Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,407
- 31,392
SAFARI YA DODOMA
Uamuzi wa kuhamia Dodoma ni tukio la 'kushtukiza' lililopokelewa kwa mshawasha na hisia
Ni tukio lilozua taharuki kwa taasisi, watendaji ,wafanyakazi na jamii kwa ujumla
Kadri siku zinavyosonga mbele mengi tuliyojadili yanajitokeza kwa sura tofauti
Hoja kubwa si kuhamia Dodoma, bali utaratibu wa kuhamia Dodoma
Wengi wanadhani ni suala jepesi kuhamisha makao makuu ya nchi
Kuna kuchanganya mambo kati ya kuhamia Dodoma kama makao makuu ya nchi/serikali
Halafu kuna kuhamia Dodoma kama kitovu cha shughuli za nchi ikiwemo biashara
Makao makuu ya nchi na serikali ni sehemu maamuzi mengi ya kisera na utekelezaji hufanywa.
Ndio msingi wa kuhamisha wizara na idara za serikali pamoja na mihimili mingine ya dola
Haina maana ya kuhamisha shughuli za biashara. Dar es Salaam itabaki kuwa kitovu cha biashara kutokana na miundo mbinu yake na hata nafasi yake kijiografia ua idadi ya watu
Tunaanza kuona ugumu wa kuhamia Dodoma kwa namna tofauti
Maswali yanayojitokeza;
Je, maamuzi ya kuhamia Dodoma yalifanyiwa marejeo na kuhakiwa kabla ya kutangazwa?
Je, vyombo husika vilishirikishwa katika kupanga au kuonyesha 'concern' zao
Je, ilikuwa suala la kuhamia Dodoma kwa haraka, au lilikuwa na plan za muda mrefu?
Je, Mji wa Dodoma upo tayari kupokea ugeni utakaoongeza 'strain' huduma za umma?
Kwa umuhimu wa suala hili, uzi utakuwa endelevu kujadili nini kinachoendelea
Kwa kuanzia, tutarejea tuliyowahi kuyajadili nyuma
Tusemezane
Uamuzi wa kuhamia Dodoma ni tukio la 'kushtukiza' lililopokelewa kwa mshawasha na hisia
Ni tukio lilozua taharuki kwa taasisi, watendaji ,wafanyakazi na jamii kwa ujumla
Kadri siku zinavyosonga mbele mengi tuliyojadili yanajitokeza kwa sura tofauti
Hoja kubwa si kuhamia Dodoma, bali utaratibu wa kuhamia Dodoma
Wengi wanadhani ni suala jepesi kuhamisha makao makuu ya nchi
Kuna kuchanganya mambo kati ya kuhamia Dodoma kama makao makuu ya nchi/serikali
Halafu kuna kuhamia Dodoma kama kitovu cha shughuli za nchi ikiwemo biashara
Makao makuu ya nchi na serikali ni sehemu maamuzi mengi ya kisera na utekelezaji hufanywa.
Ndio msingi wa kuhamisha wizara na idara za serikali pamoja na mihimili mingine ya dola
Haina maana ya kuhamisha shughuli za biashara. Dar es Salaam itabaki kuwa kitovu cha biashara kutokana na miundo mbinu yake na hata nafasi yake kijiografia ua idadi ya watu
Tunaanza kuona ugumu wa kuhamia Dodoma kwa namna tofauti
Maswali yanayojitokeza;
Je, maamuzi ya kuhamia Dodoma yalifanyiwa marejeo na kuhakiwa kabla ya kutangazwa?
Je, vyombo husika vilishirikishwa katika kupanga au kuonyesha 'concern' zao
Je, ilikuwa suala la kuhamia Dodoma kwa haraka, au lilikuwa na plan za muda mrefu?
Je, Mji wa Dodoma upo tayari kupokea ugeni utakaoongeza 'strain' huduma za umma?
Kwa umuhimu wa suala hili, uzi utakuwa endelevu kujadili nini kinachoendelea
Kwa kuanzia, tutarejea tuliyowahi kuyajadili nyuma
Tusemezane