Dr Slaa jenga chama

Kwanza hizo ofisi wanazo? Kipindi cha uchaguzi mwaka jana nilibahatika kuwa mkoani Kilimanjaro, nikabahatika kutembelea kata ya Korongoni kujionea mchakato wa uchaguzi, kwa macho yangu nilimuona bwana Ndesamburo akifungua ofisi ya tawi ya CDM katika mtaa wa Wireless kwenye duka la mtu nilishangaa sana, dukani kwa mtu unafungua ofisi ya chama kikubwa kama CDM?

Taarifa nilizopata ni kwamba duka hilo limefungwa kwa maana mtaji umekwisha je na ofisi bado iko? Na nini mpango uliopo? Kimsingi CDM wanapaswa kujijenga kwa sasa na si kujibizana na CCM, huwezi ku-assume kwamba utachukua nchi ili hali huna ofisi za kutosha!

CDM itumie rasilimali watu iliyo nayo kuchangia gharama za ujenzi wa ofisi ama kukodisha majengo mbalimbali, hamuwezi kujifanya mnaipenda CDM wakati mnakuwa wagumu kuichangia! You must change


CCM wana ofisi nyingi zilizojengwa na wananchi. Mali nyingi za CCM ni na umma ila CCM wameng'ang'ania.

Back to the point, Chadema hawatakiwi kufungua ofisi nyingi kama CCM ili wakubalike. Kama walivyokwisha sema watu wengi tu hapa JF, huo mtindo wa ofisi za matawi, nyumba kumi ni mfumo wa kijamaa ambao sasa umepitwa na wakati. Chadema inabidi waje na strategy mpya ambayo itawahakikishia support toka kwa wananchi. CCM wenyewe pamoja na kudai wana wanachama 5 million bado inabidi waalipe watu kuattend mikutano, kuwasafirisha, kuwalisha na bado inabidi wapate ushindi wa mezani kutoka NEC.
 
Mimi nikiwa Mjamaa wa dhati nadhani mfumo ambao CCM waliutumia wa kuwa na matawi kila mahala pamoja na wajumbe wa nyumba kumikumi (bado wapo kisheria (?) ukienda polisi unaulizwa mjumbe wa nyumba kumi) ni mfumo ambao ni mzuri. Si vibaya CHADEMA wakaiga mfumo huu. Maandamano sawa, lakini baada ya maandamano na hotuba kama watu wamekata shauri watapata wapi kadi ikiwa Dr. Slaa na wenzake wanazo kwenye ma briefcase yao? Ni vyema wakaawambia watu kama mmekata shauri basi nendeni pale kwenye ofisi yenye bendera au kwa mjumbe (anaweza kuwa wa nyumba hamsini) mkachukue kadi. Mapato yatakuwepo, ufurukutwa utakuwepo na chama kitaimarika. Maandamano na hituba mwanana bila ofisi zilizotamalaki mahala mahala ni ukengeufu mtupu!!
 
Bado wachangiaji hamjaniridhisha kiu yangu kuhusu utaratibu gani muafaka utumike ili watu wanaotaka kuwa wananchama wa CDM wataweze kupata kadi kama wengi wetu tunadhani kuwa na ofisi is a bit expensive. Can IT experts suggest an online registration facility? Vipi kuhusu CDM kuwa media firm yake ikihussha Radio, TV, magazeti na IT forums ambapo wapenzi na wanachama tutaweza kununua hisa pia?
 
Kwanza hizo ofisi wanazo? Kipindi cha uchaguzi mwaka jana nilibahatika kuwa mkoani Kilimanjaro, nikabahatika kutembelea kata ya Korongoni kujionea mchakato wa uchaguzi, kwa macho yangu nilimuona bwana Ndesamburo akifungua ofisi ya tawi ya CDM katika mtaa wa Wireless kwenye duka la mtu nilishangaa sana, dukani kwa mtu unafungua ofisi ya chama kikubwa kama CDM?

Taarifa nilizopata ni kwamba duka hilo limefungwa kwa maana mtaji umekwisha je na ofisi bado iko? Na nini mpango uliopo? Kimsingi CDM wanapaswa kujijenga kwa sasa na si kujibizana na CCM, huwezi ku-assume kwamba utachukua nchi ili hali huna ofisi za kutosha!

CDM itumie rasilimali watu iliyo nayo kuchangia gharama za ujenzi wa ofisi ama kukodisha majengo mbalimbali, hamuwezi kujifanya mnaipenda CDM wakati mnakuwa wagumu kuichangia! You must change

Walau leo umeongea kwa Busara, ila CCM nayo ilifaidi nguvu zetu, maana wanchi tulichangishwa sana kujenga majengo mengi ya Chama hicho ambayo kimsingi ni mali ya Serikali.
 
Bado wachangiaji hamjaniridhisha kiu yangu kuhusu utaratibu gani muafaka utumike ili watu wanaotaka kuwa wananchama wa CDM wataweze kupata kadi kama wengi wetu tunadhani kuwa na ofisi is a bit expensive. Can IT experts suggest an online registration facility? Vipi kuhusu CDM kuwa media firm yake ikihussha Radio, TV, magazeti na IT forums ambapo wapenzi na wanachama tutaweza kununua hisa pia?

with online registration naona ni mapema mno,wafuasi wengi wa cdm ni watanzania waliochoka na maisha na wengi wao ni masikini wakutupwa ambao kuafford gharama za internet ni kazi sana labda watumie teknolojia ya simu lakini hii unaweza kuwa na wafuasi wengi lakini monitoring itakuwaje? tutake tusitake lazima kuwe na ofisi,wanachama wa eneo lile wakutane wapange mikakati mbambali ya kuimarisha chama,narudia tena siasa siku hizi ni proffesional activity bila kuindesha kisayansi cdm itakwama,huwezi kujivunia umati wa watu ambao wengine hawajui sera za chama kimsingi mabadiriko lazima yaanzie kwenye grass root
 
with online registration naona ni mapema mno,wafuasi wengi wa cdm ni watanzania waliochoka na maisha na wengi wao ni masikini wakutupwa ambao kuafford gharama za internet ni kazi sana labda watumie teknolojia ya simu lakini hii unaweza kuwa na wafuasi wengi lakini monitoring itakuwaje? tutake tusitake lazima kuwe na ofisi,wanachama wa eneo lile wakutane wapange mikakati mbambali ya kuimarisha chama,narudia tena siasa siku hizi ni proffesional activity bila kuindesha kisayansi cdm itakwama,huwezi kujivunia umati wa watu ambao wengine hawajui sera za chama kimsingi mabadiriko lazima yaanzie kwenye grass root

Umenena kwa lugha, bila ofisi na watu kuketi na kupeana mikakati CDM inweza ikawa historia kwani hawa CCM ni wajanja sana. CDM inabidi iingie mioyoni mwa watu na wawe wanaiona kila siku kwa bendera na ofisi siyo kusubiri tu operation sangara toka makao makuu. Operation sangara ifanywe na hata wenyeviti wa mikoa, wilaya na vitongoji.
 
Mimi nafikiri Mada hii ni Muhimu sana kwa wanachadema, Mawazo yangu;

1. Kila operation Sangara inapomalizika ni jukumu la wakazi wa eneo husika kuanzisha tawi kama wameshawishika na kukubaliana na sera, wao watachagua viongozi wa tawi na kuwasilisha majina makao makuu, na ndipo viongozi wa wakuu wa chama watakwenda kuzindua tawi rasmi na kugawa kadi kwa wanachama wapya, na pia kuacha kadi kwa ajili ya kugawia wanachama watakao jiunga baadae, viongozi watabuni miradi ya kuendesha office wakisaidiwa na makao makuu.

2. sisi vijana ambao wengi wetu asili yetu ni mikoani tuanzishe utaratibu wa makusudi kutembelea babu zetu na ukifika huko kama wewe ni wanachama wa Chadema na unao uwezo wa kujenga nyumba, jenga huko na utenge chumba kimoja kwa shughuli za chama, wasiliana na makao makuu utambulike na uanze kufanya shughuli za chama kwa kusimika viongozi. ukiweza kwenda hata mara mbili kwa mwaka inatosha kuhamasisha na utapata watakaokuunga mkono,

ni mtizamo wangu tu.
 
Mimi nafikiri Mada hii ni Muhimu sana kwa wanachadema, Mawazo yangu;

1. Kila operation Sangara inapomalizika ni jukumu la wakazi wa eneo husika kuanzisha tawi kama wameshawishika na kukubaliana na sera, wao watachagua viongozi wa tawi na kuwasilisha majina makao makuu, na ndipo viongozi wa wakuu wa chama watakwenda kuzindua tawi rasmi na kugawa kadi kwa wanachama wapya, na pia kuacha kadi kwa ajili ya kugawia wanachama watakao jiunga baadae, viongozi watabuni miradi ya kuendesha office wakisaidiwa na makao makuu.

2. sisi vijana ambao wengi wetu asili yetu ni mikoani tuanzishe utaratibu wa makusudi kutembelea babu zetu na ukifika huko kama wewe ni wanachama wa Chadema na unao uwezo wa kujenga nyumba, jenga huko na utenge chumba kimoja kwa shughuli za chama, wasiliana na makao makuu utambulike na uanze kufanya shughuli za chama kwa kusimika viongozi. ukiweza kwenda hata mara mbili kwa mwaka inatosha kuhamasisha na utapata watakaokuunga mkono,

ni mtizamo wangu tu.

Umetoa mawazo mazuri sana. Madhumuni ya wananchi kushiriki siasa k.m kujiandikisha kuwa wa[iga kura. kampeni, kupiga kura na hata kugombea vyote madhumuni yake ni kutengeneza uongozi wa taifa kuanzia ngazi ya chini kwa lengo ya kutumia raslimali zilizopo kuyaletea maeno yatu maendeleo na taifa kwa ujumla. Njia ingine nzuri ya kushawishi wananchi kuipenda na kuendelea kujiunga na CDM ni sisi wanachama na wapenzi wa CDM kujihusisha na kuondoa kero mbali mbali katik ameneo yetu hata kama sisi sio viongozi. Hii itasadia sana kukubalika kwa wananchi wakati wa uchaguzi.
 
Back
Top Bottom