Sote humu ndani ya hili _kundi sogozi_tunamiliki _simu tamba_. Tuweni makini kwani kutumia _sikanu_ zetu _mkondoni_ kunaweza wapa mwanya wezi wa mtandaoni kutuibia. Wezi hutuma _maunzi laini_ yanayoweza kuharibu _kitumi_ chako au kuingilia _makavazi_ ya _sikanu_ yako. Wakishatuma _maunzi laini_ hayo nawe pasi na kujua ukibofya _kiungo_ kilichobeba _maunzi laini_ unakuwa _umeshapakua_ na _kusanidi mtaliga_ wenye uwezo wa kubadili au _kughushi nenomsingi_ lako na hivyo kunyima uwezo wa kuitumia _sikanu_ yako kwa kuifanya _*puku_ kushindwa kutambua amri unazoipatia _baobonye_ ya _kiwambagusa_ cha _sikanu_ yako.
lJE KISWAHILI KITUMIKE KAMA LUGHA YA KUFUNDISHIA KWA NGAZI ZOTE ZA ELIMU?