Edward Lowassa: Msilalamike, piga kura kuing'oa CCM

Edward Lowassa: Msilalamike, piga kura kuing'oa CCM

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,345
Gazeti la Raia Mwema, toleo na. 421 la tarehe 2 Septemba, Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema, Edward Lowassa ameandika makala yanye kichwa cha habari, "Msilalamike, piga kura kuing'oa CCM"

Lowassa 1.png Lowassa 22.png

 
Ndefu na bado inaendelea ukurasa mwingine, uwezo wake wa kujenga hoja kwa siku za karibuni unanipa mashaka kama kaandika mwenyewe!
 
Ndefu na bado inaendelea ukurasa mwingine, uwezo wake wa kujenga hoja kwa siku za karibuni unanipa mashaka kama kaandika mwenyewe!

acha dharau kwni wajua fika yeye si mwongeaji sana ni vitendo tu.
 
acha dharau kwni wajua fika yeye si mwongeaji sana ni vitendo tu.

Sijasema hana uwezo wa kutenda mkuu, uwezo wa kujenga hoja. Kama umemsikiliza utaungana nami..
 
sijasema hana uwezo wa kutenda mkuu, uwezo wa kujenga hoja. Kama umemsikiliza utaungana nami..

mkuu lowassa anabusara na hekima sana ndio mtu anafaa kuwa rais. Kumbuka ikulu hakuna viwanja vya mazoezi ya kukimbia wala zege ya kubeba
 
Ndefu na bado inaendelea ukurasa mwingine, uwezo wake wa kujenga hoja kwa siku za karibuni unanipa mashaka kama kaandika mwenyewe!

Hana uwezo wa kushika kitu sembuse kuandika? Mnamuonea sasa mzee watu.
 
Lowassa you need to prove to thinkers that you are not a Fisadi as allegations are continuing encumbering your name and destroying your integrity day after day.

Lowassa, you have failed despite repeated demands to address said allegations but wantonly disregard them as abortive. It is hard if not impossible to trust a person with such behavior of dismiss syndrome.

Please, Lowassa, prove to us that the allegations encumbering you are frivolous by giving us impeccable evidence which are pristine.
 
Mh. lipia ngalau nusu saa uongee laiv haya kwenye TV:

"Taifa letu linayo kansa inayolitafuna. Kansa hii ni rushwa na ufisadi. Bila kuliondoa hili hakuna maendeleo yatakayopatikana wala umaskini hautaondoka. Maraisi wote kuanzia awamu ya pili, tatu na nne wameshughulika sana na tatizo hili lakini yumkini hawakufika mbali. Rais Kikwete alikuwa amejivika silaha zote na kwa nia ya dhati alikusudia kulimaliza hili lakini kinyume chake tatizo limezidi kukua. Sasa tunajiuliza kikwazo ni nini? Niseme tu kwmba kikwazo chetu kikubwa ni kukosekana dira ya Taifa, vipaumbele na maadili ya uongozi. Mambo haya yanapatikana ndani ya Katiba ya wanchi walioikataa baadhi yetu;

Hiyo ndiyo nyenzo ya kipekee kabisa ya kuweza kudhibiti tatizo la rushwa na ufisadi. Katiba madhubuti itasaidia kuwabana viongozi wasichafuke wakiingia madarakani hata kama wangependa kufanya hivyo. Bila katiba madhubuti hata aingie Raisi msafi kiasi gani hakutakuwa na uhakika kwamba yeye mwenyewe hatatumbukia kwenye tatizo lilelile na kuanza kuwaonea aibu marafiki zake. Ilani za vyama kuwa na maadili hazisaidii kitu kwa kuwa haitakuwepo nguvu ya kisheria bila katiba.

Haiwezekani kabisa kabisa kuondoa rushwa na ufisadi kwa Ilani za vyama; kwanza sio kila raia yuko kwenye vyama. Chama kinachoikataa katiba ya wananchi na kuikanusha hadharani hakiwezi kuwa na nyenzo muhimu ya kushughulikia ufisadi hata kingefanya nini. Kitakwama tu hata kama mgombea wao ana nia nzuri kiasi gani na ni msafi kama malaika. Inaanza katiba , zinakuja sheria halafu ndipo vinakuja vyama. Nchi inatawaliwa kwa mujibu wa katiba na sio ilani za vyama. Sisi UKAWA tunasema agenda yetu ni KATIBA YA WANANCHI ambayo itang'oa ufisadi na upotevu wa rasilimali za nchi. Wala huwezi kupeperusha agenda ya ufisadi huku unaiweka kando Katiba ya wananchi inayokupa nguvu hiyo.

KATIBA YA WANANCHI ni agenda kubwa kuliko ufisadi. Huo ndio mwanzo mpya wa taifa letu.; tuangalie mbele na sio kufukua makaburi na kulipa visasi. Watu wanajenga madaraja kwenda mbele sio kurudi nyuma. Kansa imekula taifa zima toka juu hadi chini kwa mwananchi wa kawaida kutokana na umasikini wake; utauwa au kufunga wangapi? Heri tuanze upya, tutafute muafaka wa kitaifa tuijenge nchi yetu upya chini ya KATIBA YA WANANCHI."

Baada ya hapo UKAWA komaeni na katiba ya wananchi mkionyesha ilani yenu inavyooana nayo; hapo mtawafunga wengi midomo. Vinginevyo mtapakwa matope ya kila aina
 
Lowasa hatakiwi kuongea chochote wahusika wa richmond utawala wa juu
 
Lowassa you need to prove to thinkers that you are not a Fisadi as allegations are continuing encumbering your name and destroying your integrity day after day.

Lowassa, you have failed despite repeated demands to address said allegations but wantonly disregard them as abortive. It is hard if not impossible to trust a person with such behavior of dismiss syndrome.

Please, Lowassa, prove to us that the allegations encumbering you are frivolous by giving us impeccable evidence which are pristine.

Je, na Makufuli naye anaweza kukanusha tuhuma za kifisadi za kuratibu uuzaji wa nyumba za serikali kwa bei ya maandazi na nyingine kuwagawia vimada wake?
Mimi ninaweza kusema kila kigogo aliye CCM ni fisadi kwa sababu ni vigumu kuwemo kwenye mfumo fisadi na usiwe fisadi. Tuna kila sababu ya kumpongeza Lowassa kwa kufanya maamuzi magumu ya kuvuka na kuja upande wa mabadiliko ili kuteketeza mfumo fisidi. CHAGUA MABADILIKO, CHAGUA UKAWA, CHAGUA LOWASSA
 
Anaweza kuandika wakuu, khaaa!
 
Binafsi nina machungu makubwa sana kwani CCM wamesababisha ugumu wa maisha kuongezeka maradufu kwa watz.
Chama na watu wake wananuka rushwa na ufisadi. Pia kwa sasa wanajifanya wapo karibu nasi kiasi cha kutuigizia kubeba watoto majukwaani. Mimi naikataa CCM, Pia namkataa Magufuli ambaye kwa sasa wanajaribu kumtenga na CCM, NA MAGUFULI NI MWANA CCM SIMPI KURA YANGU. CCM IMETUTESA VYA KUTOSHA.

Asante
 
Zoezi la mgambo na wamachinga kariakoo limeishia wapi?

sakata la madereva wakasome limeishia wapi?

Wafanyabiashara na mashine za TRA zimeishia wapi?

Bodaboda kuingia mjini limeishia wapi?

Vyote kimya...sasa ngoja uchaguzi upite halafu CCM warudi uone moto itakuwa mara 10 ya vile...

Chagua UKAWA kwa mabadiliko....✌✌
 
Back
Top Bottom