Edward Lowassa special thread

TeamLowassa

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2013
Posts
1,495
Reaction score
937
SAFARI ya matumaini kuelekea ikulu imewadia. Tulianza pamoja kwa umoja na tutamaliza pamoja kwa umoja. Tumaini letu ni kwa mgombea mwenye maamuzi.

Njoooni hapa wana LOWASSA tupeane update kwa yanayojili tangu sasa mpaka magogoni. TAREHE 30 mei 2015 Mr Edward Ngoyai lowasa kwa kishindo kikubwa azindua safari ya matumaini jijini arusha. Maelfu wamiminika. Mzee msukuma, kangi lugola na Mzee Kingungwe wasababisha mtikisiko taifa.

Endelea kufahamu kidogo kidogo kuhusu Lowassa

Lowassa alizaliwa tarehe 26 August 1953 mkoani Arusha. Ni waziri wa 8 wa JMT akipokea kijiti kutoka kwa Mh Fredrick Sumaye kutoka 30 Desemba 2005 hadi 7 Februari 2008 na kumuachia Mh Mizengo Pinda ambaye hadi tunavyooandika hapa ndie waziri mkuu wa JMT nae ametangaza nia ya kugombea urais kwa tiketi ya ccm mwaka 2015!


Kabla ya kuwa waziri mkuu, Lowassa alikuwa waziri wa Maji na Maendeleo ya mifugo kuanzia mwaka 2000 hadi 2005 akiwa chini ya rais Mkapa. Wizara hii alimuachia Mh Stephen Wassira baada ya yeye kuteuliwa kuwa waziri mkuu mwaka 2005. Aliingia bungeni kama mbunge wa Monduli kwa tiketi ya CCM mnamo Novemba, 1995.

Lowassa aliwahi kuwa waziri katika ofisi ya waziri mkuu kipindi cha pili cha urais wa Mh Ali Hassan Mwinyi. Mwaka 1995 alianza harakati zake za kuwania urais wa JMT ndani ya CCM. Hakufanikiwa kupata ridhaa ya kupeperusha bendera ya CCM mwaka huo wa 1995 hivyo aliamua kugombea ubunge wa jimbo la monduli na kushinda kwa zaidi ya 90%.

Mnamo mwaka 1997 aliteuliwa kuwa waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais - mazingira na umaskini. Lowassa alidhihirisha uwezo wake wa kiongozi zaidi akiwa waziri wa Maji na Mifugo kuanzia mwaka 2000 hadi 2005.

Mwaka 2005 Lowassa aliacha harakati zake za kuusaka urais badala yake akaanza harakati za kumuunga mkono Mh Jakaya Kiwete kwenye mbio zake za urais. J Kikwete alikuwa ni rafiki yake wa muda mrefu sana, naye Lowassa alikubali kuwa campain manager kwenye mbio zake urais, ambapo Mh Jakaya Kikwete alishinda urais wa JMT kwa zaidi ya 80% chini ya menejimenti ya Lowassa

Elimu ya Edward Lowassa

Lowassa alipata shahada yake ya sanaa na elimu kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na Shahada ya uzamili ya Maendeleo ya jamii kutoka Chuo Kikuu cha Bath kilichopo UK.

Elimu yake ya sekondari alipata kutoka shule ya Ilboru moja ya shule maalum kwa ajili ya wanafunzi wenye vipaji maalum darasani wakati huo; na kumalizia elimu yake ya kidato cha 5 na 6 kutoka shule ya sekondari Milambo mwaka 1977. Lowassa anapozungumzia maendeleo anajua anachozungumzia, habahatishi.

General summary kuhusu utumishi wa Lowassa


  • Mkurugenzi Mtendaji, AICC, 1989 - 1990
  • Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu na makamu wa kwanza wa rais (Sheria na mambo ya bunge), 1990 - 1993
  • Waziri wa ardhi na maendeleo ya makazi, 1993 - 1995
  • Waziri wa nchi, makamu wa rais - mazingira na umaskini, 1997 - 2000
  • Waziri wa maji na mifugo, 2000 - 2005
  • Waziri Mkuu, 30 Desemba, 2005 - 7 Februari 2008

Alianza kuwa mbunge tangu mwaka 1990, na kuteuliwa kuwa waziri kama tulivyoonyesha hapo juu! Hadi sasa bado ni mbunge alietia nia kuwania urais kwa tiketi ya CCM mwaka 2015

Kauli mbiu yake: Safari ya matumaini.

=====
update
=====

TeamLowassa imeishinda TeamJK. JK kashindwa kumuweka mgombea wake kwa namna yoyote ile!

JK kaweka mizengwe, TeamLowassa tukafanya yetu!

Hongereni TeamLowassa mmepambana sana!
 
....bhahahahaaaaa hii inafaa kuitwa mafisadi supporters special junction....
Hoja yenu dhaifu wananchi wameichoka hakuna atakaye kuelewa sikuhizi ukisema LOWASSA ni fisadi. Pia tumeanzisha uzi huu tutiane moyo, tuufaamishe UMMA wa JF na watanzania kwa ujumla kwamba E.L ni nani hasa cha kushangaza unaingia kichwa kichwa na point zako dhaifu
 
Lowasa atawezaje kuwaepuka mafisadi kwenye utawala wake?

Yaani akae mbali na mapacha zake rostam na chenge na hao wemgine
Atawezaje kupiga vita rushwaaa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…