mmmuhumba
JF-Expert Member
- Nov 8, 2017
- 491
- 476
ELIMU WAKATI TULIONAO NA TUENDAPO
Kwa nchi nyingi za Afrika, elimi ni kurithisha maarifa, stadi na ujuzi kwa mwanafunzi katika eneo maalumu. Hata katika jadi ilikuwa ni hivyo hivyo ambapo walirithisha ujuzi, maarifa na stadi kwa vijana kwa kuzingatia umri na jinsia.
Katika mabadiliko ya dunia, elimu sasa ina sura mbili ya kurithisha na kukuza kile alichonacho mtu kichwani. Tanzania bado tupo katika mfumo wa jadi wa kurithisha tunamchukulia mtoto kama mtu asiye na chochote kichwani, hivyo anatakiwa kupewa maarifa, stadi na ujuzi.
Yapo mambo yanayokwamisha tuwe kwenye duara la elimu tegemezi, watumishi wasio hali, mambo haya yanafanya elimu ikose muelekeo sahihi kulingana na mabadiliko ya dunia, sera za nchi, uchumi wa serikali katika ajira, mazingira na watumishi kama ifuatavyo:
Kuendana na wakati. Mitaala inatakiwa ibadilike kufuata muelekeo wa elimu kidunia, sera za nchi na mahitaji ya jamii, badala tu ya kuingiza kitu kwa mwanafunzi sasa zinapaswa na kukuza kile kitu alichonacho mwanafunzi. Hii itajenga teknolojia na wawajibikaji maana wanafanya wanachokipenda. Mfano tuna watumishi hawakuwa na ndoto ya kazi wanazofanya ila mfumo wa elimu umewapeleka huko.
Ziwepo posho za mazingira magumu ya kazi. Ni ukweli yapo mazingira magumu katika utendaji, ndio maana wengi wanakimbilia mijini na maeneo nafuu. TAMISEMI iangalie namna ya kuweka utaratibu utaokuwa chini ya halmashauri kutoa posho za mazingira magumu. Mwl. J.K. Nyerere alipoanzisha vijiji vya ujamaa, alitambua, kuna changamoto kimazingira katika kutoa huduma za kijamii, hivyo ni bora watu wakae sehemu moja.
Sasa leo ni wakati mwingine serikali kupitia wizara ione tija katika hili.
Vyuo vya ufundi vijengwe vijijini. Unapotembelea katika wilaya zetu utakuta vijiji vingi kiwango cha elimu cha watu wake kipo chini( darasa la 7,kidato cha 2 na 4). Ni wazi rasilimali watu wa eneo husika ni duni, uwepo wa vyuo vya ufundi ingesaidia kuwapatia nafasi ya kupata utaalam na vyeti wakaingia katika mfumo rasmi wa uzalishaji kama udereva, ufundi, kilimo, uvuvi, uvunaji misitu, nishati endelevu, ufugaji nk.
Zipo halmashauri uchumi wake na hali ya maisha ni duni kutokana na elimu ni duni. Tuwekeze katika vyuo vya ufundi.
Elimu itazame upya ukomo wa maisha. Ni muhimu kufanya tafiti na uzuri sensa imepita, serikali kupitia wizara wafanye tathimini juu ya idadi ya madarasa anayopaswa kusoma mtu, umri wa kuanza hadi kumaliza, umri wa ajira, kustaafu na hali ya starehe ya maisha nchini. Umri wa elimu nchini ni mrefu ukilinganisha na ukomo wa maisha (miaka 7 shule msingi, miaka 4 sekondari, miaka 2 sekondari tena na chuo miaka 3,4, 5 na kuendelea ). Kuna haja ya kujenga taifa la wasomi ila wanao yafurahia maisha ya elimu na ukomo wao wa maisha.
Wizara isimamie haki na maslahi ya walimu sekta binafsi. Kuna anguko kubwa la mishahara, kuna wingi wa mikataba feki ila walimu hawalipwi hii mishahara wala hizo stahiki zilizoanishwa, BIMA hakuna. Serikali inapoteza pesa kwa wasomi waliokopa, wengi wapo sekta binasfi ila hawawezi kulipa madeni na serikali inakosa kodi katika mishahara ya walimu sekta binafsi kwa uduni wa mishahara na malipo yake hayapo katika mifumo rasmi.
Elimu iendane na soko la ajira la dunia. Tukubali serikali ina mzigo mkubwa wa vijana wanaotaka ajira, lazima tuwaandae vijana kifikra na kitaaluma ili waendane na soko la ajira ndani na nje. Ushauri, Serikali ione namna ya kuunganisha vyuo vyetu vya ndani na vyuo vya nje kitaaluma, kimkakati, kwa mbadilishano kupitia ufundishaji wa teknolojia ya mbali na mualiko. Tumudu lugha za mataifa, diplomasia, historia, utamaduni na sanaa.
Kozi za mafunzo ya ualimu msingi ngazi ya 4, 5 na 6 (NTA Diploma ) zilirudishwe walimu wa shule za msingi waweze kujiendeleza. Naishauri pia Wizara hili suala lipewe sekta binafsi kuliendesha kwani itafufua vyuo na serikali itanufaika kwa kuongeza umahili, kodi na kupanua wigo wa tafiti za elimu, ajira na matumizi ya teknolojia katika ufundishaji kwa kuwa sekta binafsi ni uwekezaji mkubwa usiotaka pesa ya serikali.
Wizara izingatie haya:
Masomo ya ziada yasiwekewe vikwazo. Masomo ya ziada wakati wa masomo na wakati wa likizo yaachwe. Yanasaidia kumjenga mwanafunzi awe na uwezo wa kupambanua mambo, kuchambua mambo na kilinganisha mambo. Umpa nafasi ya kubadili mazingira ya ujifunzaji na kujipima katika mazingira mengine.
Inasaidia wahitimu kujiajiri na kujengwa kwa taasisi za ustawi wa jamii zenye kutoa huduma za elimu na malezi.
Kutafsiri vyema sera za elimu ili kutoua ushiriki wa wadau wa elimu hususani wazazi na walezi. Mfano, tafsiri ya elimu bila malipo imepunguza kwa kiwango kikubwa ushiriki wa wazazi katika maendeleo ya shule, kumekuwa na mvutano kati ya walimu na wazazi na kumekuwa na kutokuaminiana kati ya mwalimu na mzazi.
Uhamasishaji wa elimu ufanyike vijijini na miradi inapokuja wapewe wasomi waliopo katika maeneo hayo ili kuzidi kuonyesha umuhimu wa elimu katika vijiji hivyo. Maeneo ya vijijini bado elimu imekuwa ni sehemu tu ya kupeleka watoto wakakue na sio kwa malengo kwamba watapata maisha bora ndio maana asilimia kubwa ni darasa la saba hadi kidato cha nne na baada ya hapo wengi wanakuwa tu mtaani, ile thamani ya elimu haipo.
Uchumi wa viwanda ni lazima tutengeneze rasilimali watu wenye ujuzi husika. Hili ni suala la elimu kuendana na sera za nchi ya viwanda.
Viongozi waache kudharau michepuo ya elimu nchini. Kwasasa sanaa sio bora, bora sayansi huku ni kuua sekta binafsi za elimu nchini. Bunge kikatiba Mbunge inahitaji kujua kusoma na kuandika, mahakama haina wanasayansi.
Wito wangu kwa Watanzania, tushiriki kikamilifu katika elimu, sisi ndio wadau wakuu wa elimu nchini ni lazima tushiriki kimawazo, kimali na kinguvu na huu ni wajibu sio hiari.
Wito wangu kwa wizara, itazame haya kwa jicho la tatu.
Na mmmuhumba
0624 440 454
Kwa nchi nyingi za Afrika, elimi ni kurithisha maarifa, stadi na ujuzi kwa mwanafunzi katika eneo maalumu. Hata katika jadi ilikuwa ni hivyo hivyo ambapo walirithisha ujuzi, maarifa na stadi kwa vijana kwa kuzingatia umri na jinsia.
Katika mabadiliko ya dunia, elimu sasa ina sura mbili ya kurithisha na kukuza kile alichonacho mtu kichwani. Tanzania bado tupo katika mfumo wa jadi wa kurithisha tunamchukulia mtoto kama mtu asiye na chochote kichwani, hivyo anatakiwa kupewa maarifa, stadi na ujuzi.
Yapo mambo yanayokwamisha tuwe kwenye duara la elimu tegemezi, watumishi wasio hali, mambo haya yanafanya elimu ikose muelekeo sahihi kulingana na mabadiliko ya dunia, sera za nchi, uchumi wa serikali katika ajira, mazingira na watumishi kama ifuatavyo:
Kuendana na wakati. Mitaala inatakiwa ibadilike kufuata muelekeo wa elimu kidunia, sera za nchi na mahitaji ya jamii, badala tu ya kuingiza kitu kwa mwanafunzi sasa zinapaswa na kukuza kile kitu alichonacho mwanafunzi. Hii itajenga teknolojia na wawajibikaji maana wanafanya wanachokipenda. Mfano tuna watumishi hawakuwa na ndoto ya kazi wanazofanya ila mfumo wa elimu umewapeleka huko.
Ziwepo posho za mazingira magumu ya kazi. Ni ukweli yapo mazingira magumu katika utendaji, ndio maana wengi wanakimbilia mijini na maeneo nafuu. TAMISEMI iangalie namna ya kuweka utaratibu utaokuwa chini ya halmashauri kutoa posho za mazingira magumu. Mwl. J.K. Nyerere alipoanzisha vijiji vya ujamaa, alitambua, kuna changamoto kimazingira katika kutoa huduma za kijamii, hivyo ni bora watu wakae sehemu moja.
Sasa leo ni wakati mwingine serikali kupitia wizara ione tija katika hili.
Vyuo vya ufundi vijengwe vijijini. Unapotembelea katika wilaya zetu utakuta vijiji vingi kiwango cha elimu cha watu wake kipo chini( darasa la 7,kidato cha 2 na 4). Ni wazi rasilimali watu wa eneo husika ni duni, uwepo wa vyuo vya ufundi ingesaidia kuwapatia nafasi ya kupata utaalam na vyeti wakaingia katika mfumo rasmi wa uzalishaji kama udereva, ufundi, kilimo, uvuvi, uvunaji misitu, nishati endelevu, ufugaji nk.
Zipo halmashauri uchumi wake na hali ya maisha ni duni kutokana na elimu ni duni. Tuwekeze katika vyuo vya ufundi.
Elimu itazame upya ukomo wa maisha. Ni muhimu kufanya tafiti na uzuri sensa imepita, serikali kupitia wizara wafanye tathimini juu ya idadi ya madarasa anayopaswa kusoma mtu, umri wa kuanza hadi kumaliza, umri wa ajira, kustaafu na hali ya starehe ya maisha nchini. Umri wa elimu nchini ni mrefu ukilinganisha na ukomo wa maisha (miaka 7 shule msingi, miaka 4 sekondari, miaka 2 sekondari tena na chuo miaka 3,4, 5 na kuendelea ). Kuna haja ya kujenga taifa la wasomi ila wanao yafurahia maisha ya elimu na ukomo wao wa maisha.
Wizara isimamie haki na maslahi ya walimu sekta binafsi. Kuna anguko kubwa la mishahara, kuna wingi wa mikataba feki ila walimu hawalipwi hii mishahara wala hizo stahiki zilizoanishwa, BIMA hakuna. Serikali inapoteza pesa kwa wasomi waliokopa, wengi wapo sekta binasfi ila hawawezi kulipa madeni na serikali inakosa kodi katika mishahara ya walimu sekta binafsi kwa uduni wa mishahara na malipo yake hayapo katika mifumo rasmi.
Elimu iendane na soko la ajira la dunia. Tukubali serikali ina mzigo mkubwa wa vijana wanaotaka ajira, lazima tuwaandae vijana kifikra na kitaaluma ili waendane na soko la ajira ndani na nje. Ushauri, Serikali ione namna ya kuunganisha vyuo vyetu vya ndani na vyuo vya nje kitaaluma, kimkakati, kwa mbadilishano kupitia ufundishaji wa teknolojia ya mbali na mualiko. Tumudu lugha za mataifa, diplomasia, historia, utamaduni na sanaa.
Kozi za mafunzo ya ualimu msingi ngazi ya 4, 5 na 6 (NTA Diploma ) zilirudishwe walimu wa shule za msingi waweze kujiendeleza. Naishauri pia Wizara hili suala lipewe sekta binafsi kuliendesha kwani itafufua vyuo na serikali itanufaika kwa kuongeza umahili, kodi na kupanua wigo wa tafiti za elimu, ajira na matumizi ya teknolojia katika ufundishaji kwa kuwa sekta binafsi ni uwekezaji mkubwa usiotaka pesa ya serikali.
Wizara izingatie haya:
- Usimamizi wa mitihani udhibitiwe kama wa utaratibu wa necta katika upakiaji wake.
- Kuandaliwa kwa rasimali za ufundishaji na ujifunzaji kwani mitaala ipo.
- Vyuo binafsi vipewe kuendesha hii kozi.
Masomo ya ziada yasiwekewe vikwazo. Masomo ya ziada wakati wa masomo na wakati wa likizo yaachwe. Yanasaidia kumjenga mwanafunzi awe na uwezo wa kupambanua mambo, kuchambua mambo na kilinganisha mambo. Umpa nafasi ya kubadili mazingira ya ujifunzaji na kujipima katika mazingira mengine.
Inasaidia wahitimu kujiajiri na kujengwa kwa taasisi za ustawi wa jamii zenye kutoa huduma za elimu na malezi.
Kutafsiri vyema sera za elimu ili kutoua ushiriki wa wadau wa elimu hususani wazazi na walezi. Mfano, tafsiri ya elimu bila malipo imepunguza kwa kiwango kikubwa ushiriki wa wazazi katika maendeleo ya shule, kumekuwa na mvutano kati ya walimu na wazazi na kumekuwa na kutokuaminiana kati ya mwalimu na mzazi.
Uhamasishaji wa elimu ufanyike vijijini na miradi inapokuja wapewe wasomi waliopo katika maeneo hayo ili kuzidi kuonyesha umuhimu wa elimu katika vijiji hivyo. Maeneo ya vijijini bado elimu imekuwa ni sehemu tu ya kupeleka watoto wakakue na sio kwa malengo kwamba watapata maisha bora ndio maana asilimia kubwa ni darasa la saba hadi kidato cha nne na baada ya hapo wengi wanakuwa tu mtaani, ile thamani ya elimu haipo.
Uchumi wa viwanda ni lazima tutengeneze rasilimali watu wenye ujuzi husika. Hili ni suala la elimu kuendana na sera za nchi ya viwanda.
Viongozi waache kudharau michepuo ya elimu nchini. Kwasasa sanaa sio bora, bora sayansi huku ni kuua sekta binafsi za elimu nchini. Bunge kikatiba Mbunge inahitaji kujua kusoma na kuandika, mahakama haina wanasayansi.
Wito wangu kwa Watanzania, tushiriki kikamilifu katika elimu, sisi ndio wadau wakuu wa elimu nchini ni lazima tushiriki kimawazo, kimali na kinguvu na huu ni wajibu sio hiari.
Wito wangu kwa wizara, itazame haya kwa jicho la tatu.
Na mmmuhumba
0624 440 454