABORATORY TESTING kabla ya kujenga jengo na vitu vingine vinavyohusiana na uhandisi kabla ya kupeleka katika actual field....hapo utagundua kuwa bado tuko nyuma katiak suala la mitaala na system nzima ya kufundisha wahandisi ambao ndio tegemeo kubwa la maendeleo ya nchi hii
 
Back
Top Bottom