Watoto wako shule ndugu hawawezi subiri. JPM mwenyewe hakusubiri akutane na wadau waelimu ili ajue nini changamoto za elimu na ni njia ipi ifanyike ili elimu bure iwezekane. Yeye alikurupuka bila hata kuwa na waziri wa elimu. hakujipa hata muda, sasa kwanini unataka sisi wananchi tunaoumia tumpe muda? Mbona hakuwapa muda hao aliowasimamisha kazi na kuwafukuza? Rais aache kukurupuka asiongoze nchi kama shule.U
Ukishaingia u ccm na uchadema mambo yanaharibika utaifa unafutika, uzalendo unayeyuka! Rais Magufuli ameingia madarakani akiwa na nia ya kutaka kurekebisha mambo mengi yaliyoharibika ikiwemo Elimu. Ninaamini kwamba kama zingekuwepo fedha za kutosha asingesita kuagiza zielekezwe sehemu zilizo na upungufu. Pia, waziri wa Elimu Watanzania wengi wanamkubali kwamba anao uwezo wa kusimamia mageuzi katika elimu nchini. Inasikitisha kuona ndani ya miezi mitatu tu ya awamu ya 5 watu wanataka mambo yabadilike. Magufuli ameonyesha nia njema, jukumu letu in kumpa muda na ushirikiano ili juhudi zake za kutuletea maendeleo zizae mtunda.