Dr. Slaa is officially jobless

ukweli ni kwamba, kwa move ambayo chadema wameichukua, wana uwezekano mkubwa wa kutwaa dola, lakini hawatakuwa na maisha marefu katika utawala wao maana tayari wameshakubali kujijenga kwenye msingi mbovu. Tusishangae endapo chadema itaongoza kwa miaka mitano tu na ikawa ndio mwisho wake wa kushika dola. Kwa msingi waliojiwekea, itahitaji muujiza wao kuweza kushinda muhula wa pili. Kuna hatari kubwa sana ya wao kuwa na mpasuko dhariri watakapokuwa madarakani.
 
Chukua account namba yake ya benki... peleka kwa mwajiri wako ili mshahara wako uende kwake moja kwa moja...!!
Imekaa vipi hilo wazo...??
 

Unatuchanganyia habari, nani kasema Dr katoswa. kilichopo tuliambiwa kwamba anapumzika, taratibu za kiofisi zipo na kama kaonewa achukue hatua. Mwenyekiti wa tume ya katiba aliwahi kusema kwamba yeye binafsi alikuwa muumini wa sirikali moja na wala si serikali tatu kura ikapigwa na wale wa tatu wakashinda ikawalazimu wale wa mbili na wa moja wkubaliane na wenzao waliokuwa wengi. Inawezekana walikuwa wengi wenye wazo kama lake lakini sasa amebaki peke yake, busara imuelekeze kama abaki peke yake, awafuate wenzake au ahame chama. Siku zote ukibaki peke yako uanapungukiwa na nguvu. Sasa hivi kampeni karibu zitaanza. UKAWA wakifanikiwa kwenye kampeni watazidi kumsahau hata kabla ya uchaguzi kufanyika. Ajipe moyo na afanye maamuzi magumu kama mwenzake profesa na awe tayari kwa matokeo kama yatakuwa chanya au hasi.
 
Zemarcopolo ishapitwa na wakati zipo YUTONG zinapiga mzigo balaa umetuma post ya kishakinaku sana kajipange kwanza slaa ataendelea kuwa na heshima yake ila wewe ni mwasibu wa chadema?
 
Kwa sheria ya kazi ya sasa Tanzania Slaa hawezi kuwa hana "pension" kama ulivyodai kwenye uzi wako huu. Na hii ni dalili kwamba habari yako ni propaganda za kisiasa.
 

Hofu yako umasikini wako wa fikra.kama huko ccm ukizeeka utakuwa mchawi na kama huko ukawa angalau utakuwa mtabiri feki .mtoto mdogo unawaza kushindwa kabla ujaanza ni tatizo kubwa sana unalo.Hakika ni lazima ccm out 2015.
 
Zemarcopolo ishapitwa na wakati zipo YUTONG zinapiga mzigo balaa umetuma post ya kishakinaku sana kajipange kwanza slaa ataendelea kuwa na heshima yake ila wewe ni mwasibu wa chadema?

Siasa ni mchezo unaobadirika, unachokiamini leo kinaweza kisiwe hivyo kesho, wanasiasa kwa kawaida yao huenda na mvumo wa upepo. Tulikuwa na Azimio la Arusha hapa na kuna watu walikuwa wanaliamini kweli kweli, nani aliacha kazi serikalini kwa sababu ya kuvunjwa kwa Azimio, wameendelea kuwemo na wanakula nchi kama kawaida. Kulikuwa na Wakomnisti wa Urusi na China (Wakomnisti kweli kweli) leo wako wapi wote wanatinga suti kama watu wa magharibi. Wakatoliki wa zamani (Dr anajua vizuri zaidi) ilikuwa ni dhambi kula nyama siku ya Ijumaa leo hii ni Ijumaa moja tu hawali nyama katika mwaka, hakuna aliyekuwa anaruhusiwa kushika kwa mkono hostia isipokuwa kama yeye ni Padre leo hii hadi wanawake wanashika, wanawake walikuwa hawaruhusiwi kuingia katika eneo la madhabahu, patakatifu pa patakatifu (meza takatifu) leo hii wanakaribia na kuishika. Dr aachane kuwa na msimamo mkali kiasi hicho itamghalimu yeye peke yake na familia yake watu wanasonga mbele.
 
ni heshima kwa mungu kumzomea fisadi kama lowassa by Godbless lemah
Hawa wote waliomshirikisha Mungu wanatakiwa watubu! Kwa hiyo leo Lema badala ya kuzomea anamshangilia mtu yule yule ambaye hajabadilika! Siasa kweli zimejaa unafiki.
 
Marco polo.jina la kampuni nzuri ya machine za kufua upepo duniani.vipi ulikuwa wapi muda sasa.duhh karibu tena .Ila njoo ukijua atuitaji upepo wa mashine.tayari tuna kimbunga kimeleta na mafuriko .ukawa na Lowasa
 

Kweli siasa imejaa unafiki. Huyu si ndiye mlikuwa mkimuita Rais wa Mioyo ya Watanzania, leo mmemuacha peke yake tena tayari katoka mioyoni mwenu!?
 
Zemarcopolo ishapitwa na wakati zipo YUTONG zinapiga mzigo balaa umetuma post ya kishakinaku sana kajipange kwanza slaa ataendelea kuwa na heshima yake ila wewe ni mwasibu wa chadema?


kweli wewe nyeti za kuku..........
 
Taarifa hii ya mwaka 2013 hatimaye imetimia...

Tofauti ni kwamba zzk alifukunzwa uwanachama wake ndani ya cdm, Lakini Dr hajafanywa hivyo... Kwa hiyo nahisi hapo issue inayojitokeze ni kama zzk ametoka basi na Dr nae amefuata lkn kwa njia tofauti.
 
Yuko wapi huyo Slaa nimpatie kitu kidogo. Malipo hapa hapa duniani waliompindua Dr Slaa laana itawarudia. Mzee Slaa poa watadondoka na dhuruma zao
 
Kundi gani bora: shetani mmoja kwenye kundi la watakatifu and mtakatifu mmoja kwenye kundi la mashetani
 
Chadema wana Taarifa kuwa Membe kupitia madalali wake wa Sinda Nape na makonda wamempatia dollar million 2.5 ingawa Nape na mwenzake walipiga panga hilyo 5 wakafikisha 2 tu ambazo ni sawa na tshs bilion Nne, bilion moja wamegawana wakanunua Nyumba Dubai kwa Ajili ya kukimbilia pindi ukawa wakiingia ikulu. Dr slaa hapo alipo ana Dola million 2 cash ndiyo maana wameacha kumlipa kitu pia kuna Deni kubwa anadaiwa na chama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…