Wana JF, mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Edward N Lowasa alijiuzulu uwaziri mkuu kwa sababu ya kuwajibika tu na wala si kwamba aliiba pesa ya Richmond.
Lowasa ni tajiri tangu zamani sana, na utajiri wake ni wa kupewa na wazazi wake na mwingine ametafuta mwenyewe na kwa njia halali kabisa. Lowasa ni mchapa kazi na pia ana vision nzuri. Kuna kipindi huko nyuma alikuwa si waziri wa wizara yoyote, na muda huo aliutumia kufanya biashara zake halali kabisa na alilipa kodi kama ipasavyo.
Katika hizi harambee anazoitwa si kwamba anatoa mapesa yote hayo, anachofanya ni kwamba anawaomba marafiki zake wa ndani na nje ya Tanzania wachangie harambee hiyo. Juzi kwenye hiyo harambee lowasa na rafiki zake walitoa Tsh 10M tu ambazo hata mimi na wewe tunaweza kuzitoa bila ya kujiuliza mara mbili na hizo nyinginezo zilichangwa na watu wengine.
Kuitwa kwa Lowasa kwenye hizo harambee pia kunatokana na kipaji cha uhamasishaji alichokuwa nacho. (Gift from GOD).
Kuna watu wengi wanaweza kuitwa lakini ukweli ni kwamba jamaa ana kipaji ya kuongea vizuri na watu na anakubalika vyema.
Kama Lowasa atagombea kiti cha uraisi 2015 kwa dhamana ya CCM ,mimi kama Kidatu, nitakuwa mstari wa mbele kabisa kumpigia kampeni ili ashinde kiti hicho, bila malipo yoyote. Lowasa ni mchapa kazi, yuko tayari kufanya maamuzi magumu hata kama yatawaumiza watu kwa lengo lililo bora kwa Taifa letu, ni mkweli, mwadilifu, hana woga, ana mapenzi ya kweli na nchi yake, anawapenda watanzania wote bila kujali dini, umri, rangi na itikadi za kisiasa. Lowasa hana haya ya kuwaonea haya wazembe na wapuuzi.
Ingekuwa ni hekima kumshukuru kwa haya anayoyafanya kwa jamii badala ya kumshutumu na kumsema vibaya.