Tatizo ufahamu wenu ni mdogo juu ya mpango mzima wa maoni ya Katiba. Kuna awamu tofautitofauti katika uundwaji wa katiba; hatua yakwanza ilikuwa ni ukusanyaji wa maoni toka kwa wananchi kupitia tume, pili mabaraza ya katiba, kisha taasisi mbalimbali na vyama vya siasa. Sasa CHADEMA kama chama cha siasa kimeanza rasmi jukumu lake, na hii ni kisheria wana haki hiyo. Na hata ccm nao watafanya ama wameanza kufanya shughuli hiyo hiyo. Ndivyo itakavyokuwa!! Naona mmetanguliza chuki binafsi kwenye jambo hili!