Eneo la Kunduchi Skanska Kurudishwa Serikalini?

Eneo la Kunduchi Skanska Kurudishwa Serikalini?

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
17,016
Reaction score
26,192
Kama utakuwa umewahi kufika katika Jiji la Dar es salaam Wiliya ya Kinondoni mitaa ya SKANSKA basi utakubaliana na mimi kuwa pale Mashimoni-Mtongani ndiyo mitaa yenye Waswahili wengi Kinondoni Nzima. Kila siku watu wanazidi kuongezeka , HAKUNA MPANGILIO WALA MPANGO.

2015 PALIKUWA PANACHIMBWA MAWE. SERIKALI ILIPASWA KUCHUA NA KUPIMA VIWANJA VYENYE ROBO HEKA NA NUSU HEKA NA KUWEKA BARABARA KUBWA AU BASI KUJENGA CHUO NA KITUO CHA POLISI.

NATUMAINI BADO SERIKALI INAWEZA KULICHUKUA HILI ENEO .

b.jpg
 
Kila nikifika hapa najiuliza maswali mengi kuhusu hizi nyumba

Eniwei nakuwa nafurahia zaidi view ya bahari tuu
WAsomi tusaidieni, hawa watu siku wakipata moto ni janga la kitaifa, patatekea pote, hakuna miundombinu ya uokozi.

Hapo unakuta kuna bosi yupo Ardhi ni afisa mipango miji anazungusha kitabi na kufutia miwani sijui wanapewa mishahara ya nini.
 
WAsomi tusaidieni, hawa watu siku wakipata moto ni janga la kitaifa, patatekea pote, hakuna miundombinu ya uokozi.

Hapo unakuta kuna bosi yupo Ardhi ni afisa mipango miji anazungusha kitabi na kufutia miwani sijui wanapewa mishahara ya nini.
Yaani walikwisha kosea aseeh.... Hapo sjui hata miundo mbinu ya dawasa inapitaje huko ni uswahilini tosha 😂
 
Yaani walikwisha kosea aseeh.... Hapo sjui hata miundo mbinu ya dawasa inapitaje huko ni uswahilini tosha 😂
Buza ya Uzunguni, lakini nafasi ipo. Serikali iwafidie majengo yao, ichukue iwekek viwanja vikubwa watumishi wa mahakamani au maafisa wa serikli ambao ni wasafi , zingatia ambao ni wasafi , wapewe waishi hapo.
 
Nimepita hapo mara kadhaa kwa shughuli flani. Nahisi kuna hoja inajengwa ili Watu/Mtu achukue eneo hilo. Eneo la Mecco linapitika vizuri, hakuna maji kutuama kwa sababu lipo juu ya usawa wa bahari. Kuna nyumba nyingi nzuri tu kama unavyoona kwenye view ya picha huko juu. Hakuna makelele ya soko au vilabu vya pombe za kienyeji. Kama ilivyo kwa maeneo mengine ya Dar, kuna upungufu wa barabara. Hivi hiyo Mecco unalinganishaje na Manzese, Tandale, Tabata Dampo nk nk.
 
Back
Top Bottom