Asili ya Jumuia ya Afrika Mashariki ni Nchi tatu tu, Tanzania,Kenya na Uganda huu muongezeko wa hizi Nchi mbili Rwanda na Burundi umefanyika kwa kuwa Nchi hizi tuko nazo karibu sana Kijiografia lakini siyo Kijamii. Nchi yetu Tanzania tumekuwa wahanga wa Wakimbizi kwa miongo kadhaa sasa na tumejitahidi sana kuwavumilia ndugu zetu hawa kwa kipindi hiko chote,lakini ninaamini kuwa kama matatizo ya ukimbizi yangekuwa yanatukuta sisi Watanzania basi hawa jirani zetu wangetunyanyasa sana! tumuombe Mungu na sisi wenyewe Watanzania tuilinde amani yetu kwa jinsi yoyote ile.
Nimesoma matusi na kejeli nyingi zilizotolewa na Rais wa Rwanda kwa Rais wetu wa Tanzania Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kweli yamenisikitisha sana kwanza Kagame hana shukrani pili si mstaarabu na tatu ni Muuaji tena siyo wa kufikirika bali ni muuaji wa dhahiri! Kejeli za Kagame hazina kichwa wala miguu anashindwa kukumbuka nani waliomfikisha hapo alipo kama Rais.Tanzania ina mchango mkubwa sana kwa nafasi yake aliyokuwa nayo amepata mafunzo yake ya awali ya kijeshi pale Monduli ameishi Tanzania kama nyumbani kwake kwa miongo kadhaa kabla ya kujiunga na Museveni wakiwa na Meja Jenerali Fredy Rwejiema,mim naamini kuwa ushauri aliokuwa anaupata Kagame toka kwa Viongozi wa Tanzania wakati huo na mpaka sasa bado haujabadirika ni uleule,tuna msisitiza akae kwa amani na wale wote raia wenzake wa Rwanda,nchi ile si ya kwake pekee bali ni nchi ya wote raia wa Rwanda.
Dharau za Kagame ni matokeo ya tabia zake mbovu alizokuwa nazo toka yuko Tanzania.Mwalimu Nyerere alikuwa anamvumilia tu lakini alishindwa kufahamu kuwa huyu kijana atakuja kuwa msumbufu baadae matokeo yake ndiyo haya sasa sisi Watanzania tunapenda kuishi vizuri na majirani zetu kwa sababu hivi sasa tumeshachoka kuwapokea wakimbizi kila kunapokucha,kama wanashindwa kuishi vizuri nyumbani kwao basi wajue nasi hatutakuwa radhi kuwapokea tena ingawa tumesaini mkataba wa Kimataifa kuhusu Wakimbizi.