Dr. Tulia Ackson, nani amekutuma? Unataka nini? Kwanini?

Dr. Tulia Ackson, nani amekutuma? Unataka nini? Kwanini?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Naweza kuamini kuwa sasa umeshaanza kunogewa na vyeo. Ulianza kuwa Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Ukafuata kuwa kiongozi wa Kamati ya Bunge Maalum la Katiba. Kama hiyo haitoshi, ukateuliwa kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Sasa unataka Uspika wa Bunge.

Ukiwa ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, hukupaswa kujitokeza kisiasa na kugombea Uspika wa Bunge. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali si mtu mdogo. Ndiye Kaimu Mwanasheria Mkuu wa Serikali pale ambapo Bunge hufanyika kwakuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali huwa Bungeni Dodoma. Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ni mtu wa kitaifa zaidi.

Kujianikaanika kama kada wa CCM si jambo jema wala vutizi. Kutakuwa na kitu na watu wanaosababisha. Nani kakutuma? Unataka nini hasa? Kwanini? Dr. Tulia, umejianika kama kada. Watumishi wa Ofisi yako na wananchi kwa ujumla watakuonaje ikiwa utaendelea kuwa Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali?

Ili kulinda heshima yako, jiuzulu Unaibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali na urejee Shule Kuu ya Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ukahadhiri pale ambapo Uspika utagoma kupatikana. Ujiuzulu haraka!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Dodoma)
 
Ukiwa CCM ni vigumu sana kuficha upumbavu wako...
 
Ndo wasomi/viongozi wetu hao.Tanzania si nchi ya kutegemea kwamba mtu fulani kwa sababu ana wadhifa fulani hatafanya kitu fulani kwa sababu ni ujinga kufanya hiki kitu.Tanzania watu wachache wanaweza kufanya vitu vizuri,lakini watu wengi wanaweza kufanya ujinga.
 
Kwa kulinda heshima yake ajiuzulu, huwezi kua Deputy AG ukawa kada wa chama.hapo kachemka
 
Afu mimi hata hanivutii kuwa deputy AG.
Sasa na hii ya kuongeza sifa za kuwa gamba ndo kazid kunichefua zaidi.
Mh. Magufuli tafadhari shughulika nae kama yule CEO wa muhimbili.
 
kati ya watu ninoawana makada wa ccm walio wajibga ni huyu dr akson, kuna ka mama kana vinywere vya hovyo semakafu, dr bana misuli na michael hawa ni wasomi wasiojitambua. ukiona mambo yao unakata tamaa ata ya kusoma. mtu anasoma hajitambui ni full kujipendekeza je elimu yake imemsaidia?
 
BAWACHA wajinga sana nyie unaandika kama zuzu huna hata kifungu kimoja cha sheria ambacho kimevunjwa wenzako wanafanya kwa mujibu wa sheria na katiba kama kavunja sheria sema.
 
Kifungu gani cha sheria au kanuni kinamkataza kuwania hiyo nafasi?
Kaka kanuni na sheria ziko hivi, kwa cheo chake alichonacho cha kiserikali (naibu Mwanasheria Mkuu) hauruhusiwi kujihusisha na mambo ya kisisasa au kuwa mwanachama wa chama chochote cha kisiasa, sasa anapoenda kuchukua fomu za kugombea Uspika kwa mgongo wa CCM hili hali bado ajatoka serikalini hilo ni kosa
 
Chama dola kinadhibitoshwa na Hali ya kuwa KILA Afisa wa ngazi ZA juu serikalini hata ambao kwa kawaida hawatakiwi kwenye siasa ...wakichukua likizo Ili wagombeee wote wanagombea kwa tiketi ya ccm ...HII inamaanisha kuwa ccm Sio Chama Bali Ni Dola .
 
Huyu Dada ni kichwa sana- hili halina ubishi. Tangu wakati wa Bunge Maalum la Katiba alionekana kuwa ni Kada wa CCM.
 
Kaka kanuni na sheria ziko hivi, kwa cheo chake alichonacho cha kiserikali (naibu Mwanasheria Mkuu) hauruhusiwi kujihusisha na mambo ya kisisasa au kuwa mwanachama wa chama chochote cha kisiasa, sasa anapoenda kuchukua fomu za kugombea Uspika kwa mgongo wa CCM hili hali bado ajatoka serikalini hilo ni kosa

haya mambo yapo kila mahali mfano chadema kuteua viti maalum ilhali bado ni ccm ajabu kabisa.
 
Kaka kanuni na sheria ziko hivi, kwa cheo chake alichonacho cha kiserikali (naibu Mwanasheria Mkuu) hauruhusiwi kujihusisha na mambo ya kisisasa au kuwa mwanachama wa chama chochote cha kisiasa, sasa anapoenda kuchukua fomu za kugombea Uspika kwa mgongo wa CCM hili hali bado ajatoka serikalini hilo ni kosa

Atakuwa anapendekeza sheria kandamizi dhidi ya upinzani,pia tutarajie wapinzani kubambikiwa kesi za jinai,tumeshaanza kuona tayari, inawezekana kameanza kutafunwa
 
Huyu Dada ni kichwa sana- hili halina ubishi. Tangu wakati wa Bunge Maalum la Katiba alionekana kuwa ni Kada wa CCM.
Wapinzani watabambikiwa kesi mpaka wakome,pia atapendekeza miswada inayokandamiza kambi ya upinzani ili ailinde ccm
 
Back
Top Bottom