Elimu kuhusu majini kabla ya binadamu

Elimu kuhusu majini kabla ya binadamu

hamis77

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
18,250
Reaction score
26,641
Uislamu wa Majini na Historia Yao Kabla ya Mtume Muhammad ﷺ
FB_IMG_1756452967951.jpg

Katika Qur’ani na Hadithi, kuna maelezo yanayosema kuwa majini waliumbwa kabla ya binadamu, na walikuwa na uwezo wa kubeba dini na kumwabudu Allah. Hii inatupa msingi wa hoja na maswali mengi sana kwasisi tunaopenda kutoka nje ya box, tunapata hoja za kiimaninzinazohusu uislamu wa majini kabla ya Mtume Muhammad ﷺ kuja duniani.


1. Uislamu wa majini kabla ya kuzaliwa kwa binadamu

Qur’ani inasema
“Sizani kwa ajili ya ibada yangu tu, nimewazalia binadamu na majini.” (Surah Adh-Dhariyat 51:56)


Hii inaonyesha kuwa majini waliumbwa ili kumwabudu Allah, na hivyo katika hali ya asili walikuwa waislamu

Aidha, Qur’ani inabainisha kuwa majini walikuwepo kabla ya binadamu (Surah Al-Hijr 15:27):

“Na jinn tumewatengeneza kabla ya kumuumba binadamu kutoka makundi ya matope yanayokauka.”


Kwa hivyo, kwa mtiririko wa muda, majini walikuwepo kwanza, na binadamu walifuatia baadaye.


2. Majini na uislamu wa asili

Majini walikuwa wamislamu kabla ya kuzaliwa kwa Muhammad ﷺ.

Kwa hivyo, kwa mtazamo wa historia ya dini, majini walikuwa na dini ya uislamu kabla ya Mtume Muhammad ﷺ kuja duniani.

Hata hivyo, Muhammad ﷺ ndiye Mtume wa mwisho, na Qur’ani ilitolewa kwake ili kurekebisha na kurudisha njia halisi ya ibada ya Allah, kwa binadamu na majini wote.


3. Swali la msingi: Majini walitegemea vitabu vya kale vya Allah?

Qur’ani inataja vitabu vilivyoletwa kabla ya Qur’ani: Torati, Zaburi, Injili (Surah Al-Maidah 5:44-46):

“Hakika tumepewa Torati, ndani yake kuna nuru na hukumu… Zaburi tumeileta Daudi… na Injili tumempa Isa, mtoto wa Maryam…”

Majini waliokuwa wamislamu walipokea mwongozo kupitia vitabu hivi.

Hata hivyo, binadamu waliharibu baadhi ya vitabu hivyo, na hivyo majini walikosa kupata mafundisho ya moja kwa moja, kama ilivyotokea kwa binadamu.


Qur’ani inatufundisha:

“Lakini wao walikosa kuzingatia wito huu; wengi wao ni wapotofu.” (Surah Al-Ahqaf 46:29-30)


Kwa maneno mengine, majini walijua dini ya Allah, walikuwa wamislamu kwa asili, lakini hawakuwa na vitabu vyote vya Allah kwa moja kwa moja.

4. Muhammad ﷺ na majini

Muhammad ﷺ alikuwa Mtume wa binadamu na majini wote (Surah Al-Jinn 72:1-2):

“Sikika kutoka majini, wakasema: Tumemsikia mtu akitaja Qur’ani ya kushangaza, inatuongoza katika njia ya haki…”


Hapa tunaona kuwa majini walifuata Qur’ani na uongozi wa Mtume ﷺ, wakithibitisha kuwa walikuwa tayari wamislamu.

Mantiki inaonyesha kuwa majini walikuwa wamislamu kabla ya Mtume ﷺ, lakini walihitaji mwongozo wa Qur’ani kwa sababu mafundisho ya awali yaliharibiwa au kupotoshwa na binadamu.


5. Maswali ya kiufahamu

1. Majini walipokea dini ya Allah kwa asili, waliikubalije Qur’ani na kuifuata wakati Muhammad ﷺ alipoisoma. Je, walijua mafundisho yote yaliyokuwa yametoweka katika Torati, Zaburi, na Injili?

2. Kwa nini binadamu waliharibu vitabu vya Allah, na majini hawakuweza kuziokoa vitabu hivyo?


3. Je, waislamu majini waliweza kudumisha maneno ya Allah kifuani mwao? Ikiwa ndiyo, je, kwanini Qur’ani ilihitajika kutolewa kwa Muhammad ﷺ?
 
Kwani haiwezkn bila kuutaja Uislamu??

Mbona mara zote mada zako ni juu ya Uislamu??

Kwanini usijiulize toka kuanzishwa Roman Catholic Kuna makanisa yasiyo na idadi??

Kwann msiutafute huo upendo wa Kristo mkawa kitu kimoja ikawa mnafuasa yeye ??

Achana na dini za watu!!

Uislamu umekamilika Mash'Allah 😍 cc Poor Brain ukhty BICHWA KOMWE - Jumaa Karim!
 
Quran 55:56
"Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.

Kumbe Majini hayo pia yana wanawake.
Na yana fanya mapenz kama watu.

Ila hapa Majini yameubwaa ili kupotosha na kushirikiana na binadamu.👇👇👇

Quran 6:128
"Na ile Siku atapo wakusanya wote awaambie: Enyi makundi ya majini! Hakika nyinyi mmechukua wafuasi wengi katika wanaadamu. Na marafiki zao katika wanaadamu waseme: Mola Mlezi wetu! Tulinufaishana sisi na wao. Na tumefikia ukomo wetu ulio tuwekea. Basi Mwenyezi Mungu atasema: Moto ndio makaazi yenu, mtadumu humo, ila apendavyo Mwenyezi Mungu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mwenye hikima, na Mwenye kujua"
 
Quran 55:56
"Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.

Kumbe Majini hayo pia yana wanawake.
Na yana fanya mapenz kama watu.

Ila hapa Majini yameubwaa ili kupotosha na kushirikiana na binadamu.👇👇👇

Quran 6128
"Na ile Siku atapo wakusanya wote awaambie: Enyi makundi ya majini! Hakika nyinyi mmechukua wafuasi wengi katika wanaadamu. Na marafiki zao katika wanaadamu waseme: Mola Mlezi wetu! Tulinufaishana sisi na wao. Na tumefikia ukomo wetu ulio tuwekea. Basi Mwenyezi Mungu atasema: Moto ndio makaazi yenu, mtadumu humo, ila apendavyo Mwenyezi Mungu. Hakika Mola wako Mlezi ni Mwenye hikima, na Mwenye kujua"
Wewe unatatzo mahali si bure
 
Usiwe na jazba.

Hayo ni maneno ya Quran.
Kama nimetoa tafsiri sio sahihi rekebisha.

-Nimeonyesha tu kuwa majini yana wanawake
-majini yatapata wafuasi wengi.

Na kuwa Uislam unashirikiana na majini
Sina la kukujibu maana unaweza jifunza mwenyew hayo yote
 
Bila shaka Kuna uhusiano mkubwa kati ya Watu na majini.

(Tumeonyesha aya na sura nying sana za Quran zenye ushirikiano huo).

Lakin sio watu wote. Bali ni wale walio Waislam.

Na Majini hayo yamepewa ruhusa ya kukaa katika mwili wa Muislam yeyote,

hivyo kila Muislam ana Jini kuanzia moja na kuendelea.

Vile vile Majini wameruhusiwa kukaa katika nyumba za Waislam hata msikitini. Na Katika nyumba yoyote ya Muumini wa dini hiyo, kuna Jini au Majini wanaokaa humo.

Ni ukweli usiopingika kuwa bila Majini hakuna Uislamu.
Ni kama vile pasipo Roho Mtakatifu hakuna Ukristo.

Na Majini ndiyo yaliyomchukua mtume Muhamad kwa muda wa siku 40 akiwa Mapangoni walikompeleka na kuanza kumuagiza kuhusiana na kuanzisha imani hiyo ya Kiislamu.

NB
Hapa sijasema shetani. Nimesema jini mzur (kama mnavyosema kuwa wako majini wazuri na wabaya).
Basi huyo Jibril ni jini mzuri na ndio alimfundisha Mohamed Quran.
 
Mosi, Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasalllam hakiwahi kufuga jini.

Hicho kizibao cha picha ulichokiweka imma kimefanyiwa ghushi au aliyeongea hayo hana elimu ya dini.

Pili, kwa nini unalazimisha tufanane? Ninyi kwenu majini mna taswira mnayowapa nasi kwetu majini ni viumbe miongoni mwa viumbe vya Mungu. Kazi waliyoumbiwa hao majini ni moja tu kama ya mwanadamu, nayo ni kumtumikia Mungu (kumuabudu).

Sasa usilazimishe mazingira, kama kwenu ni sita kwetu ni tisa.
 
Bila shaka Kuna uhusiano mkubwa kati ya Watu na majini.

(Tumeonyesha aya na sura nying sana za Quran zenye ushirikiano huo).

Lakin sio watu wote. Bali ni wale walio Waislam.

Na Majini hayo yamepewa ruhusa ya kukaa katika mwili wa Muislam yeyote,

hivyo kila Muislam ana Jini kuanzia moja na kuendelea.

Vile vile Majini wameruhusiwa kukaa katika nyumba za Waislam hata msikitini. Na Katika nyumba yoyote ya Muumini wa dini hiyo, kuna Jini au Majini wanaokaa humo.

Ni ukweli usiopingika kuwa bila Majini hakuna Uislamu.
Ni kama vile pasipo Roho Mtakatifu hakuna Ukristo.

Na Majini ndiyo yaliyomchukua mtume Muhamad kwa muda wa siku 40 akiwa Mapangoni walikompeleka na kuanza kumuagiza kuhusiana na kuanzisha imani hiyo ya Kiislamu.

NB
Hapa sijasema shetani. Nimesema jini mzur (kama mnavyosema kuwa wako majini wazuri na wabaya).
Basi huyo Jibril ni jini mzuri na ndio alimfundisha Mohamed Quran.
Sasa majibu unayo unauliza ili iweje?

Unataka kubishana?
 
Na Majini hayo yamepewa ruhusa ya kukaa katika mwili wa Muislam yeyote,

hivyo kila Muislam ana Jini kuanzia moja na kuendelea.

Vile vile Majini wameruhusiwa kukaa katika nyumba za Waislam hata msikitini. Na Katika nyumba yoyote ya Muumini wa dini hiyo, kuna Jini au Majini wanaokaa humo.
Duh,
Kobaz na mijini ni kama uji na mgonjwa
 
Kwanza fafanua swali 3 likae kisomi lieleweke

Pili hoja zako unataka zijibiwe Kwa general knowledge au maandiko?

Mwisho, kama maandiko ni yapi unayakubali torat, injili zabur au Quran?
Swali linasema Je majini walitegemea Vitabu mnayoamini?

Hoja zangu nataka zijibiwe kwa Torati, zaburi na injili yaani vile vitabu mlivyoambiwa mkaulize kwa waliokuwa kabla yenu

Pia unaweza kujibu kwa historia na vitabu kabla ya Muhammad

Nakubali maandiko yote isipokuwa Quran sababu inapingana na vitabu vilivyotangulia
 
Ila mm nae natafuta ugomvi.
Nilitakiwa kukaa kimya.

Mosi, Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasalllam hakiwahi kufuga jini.

Mtume Mohamed alikuwa Binadamu.
Ila alikuwa na majini.

Sasa hoja ya kutokufuga majini hapa haipo.

Maana Kama anaweza kuongea na majini. Basi jua na yeye pia ana majini.

Simple as that.

Mtu akikuroga ina maana anakutupia majini wachafu.
Ref majini waliotumwa kwa suleiman.

Na Mtume alirogwa. Na alitupiwa majini(hao majini wabaya unaosema)

Sasa Hoja yangu.
Baada ya mtume kurogwa
Ni Nani aliwatoa hao majini kwake?.

Ili tujue yale aliyokuwa anaongea kwa maswahaba na kuita Quran kwamba sio ya huyo Jini mbaya. (Mnaemwita Shetan kwenye Quran).

Cc
Al-mukheef
Munch wa annabelletz47

Kama Quran inasema Suleiman alisaidiwa na Majini

Quran 21: 81 -82
"Na tukamsahilishia Suleiman upepo wa kimbunga wendao kwa amri yake kwenye ardhi tuliyo ibarikia. Na Sisi ndio tunao jua kila kitu.
Na pia mashet'ani wanao mpigia mbizi na kufanya kazi nyenginezo. Na Sisi tulikuwa walinzi wao."

Tutakataaje kusema kuwa Shetan kamsaidia Mohamed kuandika Quran.
 
Kwani haiwezkn bila kuutaja Uislamu??

Mbona mara zote mada zako ni juu ya Uislamu??

Kwanini usijiulize toka kuanzishwa Roman Catholic Kuna makanisa yasiyo na idadi??

Kwann msiutafute huo upendo wa Kristo mkawa kitu kimoja ikawa mnafuasa yeye ??

Achana na dini za watu!!

Uislamu umekamilika Mash'Allah 😍 cc Poor Brain ukhty BICHWA KOMWE - Jumaa Karim!
Mashaallah udugu wangu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom