Baraza la Famasi Tanzania
Member
- Mar 27, 2025
- 33
- 45
Baraza la Famasi kwa kushirikiana na Kitengo cha Elimu ya Afya kwa Umma, Wizara ya Afya limeendelea na zoezi la kuelimisha umma kuhusu kazi na majukumu ya Baraza pamoja na kuhamasisha jamii juu ya matumizi sahihi ya dawa.
Kampeni hii iliyoanza juzi, imeendelea tarehe 06 Mei, 2025 katika Mkoa wa Morogoro na imeweza kufikia wananchi wengi zaidi kwa kutoa elimu katika Kituo cha bajaji na bodaboda cha Juwata, Soko la Mawenzi na Stendi Kuu ya mabasi ya Mkoa (Msamvu).
Aidha, katika zoezi hili jamii imepata wasaa wa kuuliza maswali na kupata majibu ya papo hapo ili waweze pia
kuwa mabalozi wazuri wa kuhamasisha matumizi sahihi ya dawa.
“Nimeelimika na nitazingatia Matumizi Sahihi ya Dawa”
Kampeni hii iliyoanza juzi, imeendelea tarehe 06 Mei, 2025 katika Mkoa wa Morogoro na imeweza kufikia wananchi wengi zaidi kwa kutoa elimu katika Kituo cha bajaji na bodaboda cha Juwata, Soko la Mawenzi na Stendi Kuu ya mabasi ya Mkoa (Msamvu).
Aidha, katika zoezi hili jamii imepata wasaa wa kuuliza maswali na kupata majibu ya papo hapo ili waweze pia
“Nimeelimika na nitazingatia Matumizi Sahihi ya Dawa”