Dr Slaa ajibu upotoshaji wa Mwandishi Mayage dhidi ya CHADEMA

Straatkasyambe;

Mkuu kama ulikuwa unafuatilia Statement za Dr. Slaa mojawapo ya mkakati aliokuwa nao kupitia CDM ilikuwa ni ku-overhaul system. Hili ni neno pana kidogo, lakini ukifuatilia zaidi juu ya sera za CDM utapata majibu ya maswari uliyoyarise isipokuwa la ushoga sidhani kama lipo maana hii ni la juzi la Cameroon lakini kwa kuwa vission ya CDM ni kujenga uchumi imara wa kujitegemea automatically this cancelled out! Are you there?.

Kuna mambo mengi ambayo ukiwa huna dola utayaangalia sawa na mcheza mpira reserve na hili ndilo linalotokea hapa. Ukisoma mfumo tulionao utaona hamna ambacho CDM kwa sasa wanaweza kufanya wakiwa nje ya serikali tofauti na kuikosoa. Kwa mfano CDM wanachukia ufisadi lakini lakini hawawezi kutunga sheria ya kudhibiti mafisadi-serikali ndiyo inatunga sheria na kuileta bungeni kama muswada ambapo wabunge huchangia kuhusu huo mswada ambao baadaye huwa sheria.

Kama CDM wangelikuwa na nafasi kama hiyo tungelitegemea muswada strict kuhusu ufisadi na si miswada ya ku accelerate ufisadi. Kumbuka mchango wa Mnyika kwenye mswada wa marekebisho ya sheria ya PPRA, he made about forty (40) ammendments kwenye mswada, kwa mantiki hiyo wakiwa wao ndo wanaotunga miswada, concern zako nyindi naona zitakuwa addressed.
 

Wewe kijana wa kukuletea Maisha bora ni Dr Slaa kweli? Kwani yeye anaongoza serikali?
 

Kuna namna fulani hivi ya tabia ambapo asiyejiamini na mtu aliye nyanyaswa kwa muda mrefu ili asikilizwe inabidi amsifie yule anayedhani ni boss (Mungu mtu)mtegemezi wake u name it, ili through huyo sauti yake isikike naye apate kukumbukwa kama mtu muhimu katika kundi la watumwa wa huyo mkuu/boss/Mungu mtu. Hii ndiyo tabia ya watanzania ambao baada ya kuwa opressed kwa muda mrefu hawajiamini tena kama wana weza kusimama na kutoa maoni yao yaliyo huru bado wakaendelea kubakia jinsi walivyo ama hata kuinua hali yao jua ya hapo walipo sasa. Wanasema wasicho amini na wanatenda kwa tahadhari sana ili wasije muudhi yule ambaye wanaamini anauwezo wa kuwafanya anachotaka na bado wao wasiweze kumfanya lolote.

Na moja kati ya hao ni huyo ambaye ume-respond post yake.
 
Kaka Rejao hii kazi ya kuhamasishana kufanya kazi kwa bidii tumeshaanza polepole si unajua tena walikuwa na mgomo baridi wa kutoingia drsn, kutia mboko wanafunz kisa serkali haijawalipa madai yao. Mwisho wa siku tukaona tunawaumiza watoto wasio na hatia na tunaongeza idadi ya mafisadi si unajua tena mtoto akikulia mazingira ya kifisadi tarajia kuwa fisadi nae. Japo wenzetu wa sec bado wana mahasira hawajalipokea sana hili la kufanya kazi kwa bidii hasa shule za kata. Kuhusu masaa 24 kuwa inter siunajua tena tuko likizo hivyo tutabanana hapahapa jf.
 

Issue yenu ime ''backfire'' nendeni mkajipange upya...
 
Dr wa ukweli sasa kamwaga darasa, Mayange acha uandishi wa kishabiki kwa wale wanasiasa wa KUSADIKIKA uwapendao wewe akilini mwako peke yako kwa maslahi binafsi.
 
kwani mayage mayage ni nani?? Ata atushauri tuwe na utitili wa vyama?? Hizi ni njaa tu zinawasumbua, kujipendekeza pia wanatumiwa na mafisadi, dr slaa tunamuelewa na kumkubali sana ivi mayage mayage amesikia matokeo ya uchaguzi uko mbeya vijijini?? Aaah kama hajui basi ajue tumechukua kijiji uko, natmai km anadhani anacapacity ya kutosha basi aanzishe icho chama aone mziki wake o/w aache mdomo anabwabwaja tu uyo.. Masab...li pia tokoilake lake....
 
Mayage mchumia tumbo anaishi kwa kutegemea makala halafu kwanini Jenerali Ulimwengu unampa Air Time mdwanzi kama huyu anaharibu gazeti letu makini, aendee kulekule Rai.
 
Ama kweli hili ni darasa tosha..mayage chukua notes, usome na kuelewa.
Next time ukirudia kupotosha itabidi uchapwe viboko hadharani..
 
dr slaa badili mifani... you can go deeper than that kwa ku refer hata nje ya tz

MTM

Kwa manufaa yako na wana JF Serikali yako imekabwa na wahisani kuhusiana issues hizo unazotaka Dr Slaa asizizungumzie. Kwa taarifa yako mambo hayo yote ndiyo kwanza yamepamba moto. Kikao kati ya serikali ya JMT na wahisani cha 24.6.2011 kilitoa action plan ya utekelezaji wa ufuatiliaji wa madeni ya EPA.

Taarifa ya sasa ni kuwa makumpuni kadhaa kama Ndovu Soaps,Bora Hotels and Appartments,Venus Hotels B.V.Holdings, VB Associates Kagoda Agricultre wamerudisha asilimia 100 fedha zilizofisadiwa. Jumla yote ni 70,725,425,541.39. Makampuni 13 hayajurudisha chochote.Kikao cha Troika kilitakiwa kukaa Taarifa ya kinachoendelea. Kwa taarifa ya wanaJF hata misaada inayopewa JMT iko conditioned kwenye matokeo ya EPA. Ndio maana narudia No Research no Right to speak.

Watanzania kweli wa ajabu, Wazungu wanafuatilia uwizi nchini kwetu sisi tunapiga porojo zisizo na tija. Alafu unaongelea maendeleo wakati hata hizo zilizorudi hujui zilirudishwa wapi. Maybe wanaobisha ni mafisadi au beneficiaries wa ufisadi.
 

Hapo kwenye red: Ni macho yangu au ndo ulivyoandika? Ulitaka ajibu kwa kuonyesha negative achievements??? Otherwise, asante kwa kuthibitisha yale aliyosema kuwa kuna positive achievements hivyo CHADEMA ni chama makini.
 
thank you very much dr. ninaamini hakuna executive leader wa ccm aliye na uwezowako na pia ambaye angejali kunijibu.

kama utafuatilia kwwnye ile thread waliyoweka makala yako, i called it "masterpiece".

lengo langu ni kukupa changamoto kwenye uchambuzi na ujengaji hoja uende beyond borders, mifano yote uliyotoa ina wenzake around the globe na ingekua vyema kuainisha na kuonyesha madhara, caveats au hata hao wezi/ mashetani walipofanikiwa ili tusiangukie kwenye takwimu

my message - goes beyond monotomy/repertition sometimes that you are used to: it was a constructive criticism coz we want a new horizon in our case studies, which in fact, ccm hawawezi kwa sasa labda wavue ngozi kabisa maana magamba yamewashinda [kuna kizungumkuti kinaendelea phillipines sijui watatokaje kutokana na viscious cycle ya ufisadi, we can learn alot), kuna ya thailand (thaksin na wenzake)

hitimisho, na wewe jifunze kuchukua challenges ppsitively, uliza kama hujaelewa na punguza povu na usiwe judgemental (alledgedly). Siwezi kuwa beneficiary wa epa uliza vijana wako wakuambie mimi nina msimamo gani kwenye hilo....na pia si mfanyakazi wala mdau wa serikali ya jamhuri ya muungano wa tanzania since march 29 2002, siku ya ijumaa [na sitegemei kufanya kazi kwa sasa kwani misimamo yangu inakinzana na watumishi wa serikali - mimi ni muwazi, siogopi na sio mnafiki]
 
Ahsante Dr. Slaa, majibu yako yanajitosheleza,yenye hekima na yenye uchunguzi wa kina.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…