Dr.Slaa ndani ya Mwanza.

cjilo

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2011
Posts
884
Reaction score
447
Wanafunzi wa chuo kikuu cha mt Augustine na wakazi wa Nyegezi hivi punde wanamsubiria Mh Dr Slaa kutema cheche ndani ya viwanja vya s/m Nyamalango. Naona nyimbo mbalimbali za Chama zinapigwa, wananchi wanaimba kwa pamoja. Viongozi mbalimbali wa chama mkoa wanahutubia. Nitawapa updates.
 
Tunazisubiri.🙂

 
Sasa unataka tukusaidie nini?au unataka tumchangie nauri kama arumeru mnavyo fanya,kuwa wazi tuwasaidie
 
Kirumba lini mkuu...?Huko ndiyo pa muhimu kwa sasa.
 
Vipi tena umepotelea wapi mkuu? Updates, wengine tuko mbali na tukio, na huko ndiyo nyumbani! Nyegezi Academic Hill
 
Anaambatana na wabunge wa Chadema mkoa wa Mwanza, mh Wenje na Highless na viongozi wengine wa kitaifa. Bado tunawasubiri, watu ni wengi bado wanaendelea kusubiria timu nzima ya viongozi wa CHADEMA. Zinapigwa zile nyimbo za maombolezo ya wananchi waliouwa na polisi mkoani Arusha. Naona wameweka viti uwanja mzima, jua kali sana ila bado wanafunzi wa SAUT na wananchi ktk viunga vyake bado wana hamasa kubwa kumwona Dr Slaa.
 
Tunaomba utuwekee na picha mkuu! tunatambua kazi na juhudi zako mkuu!!
 
Ratiba inaonesha hivi 5:00 kuwasili nyamalango, 5:10-5:30 ufunguzi wa kongamano na utambulisho, 5:45-6:00 uwasilishaji mada na Fred mpendazoe na prof Mlambiti. 6:30 dr Slaa, 7:00-8:00 maoni na maswali kwa Dr Slaa. Naona msafara wa magari na pipikipiki (bodaboda) unaingia viwanjani wanamsindikiza Slaa. Tayari kaishafika uwanjani.
 
mtukwao12 tafadhali heshimu uhuru wa members wengine, sasa kuanza kupost vitu tofauti ina maana gani.
 
Wakuu tayari makamanda ameishaingia katika viwanja vya Nyamalango. Sasa ni utambulisho, katibu wa mkoa wa chama Mushumbushi anawatambulisha jukwaa kuu. Wenje, Highless, mbunge wa ukerewe, mzee Sylivester mwenyekiti wa baraza la wadhamini, mayor na naibu wake wa jiji la Mwanza, madiwani na viongozi wa SAUT. Sasa prof Mlambiti anamwaga cheche...anawaasa vijana kutolala, kupigania haki zao. Anasema ameingia CHADEMA kwasababu wanauongozi thabiti wasio na woga, anaongeza kwamba umasikini umezidi umekithiri tangu JK aingie madarakani. Thamani ya shs imeshuka....
 
don-oba endelea mkuu kutuhabarisha kinachoendelea.
 
tunasubiri upadates mkuu, usitishwe na wanaopotosha mada, nadhani leo ndo wamepewa fungu lao na nepi
Naona jamaa ameshakula haki yake aliyokuwa anaitafuta.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…