Ebola yatinga Marekani

Ebola yatinga Marekani

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Mtu mmoja amegundulika kuwa na dalili na vimelea vya ebola Jimboni Texas Marekani. Mtu huyo ambaye alisafiri kutoka Liberia hadi Marekani kwa sasa ametengwa kwenye chumba maalum kwa matibabu na pia kudhibiti uwezekano wa maambukizo.



Ebola yatua Marekani


140930214418_ebola_us_atlanta_640x360_ap.jpg

Mgonjwa wa kwanza wa Ebola Marekani

Mgonjwa wa kwanza wa ugonjwa hatari wa virusi vya Ebola amegundulika nchini Marekani, imethibitishwa katika mji wa Dallas, Texas.

Maafisa katika kituo cha afya cha Texas katika hospitali ya Presbyterian wamesema mgonjwa ambaye hakutajwa ametengwa katika hospitali hiyo.

Mgonjwa huyo anasemekana kuwa ni mtu anayeaminika kuambukizwa ugonjwa huo nchini Liberia kabla ya kuonyesha dalili za ugonjwa huo.

Zaidi ya watu 3,000 tayari wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola huko Afrika Magharibi na idadi ndogo ya wafanyakazi wa Marekani wa mashirika ya misaada wamepata nafuu baada ya kupelekwa kutibiwa Marekani.

Jumatatu, maafisa wa kituo cha afya cha Texas katika hospitali ya Presbyterian ya Dallas wamesema mgonjwa ambaye hakutajwa jina alikuwa akichunguzwa virusi vya Ebola na ametengwa katika hospitali hiyo.

Shirika la Afya Duniani, WHO limesema mpaka sasa zaidi ya watu 3,000 wamekufa kutokana na virusi vya Ebola, wengi wa waliokufa ni kutoka Liberia.

Nchini Nigeria, nchi yenye idadi kubwa ya watu barani Afrika kuna wagonjwa 19 waliothibitika kuugua ugonjwa wa Ebola na watu wanane wamekufa tangu mgonjwa wa kwanza kuthibitishwa nchini humo mwezi Julai..

Kuna mgonjwa mmoja aliyethibitika nchini Senegal, lakini hakuna taarifa za kifo mpaka sasa.

Ebola ni ugonjwa hatari wa virusi kuwahi kuzuka duniani.

CHANZO: BBC
 
Mtu mmoja amegundulika kuwa na dalili na vimelea vya ebola Jimboni Texas Marekani. Mtu huyo ambaye alisafiri kutoka Liberia hadi Marekani kwasasa ametengwa kwenye chumba maalum kwa matibabu na pia kudhibiti uwezekano wa maambukizo.

Chanzo: Aljazeera, BBC, CNN na Reuters

sio mbaya kwa vile walivitengeneza wao nadhani hata dawa yake wanayo, atapona tu msijali.
 
Sasa Dawa itapatikana

Asante Mungu kwa kuupeleka huu ugonjwa huko kwao

Cheza na Propaganda za wamarekani, mnahakika kweli anaumwa? Janja tu hiyo ni jasusi mmojawapo kaigiza katiwa kwenye karantini basi ili watu wajitangaze
 
Cheza na Propaganda za wamarekani, mnahakika kweli anaumwa? Janja tu hiyo ni jasusi mmojawapo kaigiza katiwa kwenye karantini basi ili watu wajitangaze

basi ni kheri mkuu, manake atasababisha watoe dawa.
 
"Ebola ni ugonjwa hatari wa virusi kuwahi kuzuka duniani".

Hee.!!!!
Kuliko ukimwi.????
 
Ugonjwa wa ebola ambao umesababisha vifo vya watu 3,000 Magharibi umeripotiwa kutua nchini Marekani katika mji wa Dallas,Texas.
 
japo hujaweka chanzo,acha tu niseme asante yesu kwa kusikiliza maombi yetu sisi maskini wa bara la giza.haleluya.
 
japo hujaweka chanzo acha niseme asante yesu kwa kusikiliza maombi yetu sisi maskini wa bara la giza.haleluya.

kwahiyo uliombea huo ugonjwa ufike Marekani? akili yako inafanana na kile kinyago cha kizungu kilichosurubiwa.
 
kwahiyo uliombea huo ugonjwa ufike Marekani? akili yako inafanana na kile kinyago cha kizungu kilichosurubiwa.

jamaa kasema kweli ispowaumiza wao hawatoi dawa ya kweli wanafanya mtaji Afrika
 
Mliberia aliyekuwa Liberia alirudi US wiki ya tatu ya september anakoishi na huo ugonjwa, mwanzoni alikuwa fit kabisa baada ya siku chache akaanza kuumwa. Akaenda hospital na kutibiwa lakini hakuchunguzwa kama ana Ebola. Siku tatu baadaye akawa mahututi na kupelekwa hospital na ambulance ndipo alipofanyiwa uchunguzi na kukutwa ni muathirika wa huo ugonjwa.

umeingiaje?
 
Back
Top Bottom