1. Ni kweli zaidi ya 90% ya mijadala ya Watanzania ni Simba na Yanga, sijui tulikosea wapi? Ni vigumu kujadili mambo ya kitaifa au ya kimataifa ambayo yanatuathiri moja kwa moja. Tunaathirika.
2. Kuhusu ukatili wa Israel wakati mwingine mimi nafikiri tatizo ni waarabu wenyewe ambao wameshindwa kuungana dhidi ya Israel. Wakati makaburu walipokuwa wanawatesa waafrika kule SA, Waafrika ya akina Nyerere, Kaunda, Mugabe etc waliungana licha ya kuwa hawakuwa na nguvu za kijeshi mpaka makaburu wakaangushwa. Ni nini kinachowashinda Waarabu. Unaambiwa Saudia au misri inapatana na Israel kuliko inavyopatana na Syria.
Kamili , hoja zako nitaziunga na maswali ya bandiko#60 kwasababu zinawiana sana
1. Mijadala Watanzania imejikita kwa yasiyogusa Taifa au kimatifa. Watanzania wanaungalia mgogoro wa Israel-Palestine kwa jicho la udini. Wengi wanadhani tatizo limeanza October 7,2023, humeza habari kutoka vyanzo vya aina moja. Kizazi cha vijana kimekosa utamaduni wa kujisomea , kujifunza, kudadidisi na kuyatazama mambo kwa upana.
Upeo wa kuielewa dunia ni jambo muhimu katika ushindani wa duni. Huwezi kutenga mgogoro wa Mid East na maisha au Kazi au Biashara popote alipo mwanadamu.
Jaribu kuuliza Watanzania uliza swali hili '' kwanini dollar imeadimika'' majibu utakayopata yatakushangaza.
2. Kuna swali ; Kwanini Israel inakingiwa kifua na Mataifa ya Magharibi?
Israel iliundwa na nchi za Magharibi 1948, saa 11 baada ya kujitangaza Utaifa , Rais Truman wa US aliitambua na kudharau kamati ya Uingereza-Marekani iliyopendekeza nchi mbili 'two sates' solution''
Pili, Wayahudi wanamiliki uchumi wa nchi za Magharibi, kubwa zaidi wanamiliki vyombo vya habari.
Mafanikio ya kibiashara na umiliki wa vyombo vya habari unawapa nguvu sana za kuamua siasa za mataifa.
Katika mgogoro unaoendelea CNN , Fox na MSNBC vimekuwa vyombo vya propaganda vya Israel. Habari zao ni biased hazina weledi wa kiuandishi na zimelenga kuipa Israel eneo la propaganda bila kusikiliza Wapalestina
Marekani kuna taasisi ya Waisrael inayoitwa AIPAC (America-Israel Public Affairs committee.
Ushawishi wa Taasisi hii kifedha na njia za habari ni sehemu muhimu sana ya Uchaguzi wa Marekani.
Wasrael wapo katika serikali za magharibi na wanafanya maamuzi mengi.
Waziri wa mambo ya nje US wa sasa ni Muisrael na wengi tu katika idara na taasisi mbali mbali muhimu
Wakati wa Rais Trump, waandamanaji wa kizungu (white supremacist) walibeba mishumaa na mabango yasemayo ( Jews will not rule us) yakiimanisha Wayahudi hawatutawala. Hawa niWaamerika Wazungu wanaosema hivyo.
3. Kwanini Iran inaunga mkono vikundi vinavyopingana na Israel?
Vikwazo vya nchi za Magharibi kwa Iran ni kutokana na Iran kuendeleza sayansi ya nuclear inayoweza kutoa Bomu.
Israel ina wasi wasi na Iran kwasababu ya nguvu za kitaaluma katika viwanda na Sayansi.
Tumewahi kujadili hapa kwamba Iran ikiwa na SHIA ina Raia walioelimika sana mashariki ya kati
Iran ina rasilimali za mafuta na inazitumia kwa kuelimisha Raia wake takribani Milioni 86 mara 12 ya idadi ya Israel.
Iran ina mpaka na Israel na nchi rafiki kama Syria na Lebanon kupitia makundi ya SHIA.
Iran ni tishio kwasababu haitegemei teknolojia ya Magharibi kujiendeleza na Israel inapata tabu kuipeleleza.
Kuuwa kwa kingozi wa Nuclear Bw Mohsen na Kamanda wa Jeshi Qasem ilitekekelezwa na Israel kwa juificha nyuma ya Marekani. Israel inatambua vita na Iran ni mchezo tofauti kabisa na huu wa Hamas, na huitumia Marekani
Iran imeshapata mashambulizi ya Israel kwa mauaji ya viongozi wake, inajibu mapigo kuipitia vikundi mbali mbali kama Hezebollah, Huti n.k. Kwavile 'adui yao ni mmoja' Iran na Hamas (SUNNI) wanashirikiana
Hamas kimsingi walitakiwa kuungwa mkono na Saudi Arabia, kwa kutoswa wameamua kushirikiana na Iran
Hii haina maana Hamas na Hebollah wanaiva, la hasha, wanaiva dhidi ya adui wa pamoja ''common enemy'
4. Waarabu wameitosa Palestina ? Kwanini Saud Arabia inataka 'normalization''
Ni kweli Palestina imetoswa na nchi za Kiarabu kwasababu moja, hofu ya nani mbeba Mashariki ya kati.
Saudi Arabia ina Sunni wengi kama tulivyowahi kusema. Iran ina Shia wengi. Pakistan , Afganistan, Qatar, UAE, Kuwait, Yemen , Lebanon , Syria , '' Misri , Morocco, Tunisia , Algeria' zenye Waarabu zimegawanyika kwa mrengo wa Shia na Sunni. Kuna vita ya 'dominance' ya mashariki ya kati , Saudia ikipoteza ushawishi
Tutaendelea tulipoishia '' kupoteza ushawishi''